Vinywaji vigumu: Tubadilishane maarifa na uzoefu

Abdulhalim

Platinum Member
Jul 20, 2007
17,193
3,011
Ok, heshima mbele wadau jamvini.

I feel compelled kuianzisha hii thread, pengine somewhere down the road wanajamvi tunaweza kuokota mawili matatu kuzilinda afya zetu kutokana na matumizi ya kilevi / kileo / vinywaji vigumu. Na ni wasaa wa wenye input kutujuza zaidi wanajamvi.

EFFECT YA MI-BIA KWENYE MENO/MIFUPA

Kwa sehemu niliyokuwepo ktk miaka miwili mitatu ilopita, gharama ya chupa ya maji na bia zilikuwa zikilingana, sasa unajua tena wabongo, kumaximize theory ya raha jipe mwenyewe nikawa nanunua zaidi bia kuliko maji na matokeo yake nilianza kuyaona baada ya kuona athari kwenye meno. Hii ikanikumbusha ndugu mmoja ambaye ni mnywaji sana na amepoteza meno kadhaa baada ya kutoboka na kumpa usumbufu, na kupelekea kuamua kuyang'oa baada ya jitihada za kuyaziba kuwa imefikia ukomo.

Nway, kwa uchunguzi wangu usio wa kitaalamu ni kuwa meno na mifupa yetu inajengwa kwa kiasi kikubwa na calcium, na ni imani yangu kuwa kwenye mibia hii kuna kemikali zinazopambana na calcium na kutengeza compund nyingine ambazo ni weak, na hivyo kusababisha meno kuwa easily eroded au abrased au mifupa kuwa dhaifu. Kwa hivi sasa binafsi kuna meno yamekuwa abrased kiasi kwamba nikipiga mswaki nasikia maumivu. (wenye utaalamu wasaidie hapa).


MADHARA YA WINE??

Baada ya kubaini madhara ya bia kwa meno yangu, ambayo nimeyashuhudia mwenyewe binafsi, nikaamua kuhamia kula wine, both white and red wine. Sasa majuzi hapa nimevuta wine flani hivi inaitwa Santa Ana kutoka Argentine imenifanya nijiulize maswali mazito. Baada ya kumaliza glass na nusu, nikachill kidogo. Wakati nakamua nikahisi kama kuna erosion kwenye ulimi, na kwa mbali nakawa nasikia ka-harufu flani hivi kama damu puani. Nilipoamua kwenda kuswaki ndo nikaona ulimi umebadilika rangi na mate nayo yamekuwa meusi..duh ikabidi nikimbilie maziwa kuikata hii sumu. Nashindwa kuelewa hii wine ni wine ya aina gani, au ni conco sulfuric acid?
 
Kwa hiyo hayo kwa maoni yako ndiyo madhara ya wine kwa afya siyo? Kaaz kwer kwer... Hiyo nadhani itakuwa wine feki ya Kichinachina...
 
Kwa hiyo hayo kwa maoni yako ndiyo madhara ya wine kwa afya siyo? Kaaz kwer kwer... Hiyo nadhani itakuwa wine feki ya Kichinachina...

Kiongozi,

SIwezi kusema mojakwamoja kuhusu hiyo wine ilikuwa authentic au la, maana niliinunua kwenye nchi ambayo ipo sirias na mambo ya bidhaa feki achilia mbali kuwa bidhaa yenyewe ni category ya 'chakula' na kwenye hiyo mall kuna continuos quality control ambayo binafsi nimeishuhudia mara kwa mara. Hivyo the speculation is open, in either way.


Nimejaribu tu kutoa mifano michache( sio yote) ambayo nimekumbana nayo binafsi. Kiukweli nakumbuka pia kupata sore throat kwenye tonsil na chini yake kidogo baada ya kunywa mvinyo mweupe ktk nchi moja ya kimediterania. Siwezi kusema as a total inference, lakini tatizo linaweza kuwa traced kuanzia hapo. Kumbuka matatizo mengi huhusiana na mpambano wa package na bidhaa, mabadiliko ya bidhaa kuendana na muda (kuelekea ku-expire) na matumizi ya preservatives na taathira yake pale preservatives zinapopambanishwa na bidhaa.
 
Mimi huwa najiuliza kila siku

wine
beer
whisky
rum
vodka
scotch
spirits

swali langu ni hili which is which?????
 
inawezekana ilikuwa feki auilikuwa imeeksipaya...............nakushauri kama wewe ni mtumiaji waukweli basi ujitahidi kufuatilia product identification criteria kutoka kwa manufacturer ili uweze kutofautisha orijino nafeki..................au acha kabisa kwani naamini ukiacha hutapungukiwa kitu kuliko ukiendelea na ukafanikiwa kupata matatizo.........
 
kama upo bongo jaribu local brew ukitaka inayofanana na wine tumia ulanzi,ukitaka inayofanana na lager tumia komoni,ukitaka inayofanana na whisky tumia mkangafu[ulanzi uliolazwa wiki moja na zaidi]
pombe zetu ni nzuri sana ila usitumie kiasi kikubwa sanaaaaaaa
 
inawezekana ilikuwa feki auilikuwa imeeksipaya...............nakushauri kama wewe ni mtumiaji waukweli basi ujitahidi kufuatilia product identification criteria kutoka kwa manufacturer ili uweze kutofautisha orijino nafeki..................au acha kabisa kwani naamini ukiacha hutapungukiwa kitu kuliko ukiendelea na ukafanikiwa kupata matatizo.........

Hivi vitu siyo rahisi kuacha kama unavyofikiri, BTW tunachangia uchumi wa Taifa Letu mahututi Tz
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom