sir.JAPHET
JF-Expert Member
- May 18, 2012
- 699
- 133
Nora Damian
DIWANI wa Kata ya Vijibweni,wilayani Temeka, Seleman Mathew ,ameiomba Serikali kufanya upya tathmini ya mradi wa ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni, ili kuwatendea haki wananchi.Alisema mwaka 2008 Serikali ilitoa amri kwa wakazi wa eneo hilo kutoendeleza makazi yao.
Akizungumza baada ya kukabidhi vifaa vya ofisi kwa ajili ya ofisi ya Kata ya Vijibweni, Mathew alisema baada ya amri hiyo kwisha wananchi wengi walianza kuendeleza ujenzi wa nyumba zao.
Wananchi wanautaka mradi lakini kuna haja ya wao kushirikishwa katika kutoa maoni yao ili mradi huo uweze kufanikiwa,alisema Mathew.
Diwani huyo alikabidhi vifaa vya ofisi ikiwemo kompyuta moja, saa na kuweka umeme katika ofisi hiyo na vitu hivyo vyote vimegharimu Sh2.3 milioni.
Mmoja wa wananchi wa eneo hilo, Zainabu Fatawi, aliiomba Serikali ijipange upya na kwenda kukutana nao kwa sababu amri iliyotolewa tayari ilishapitwa na wakati.Hakuna ambaye hapendi maendeleo lakini wanapokuja waanze tathmini upya kwa sababu watu wameshajenga,alisema Fatawi.
Katika hatua nyingine, diwani huyo alisema anakusudia kukutana na kampuni zinazojishughulisha na na biashara ya mafuta katika eneo hilo, ili kuzitaka zichangie shughuli mbalimbali za maendeleo.
DIWANI wa Kata ya Vijibweni,wilayani Temeka, Seleman Mathew ,ameiomba Serikali kufanya upya tathmini ya mradi wa ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni, ili kuwatendea haki wananchi.Alisema mwaka 2008 Serikali ilitoa amri kwa wakazi wa eneo hilo kutoendeleza makazi yao.
Akizungumza baada ya kukabidhi vifaa vya ofisi kwa ajili ya ofisi ya Kata ya Vijibweni, Mathew alisema baada ya amri hiyo kwisha wananchi wengi walianza kuendeleza ujenzi wa nyumba zao.
Wananchi wanautaka mradi lakini kuna haja ya wao kushirikishwa katika kutoa maoni yao ili mradi huo uweze kufanikiwa,alisema Mathew.
Diwani huyo alikabidhi vifaa vya ofisi ikiwemo kompyuta moja, saa na kuweka umeme katika ofisi hiyo na vitu hivyo vyote vimegharimu Sh2.3 milioni.
Mmoja wa wananchi wa eneo hilo, Zainabu Fatawi, aliiomba Serikali ijipange upya na kwenda kukutana nao kwa sababu amri iliyotolewa tayari ilishapitwa na wakati.Hakuna ambaye hapendi maendeleo lakini wanapokuja waanze tathmini upya kwa sababu watu wameshajenga,alisema Fatawi.
Katika hatua nyingine, diwani huyo alisema anakusudia kukutana na kampuni zinazojishughulisha na na biashara ya mafuta katika eneo hilo, ili kuzitaka zichangie shughuli mbalimbali za maendeleo.