Ni Mimi Msiogope
JF-Expert Member
- May 28, 2012
- 352
- 200
WAPUUZI MOvement ni jina la kushangaza lakini pia linastaajabisha mtu kujiita hivyo!...
Juzi Alhamisi asubuhi nikiwa nasikiliza Radio Passion FM ofisini kwangu nilishangaa kusikia vijana wanne wakiwa kwenye studio hiyo wajifafanua maana ya WAPUUZI MOVEMENT...Nilicheka japokuwa baadaye na mimi nilijiona ni MPUUZI!..
Lengo lao kubwa ni kukusanyana kwa ada ya shilingi 10,000 kila mmoja kwa vijana 1000 ambapo wanalenga kukusanya jumla ya 10,000,000/= na kutengeneza filamu (Kwa kuanzia)... Baada ya kuuza hiyo filamu wanatarajia kupata 100,000,000/= ambapo watafanya miradi mingine yenye ajira kwao...
Wameamua kujiita wapuuzi kwa kuwa wamepuuzwa na Serikali na kutokupatiwa fursa za ajira au Mikopo yenye Tija... Walikaribisha wanachama kwa kuwa hadi sasa wamefikia wanachama 700 kwa hiyo bado wanachama 300. Huo ni mwanya na fursa kwa vijana wengine kuungana nao au kubuni kitu kitakachozalisha ajira. Mwenyekiti wao niliyekumbuka jina lake ni Deus Amani na vijana wengine Katibu wao na viongozi wengine.
Nimeona niwajulishe hapa jamvini ili tuone namna gani tunaweza kuungana nao au kuwashauri,
Juzi Alhamisi asubuhi nikiwa nasikiliza Radio Passion FM ofisini kwangu nilishangaa kusikia vijana wanne wakiwa kwenye studio hiyo wajifafanua maana ya WAPUUZI MOVEMENT...Nilicheka japokuwa baadaye na mimi nilijiona ni MPUUZI!..
Lengo lao kubwa ni kukusanyana kwa ada ya shilingi 10,000 kila mmoja kwa vijana 1000 ambapo wanalenga kukusanya jumla ya 10,000,000/= na kutengeneza filamu (Kwa kuanzia)... Baada ya kuuza hiyo filamu wanatarajia kupata 100,000,000/= ambapo watafanya miradi mingine yenye ajira kwao...
Wameamua kujiita wapuuzi kwa kuwa wamepuuzwa na Serikali na kutokupatiwa fursa za ajira au Mikopo yenye Tija... Walikaribisha wanachama kwa kuwa hadi sasa wamefikia wanachama 700 kwa hiyo bado wanachama 300. Huo ni mwanya na fursa kwa vijana wengine kuungana nao au kubuni kitu kitakachozalisha ajira. Mwenyekiti wao niliyekumbuka jina lake ni Deus Amani na vijana wengine Katibu wao na viongozi wengine.
Nimeona niwajulishe hapa jamvini ili tuone namna gani tunaweza kuungana nao au kuwashauri,