WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 956
- Thread starter
- #41
Mkuu... uliberali per se siyo maendeleo for sure.Hilo liko wazi.kuna watu wanachanganya mambo wanachukulia uliberari mojakwa moja kuwa ni maendeleo bila kuzingatia mmomonyoko uliomo ndani yake.............. ...........
Neno kuntu kabisa hili! Iweje? ndicho haswa tunataka kujua....Mungu hakumuumba Mwanadamu awe Mpumbavu au Mjinga. Hatukushushiwa dini tulizonazo iwe ni mapokeo ya Uyahudi, Ukristo au Uislamu au hata dini zetu za Asili ili tuwe wanyonge.
Iweje leo Kasisi au Shekhe atoe mahubiri akilaani Wezi na Wanaohodhi mali huku yeye ni Mzinzi au ni ******?
"...religion is opium of the people",kwamba kwa imani za watu kama hata kama unaonewa na mabwanyenye,hutakiwi kurudisha "..just turn the other cheek..", ila nitofautine kidogo na mtoa maada,kwa heshima kabisa,si kuwa imani,mila na desturi ndizo zinazoduma maendeleo ya Waafrika,nataka hapa niungane na Marehemu Dr.Walter Rhodney, ambaye aliweka wazi kuwa kwa tamaduni za kiafrika zilivyokuwa karne ya 15 na 16,ziliwawezesha Waafrika kupiga hatua kubwa za kimaendeleo kwa wakati huo kuliko hata nchi za Ulaya,kumbuka hata mapinduzi ya viwanda yalikuwa bado Uingereza,tayari waafrika walikuwa na system nzuri za utawala...mfano tawala kama za Ghana, Mali, Timbuktu... Mwanamutapa, Congo, Zulu...Maghreb, zilishakuwa na hata mifumo ya taaluma na sayansi na hisabati ambazo wazungu walipokuja walizikuta mfano kama Algebra zilikuwa maarufu Afrika Magharibi kabla ya kuja wazungu.
Tamaduni za waafrika zilishika katika kazi na kujenga jamii miji na ustawi wa watu...kabila kama za Fulani,Tuareg...tamaduni za watu kama Nok zilishastawi katika teknolojia ya chuma na zana za chuma mbali sana kabla ya wazungu kutia mguu Afrika.
.
Sikatai kuwa kuna sehemu ya lawama kwa waafrika wenyewe kushindwa kutumia fursa ya kujitawala,walau kupunguza hizi legacy..kama alivyosema Prof.A.A. Mazrui "...pasingekua tatizo wakati nchi zetu zinapata uhuru viongozi wakakaa na kufikiria mifumo sahihi ya uwongozi kwa mujibu wa mazingira ya kiafirka,kama wangekaa wakafikiria tu tuwe na baraza la mji kama la mfalme wa Buganda, Wolof, Calabar, Ghana n.k...Badala yake tumekwenda mbali kutaka vyombo vyetu vya kimaamuzi viwe kama bunge la Cananada au WestminsterAbbey model.."
Ndugu yangu... nimeleta dimension hii ili tuichambue kwa undani kama tunavyofanya sasa... sikumaanisha kuwa traditions ( in its wider sense) na siyo tu mila, desturi na imani ndizo sababu za kutokupata maendeleo...
hiyo maroon ya mwisho yenye quote from Prof Ali Mazrui pengine ina mengi humo.... ungetuchambulia kwanini viongozi wali/wanashikwa na kugugumizi kutafuta models from the African good practices ( sipendi sana kutumia neno best practices maana huwa sijui best as compared to what!)
si kweli, nchi karibu zote za Kimagharibi, kimaadili na kimisingi zimejengwa kutoka katika Ukristu; nchi za Kiarabu na Kiislamu ambazo leo zimefanikiwa sana au zinapiga hatua ya maendeleo zinaongozwa na imani na desturi zao, hilo laweza kusema pia kuwa ni kweli uko Uchina, Japani, na India!
Ni Afrika tu ambapo hatutaki kukubali kuwa na sisi tuna desturri na mila zetu ambazo tunaweza kuzitumia kuchochea maendeleo. Tunaamini maendeleo ni pamoja na kukumbatia desturi na mila za wageni!!
Mila na desturi zetu si kikwazo cha maendeleo; mila na desturi za wageni zawezekana kuwa ndiyo kikwazo!
Nakubalina nawe Mkuu kuwa kuna uwezekano mkubwa sana kutumia traditions kuchochea maendeleo..... na hata kwa kuangalia trend utaona pattern ifuatayo:
Nchi zile zenye traditions kwa kiwango cha kati na viwango vya kuridhisha vya liberalism ( mfano Christian Europe kama Ujerumani, Uingereza etc ) wana maendeleo makubwa.Nchi zenye kukumbatia sana traditions mila bila imani za kidini bila kujali haki za binadamu kama Zimbabwe sihitaji kuhitimisha.Nchi zenye kujali traditions kwa saaana kwa maana ya imani za kidini bila kujali sana haki za binadamu kama tunavyozijua wengine ( mfano nchi za kiarabu) nazo zina maendeleo.Halafu kuna zilizo moderate nazo utaona ziko katika kati hazin extremes......
TX! U can say that again.Mungu ain't got nothing to do with development. Development is brought about by the people and for the people.
I agree with this part absolutely!My sentiments, although I would also say when people put too much faith in god they tend to neglect their own roles in the attainment of development.
The more a society believes in god, the more backward it is bound to be.
Just look at Atheist/ non-religious northern Europe na evangelical west Africa.
Angalia attendance za kanisani ulaya na Africa, halafu angalia pattern za maendeleo ya kiuchumi.
.
Mwana fa...
Lugha ni muhimu ikatangulia kwanza.
halafu umuhimu wa lugha yako ni kuwa
utaweza kujiajiri na sio kusuburi kuajiriwa...
imagine wahandisi wa majengo na barabara na madaraja
na madaktari na wafamasia wenye uwezo wa kutengeneza madawa n.k..
tutajitosheleza wataalam na tutajiajiri wengi na tata dominate the region.
dunia nzima kuna upungufu wa madaktari kwa mfano na wana taalumazingine.
na kama daktari wa upasuaji wa moyo kwa mfano huitaji kujua kiingereza
sana zaidi ya mawasiliano tu.
madaktari waliojifunza udaktari kwa kihispania wanafanya kazi
katika nchi zinazotumia kiingereza,right now as i am speaking....
Hii nayo ni dimension nyingine worthy exploring.