Ndugu wanaJF, nimekuwa nikifikiria kwa nini baadhi ya vijana wanaamua kushusha suruali zao nusu makalio na kuonesha nguo zao za ndani na wanaona sifa kufanya hivyo. Wengine wanakuwa wanajifanya wanasogeza juu lakini wanairudisha palepale. Huwa najaribu kujiuliza: hivi maana ake ni nini - ni ushoga au? Nasema hivi kwa sababu nakosa neno sahihi la kutumia hasa kwa kuzingatia kuwa kama wangekuwa ni wasichana wanavaa kiaina unakuta watu wengine wanawaita malaya au "wako kwenye biashara hao!" Ila kwa wavulana sijasikia mtu yeyote akiwaita majina mabaya. Je, hii staili ya uvaaji ni ya heshima? Kama siyo mbona haikemewi lakini wasichana wakivaa kwa namna tofauti tunakuwa wa kwanza ku'label'?