Vijana wakati wa kulalamika umepita tuchukue maamuzi

Joblube

JF-Expert Member
Mar 4, 2011
369
151
Juzi katika Kongamano la kumuenzi Mwalimu Nyerere, viongozi wa zamani akiwapo Jaji Warioba alishauri kuwa vijana tuache kulalamika tuchukue maamuzi na kuamua kutenda nami nakubaliana naye mia kwa mia. Katika nchi yeyote mabadiliko huletwa na vijana ikiwa jamii husika iko tayari au la. Na Tanzania yetu ya leo mabadiliko ya kweli yataletwa na vijana. Ni ukweli uliodhihiri kuwa maendeleo ya Tanzania hayawezi kuja chini ya CCM lije jua au mbalamwezi. Mtoto aliyelelewa kifisadi atafikiri kifisadi na kutenda kifisadi ndio maana wanarithishana majina yale yale tazama kuna J. Makamba, N. Mnauye. H. Mwinyi, Kipi Warioba,R. Kwikwete n.k.Hawa wote ni mvinyo wazamani kwenye chupa. Hawawezi kuwa na jipya katika kupambana matatizo yetu hawayajui kwanza wamesoma nje hawajui matatizo ya shule zetu kuwa pale mlimani wenzao tulikuwa tunalala mzungu wanne.

Ni ukweli ukombozi wa nchi yetu utaletwa na vijana nishauri vijana wote tuamue kuwa sasa basi kila kijana ahakikishe kuwa anakitambusho cha kupigia kura na kama hana wakati ukitimia wa kujiandikisha kila kijana ajiandikishe na afanye kwa nafasi yake kuelisha umma juu ya madhara ya kuendele kutawalwa na CCM tusiendeleze janga la kitaifa.

Tuachekulalamika tuchukue hatua.

Mungu Ibariki Tanzania
 
Ni dhahiri kabisa kwa watanzania hasa vijana kulalamika hali ya maisha ni ngumu kutokana na kutokupea uwezo na fursa za kuwafanya wajiendeleze kimaisha, lakini tatizo bado lipo kwetu sisi vijana, ambao tunauwezo wakuleta mabadiliko ya hii nchi lakini tumeridhika na umaskini na ufukara na kuwaacha wengine wakiishi maisha ya anasa yanayotokana na nguvu kazi yako na kupumbazwa kwa kutopewa uwezo wa kuelewa.
KIJANA badilika na kuhamasika kwa kuchagua viongozi wakukuongoza kwa kutumia fursa yako ya kupiga KURA sio unalala tu.
 
tukichukua maamuzi magumu mnatubiga mabomu mfululizo -ccm nyie mbona vigeugeu sana? (Taking into consideration kauli hii imetokewa na Kada mzoefu / msaafu wa chama chenu).
 
Back
Top Bottom