Vijimambo vinavyotokea kwenye Daladala

Al-Mende

Member
Apr 14, 2011
77
11
WAKATI MWINGINE DALADALA
INARAHA ZAKE,KWA WALE WENYE
MAGARI NA AMBAO HAMPANDI
DALADALA...HIVI NDO VIOJA
TUNAVYOPATA WENZENU
BARABARANI! Mlokole: "Nyimbo gani
mnapiga?!? Wekeni
nyimbo za Yesu.."
Konda: "Vipi wewe, Yesu
... bado hajatoa album..."
******************************** Abiria: "Kuna Kiti au
unasema panda tu!?"
Konda: "hao wengine wamekalia
ndoo?! "
*******************************
Abiria: "Embu punguzeni sauti ya redio..."
Konda: "Sheria za nchi tu zinatushinda,
tusikilize
na zako!? hebu tupunguzie misheria"
*******************************
Mmama: "Bwana ondoa gari joto sana!!"
Konda: "Usituzingue wewe, shuka
upande fridge...."
******************************
Konda: "Anti, kuna siti pale nyuma,
ingia...." Anti: "Siwezi kaa siti za
nyuma..."
Konda: "Kwenda zako
wewe, Kwani za nyuma ziko nje ya
gari?!"
******************************** Sister duu: "Konda
unanibana bwana..."
Konda: "mbona nguo ulizovaa
huzisemi, kama ulitaka kujiachia
ungekodi treni
peke yako!!!" *******************************
Sharobaro: "Kuna kiti?!
Kama hamna sipandi..."
Konda: "Kama unaogopa kukosa kiti si
ungebeba chako!!?"
 
Yaah! hiyo ndo daladala bwana. Mimi kila siku huwa nafika kazn natabasam, jioni nafika nyumbani natabasam sababu ya maneno ya kwenye daladala.
 
thanx for this mkuu maana wengine tunausafiri wa kazini kwa hiyo tunamiss vitu hivi!
 
haya bwaba tumeona na hii ni kawaida tuu kwa wale amboa walisha zoea matusi....
 
Searching...100%
Loading...100%
Network Connected !

Konda: Mna shuka ?
abiria: Hapana ! tuna blanketi.
 
Back
Top Bottom