Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,138
Vilio, simanzi vyatawala kumuaga Jackline
na David Frank, Arusha
VILIO, simanzi na kwikwi jana vilitawala karibu nusu saa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Rufaa ya Selian, mjini hapa, huku baadhi ya waombolezaji wakizimia ovyo katika tukio la kuaga miili ya marehemu Jackline Minja (27) na mwanaye aliyetolewa tumboni kwa njia ya upasuaji baada ya kifo kilichotokana na kupigwa risasi na majambazi.
Marehemu Jackline aliuawa mwanzoni mwa wiki hii akiwa na ujauzito wa miezi nane ambapo madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya Selian walimfanyia upasuaji.
Vilio hivyo vilianza mara baada ya miili hiyo kutolewa nje ya chumba cha maiti na kulazwa nje huku mtoto huyo akiwa pembezoni mwa mwili wa mama yake.
Baadhi ya kina mama ambao ndio wengi waliokumbwa na hali hiyo walisikika wakigugumia na kulia huku wakihoji kwamba mtoto huyo alikuwa na kosa gani hadi auawe wakati hakuwa na hatia.
Mwili wa Jackline ulisafirishwa kwenda nyumbani kwao kwa mazishi katika kijiji cha Rawiya, Marangu Moshi.
Marehemu Jackline akiwa anaingia nyumbani kwake saa 3.30 usiku Jumanne iliyopita akiendesha gari aina Toyota Nadia T 125 AUW alivamiwa na watu wawili waliokuwa na pikipiki ambapo mmoja alimfuata upande wake na kuhoji alikokuwa mumewe Deo Minja ambaye ni mchimbaji wa madini katika mgodi ya Tanzanite Mererani wilayani Simanjiro.
Siku ya pili baada ya tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Basilio Matei, aliwaambia waandishi wa habari kuwa jeshi hilo limefanikiwa kuwaua kwa kuwapiga risasi watu wawili waliohusika na kifo cha Jackline. Aliwataja majambazi hayo kuwa ni Gilbert Charles (32) na Deus Dossa ambao waliuawa baada ya kurushiana risasi na polisi katika eneo la Soweto.
na David Frank, Arusha
Marehemu Jackline aliuawa mwanzoni mwa wiki hii akiwa na ujauzito wa miezi nane ambapo madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya Selian walimfanyia upasuaji.
Vilio hivyo vilianza mara baada ya miili hiyo kutolewa nje ya chumba cha maiti na kulazwa nje huku mtoto huyo akiwa pembezoni mwa mwili wa mama yake.
Baadhi ya kina mama ambao ndio wengi waliokumbwa na hali hiyo walisikika wakigugumia na kulia huku wakihoji kwamba mtoto huyo alikuwa na kosa gani hadi auawe wakati hakuwa na hatia.
Mwili wa Jackline ulisafirishwa kwenda nyumbani kwao kwa mazishi katika kijiji cha Rawiya, Marangu Moshi.
Marehemu Jackline akiwa anaingia nyumbani kwake saa 3.30 usiku Jumanne iliyopita akiendesha gari aina Toyota Nadia T 125 AUW alivamiwa na watu wawili waliokuwa na pikipiki ambapo mmoja alimfuata upande wake na kuhoji alikokuwa mumewe Deo Minja ambaye ni mchimbaji wa madini katika mgodi ya Tanzanite Mererani wilayani Simanjiro.
Siku ya pili baada ya tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Basilio Matei, aliwaambia waandishi wa habari kuwa jeshi hilo limefanikiwa kuwaua kwa kuwapiga risasi watu wawili waliohusika na kifo cha Jackline. Aliwataja majambazi hayo kuwa ni Gilbert Charles (32) na Deus Dossa ambao waliuawa baada ya kurushiana risasi na polisi katika eneo la Soweto.