Vincent Nyerere and Deo Filikunjombe

Kwa kweli tungekuwa na wabunge kama hawa kama kumi mawaziri wangenyooka. lakini pia lingine lililonikuna nikuwa eti tangu jana mawaziri wanalalamikiwa lakini hakuna hata mmoja alie jiuzuru.

Jambo lililo niuma ni lile la wanafunzi wanapigwa virungu kumbe hela zimeliwa na wakuu wa vyuo. Hongera sana Mhe, Filikunjombe kwa ujasiri Mungu akulinde sasa
 
Naona hoja nzito alizotoa Vicent Nyerere ni nzito sana kwa Chami na Deo Filikunjombe amegusa kwa Mkullo mwanachama mwenzake wa CCM

Kwa ujumla hawa jamaa wamenivutia sana kwa jinsi walivyokuwa wakiwasilisha hoja zao, nawapa big up sana & I really admires them so much!
 
Filikujombe amemaliza kila kitu, nafikiri wahusika wapime uzito wa tatizo na wachukue hatua.
 
Huyu Filikunjombe atakuwa anawafanyizia wenzake tu!! Maana CCM wana sera za "..mwenzetu" It is either kuna cut aliikosa au alibaniwa sana huko nyuma na anabanwa asifaidike!!

Magamba ni wanafiki, yeye kama anataka kujitenganisha aachie ngazi...
 
ccm hawana uwezo wa kumfukuza fili.kwani uwezo wa kurudisha jimbo hawana.2nataka wakina fili na milya sasa hivi 2015 hatutaki m2 kazi kwenu
 
[h=3]Deo Filikunjombe:Nimekukubali japo mimi siwapendi magamba.Nimekusikiliza tangia asubuhi na jioni hii kweli unadhamira ya kweli,ila huwezi kujifuta kwa kutumia taulo ukiwa ndani ya maji,ww ni mpiganaji mzuru na jasiri huko hakukufai chukua magwanda au kama hutaki magwanda nenda NCCR.[/h]

nadhani amekusoma!
 
Natamani nimtafutie Body guard maana hawakaii kuifupisha safari ya Mwanamwema Deo
 
Inaonesha amkuna kila aliyechangia japo sielewi alichosema . Nami nimfagilie kwa ujasiri wake kwa maslahi ya umma.
 
Filikunjombe asipoangalia yatamkuta ya Mwakyembe muda si mrefu... Anatakiwa kutoka kwenye lile Genge la wahuni.

Kweli, hawa jamaa ni bora kuwa nao macho sana, wanaweza kukumwakyembe. Safi sana Filikunjombe saidia kutoa uozo uliope, na wala usiope. Mwisho Anna kilango Mbona yupo kimya, maana alikuwa moto sanaa...au wamemsilence.
 
Safi sana Fili. Tunahitaji Wabunge kama hawa wenye uzalendo na nchi yao. Tulikuwa tunawachukia makaburu lakini leo wako wenye rangi moja na sisi na tunaishi nao(muone aibu). Filikunjombe tunakuombea. Fahamu dua la Kuku halimpati Mwewe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom