Vinywaji, Sigara,Usajili wa Magari imekula kwao

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,314
33,108


4625274.jpg

Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustapha Mkulo
Katika bajeti ya mwaka 2010/11 iliyowasilishwa bungeni na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustapha Mkulo ilibainisha kuwa vinywaji, sigara na usajili wa vyombo vya usafiri vya moto vimepanda maradufu kwa asilimia 8. Hatua hiyo imekuja katika katika kuzinazingatia dhamira ya Serikali kukuza viwanda, ajira na mapato ya ndani.

Katika uainisho huo vinywaji baridi ushuru utapanda kutoka Shilingi 58 hadi Shilingi 63 kwa lita, bia iliyotengenezwa kwa nafaka ya nchini na ambayo haijaoteshwa itapanda kutoka Shilingi 209 hadi Shilingi 226 kwa lita, na bia nyingine zote ambazo nafaka hutoka nje ya nchi itatozwa kwa Sh 354 hadi Sh 382 kwa lita moja.

Mvinyo uliotengenezwa kwa zabibu kutoka nje ya nchi kwa kiwango kinachozidi asilimia 25 ushuru utapanda kutoka Shilingi 1,132 hadi kufikia Shilingi 1,223 kwa lita moja.

Na vileo vikali vitapanda kutoka Shilingi 1,678 hadi kufikia Shilingi 1,812 kwa lita moja.

Kwa upande wa usajili wa magari na pikipiki, ada ya usajili gari utatoka kwenye shilingi 120,000 hadi kufikia 150,000 na pikipiki kutoka 35,000 hadi kufikia Shilingi 45,000.
NIFAHAMISHE Tanzania news portal .: Habari za Tanzania :.
 
Kwa kuwa akina Mkulo et al wameamua walevi wachange fedha za kuendesha nchi mbona wameacha wangine kule Chibuku, Mbege, Ulanzi, dengelua, gongo (Local whisky) etc etc ....................


Ewe Mkulo mwana wa Mstapha a.k.a whatever .. Please be fair to us and bring up suplementary budget to cover the rest of us who you deliberately skipped in this malabuku budget. halafu uache kutembeza libakuli lako huko ulaya na marekani cause we boosers aka. walevi have all the money for this weaked budget.

The problem with you Mkulo is you have idea how much litres we consume per day , per week, per month , per year. It is 20 billions of litres fyi. What if you charge us 1000 sh. per litre per annum ? Simple calculation Mkulo bana come on . Do you need a Fake Masters Degree from Kuleee kutambua hili? Ebo.
 
Back
Top Bottom