Wana JF nawaslimu. Nimeishi na mke wangu kwa miaka 33 sasa na tumebahatika kuwa na watoto na wajukuu kadhaa. Kama miaka 5 iliyopita mke wangu alianza kupata vipele ukeni hadi kufanya ule mchezo wetu wa faraghani usiwezekane. Tumeenda hospitali tatu tofauti kwa vipimo. Nyakati zote ameambiwa mkojo wake ni mchafu na kupewa dawa. Ingawaje mimi sikuonekana na tatizo nilishauriwa nami nitumie dawa hizo kwa tahadhari na nikafanya hivyo. Miaka mitano ni mingi vipele ikawa siyo vipele tena ila ni vijipu. Mke wangu akisafiri mahala pa kukaa kiasi cha wiki mbili hivi vijipu ukeni vinapotea kabisa. Akinuia tu kurudi nyumbani niliko vijipu vinaanza usiku huohuo kiasi kwamba akifika nyumbani vijipu viko palepale na ile kazi haifanyiki. Nilifanya kama kumvizia akiwa kule mbali nikamkuta ni mzima wa afya. Kama nimefika asubuhi haifiki saa nane tayari vijipu vimeanza.
Nimehangaika hata kienyeji hakuna mafanikio. Naamini hapa jamvini kuna wataalaam wa fani zote. Naomba kujua ni ugonjwa gani huu ambao hauniambukizi mimi?. Na tiba ya ugonjwa huu ni nini?
Nimehangaika hata kienyeji hakuna mafanikio. Naamini hapa jamvini kuna wataalaam wa fani zote. Naomba kujua ni ugonjwa gani huu ambao hauniambukizi mimi?. Na tiba ya ugonjwa huu ni nini?