Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,001
- 112,636
nataka hapa niungane na Marehemu Dr.Walter Rhodney, ambaye aliweka wazi kuwa kwa tamaduni za kiafrika zilivyokuwa karne ya 15 na 16,ziliwawezesha Waafrika kupiga hatua kubwa za kimaendeleo kwa wakati huo kuliko hata nchi za Ulaya,kumbuka hata mapinduzi ya viwanda yalikuwa bado Uingereza,tayari waafrika walikuwa na system nzuri za utawala...mfano tawala kama za Ghana, Mali, Timbuktu... Mwanamutapa, Congo, Zulu... Maghreb, zilishakuwa na hata mifumo ya taaluma na sayansi na hisabati ambazo wazungu walipokuja walizikuta mfano kama Algebra zilikuwa maarufu Afrika Magharibi kabla ya kuja wazungu.
This has got to be one of the most ridiculous claims ever..that we (Africans) were more developed than Europe during the 15th and 16th centuries.
Huyo Rodney wenu hoja zake zimejikita ktk kutokujionesha kuwa duni ilhali hali halisi inapingana na hoja zake. Haingii akilini eti tulikuwa tumeendelea zaidi au tulikuwa sawa kimaendeleo halafu wao (wazungu) wakaja wakatulostisha na tokea hapo hatuja recover kabisa. This makes no sense.
Wakatuletea dini na sisi tukazikumbatia. Wakatuletea so called ustaarabu na sisi tukaukumbatia. Wakatuletea lugha tukazikumbatia. Wakatuletea elimu tukaikumbatia. Wakatuletea mambo mengine lukuki (likiwemo kulana denda-french kiss) na sisi hao kichwa kichwa tutayakumbatia. Juu ya yote hayo wakaja wakatutawala kimabavu. Wakagawiana bara letu kama vile ni mali yao binafsi, na sisi tulivyo wajinga tukakaa tu tukiwatazama na kuwasubiri.
Sasa mtu eti aje na hoja ya kudai kuwa tulikuwa sawa au kuwazidi kimaendeleo mimi nitamwona kachanganyikiwa tu. Maendeleo ni pamoja na kuamka kifikra na kuwa mwerevu. Sasa ni maendeleo gani hayo tuliyokuwa nayo wakati wenzetu walikuwa werevu zaidi kutushinda sisi?