kupelwa
JF-Expert Member
- Aug 24, 2011
- 1,087
- 450
na Mwandishi wetu
BAADHI ya vijana wanaowania uongozi kwenye Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wamelalamikia vitendo vya kuwabeba baadhi ya wagombea.
Wakizungumza na Tanzania Daima kwa masharti ya kutotajwa majina yao walisema miongoni mwa rafu hizo ni kampeni zilizoanzwa kufanywa na wenzao kinyume cha taratibu za umoja huo.
Walisema walianza kampeni hizo kwenye sherehe za Idd Pili zilizoandaliwa na Mbunge wa Ukonga, Eugene Mwaiposa (CCM) aliyewaalika baadhi ya wajumbe kwenye fukwe moja iliyopo Kawe jijini Dar es salaam.
Walisema katika sherehe hiyo wagombea hao (majina tumeyahifadhi) ambao wanawania uenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Ilala na unyekiti Mkoa wa Dar es Salaam walimwaga sera zao wakiomba wajumbe watakaoingia kwenye vikao vya maamuzi mkoani na wilayani wapitishe majina yao.
BAADHI ya vijana wanaowania uongozi kwenye Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wamelalamikia vitendo vya kuwabeba baadhi ya wagombea.
Wakizungumza na Tanzania Daima kwa masharti ya kutotajwa majina yao walisema miongoni mwa rafu hizo ni kampeni zilizoanzwa kufanywa na wenzao kinyume cha taratibu za umoja huo.
Walisema walianza kampeni hizo kwenye sherehe za Idd Pili zilizoandaliwa na Mbunge wa Ukonga, Eugene Mwaiposa (CCM) aliyewaalika baadhi ya wajumbe kwenye fukwe moja iliyopo Kawe jijini Dar es salaam.
Walisema katika sherehe hiyo wagombea hao (majina tumeyahifadhi) ambao wanawania uenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Ilala na unyekiti Mkoa wa Dar es Salaam walimwaga sera zao wakiomba wajumbe watakaoingia kwenye vikao vya maamuzi mkoani na wilayani wapitishe majina yao.