Vijana wa Vyuo vikuu wanaCCM waandamana kuunga mkono JK kuvunja baraza la mawaziri!

wameletwa na roli hadi pale maeneo ya fire ndo wakashushwa. kwa aibu wakaanza kukunjua vikaratasi vyao walivyo andika upuuzi. kwanza wenyewe walikuwa wanaona aibu walivyo kuwa wanazomewa na wamachinga. Walio wengi hawakufika rumumba.
 
Mimi ninashindwa kuelewa hivi kila mtanzania ni lazima aipende Chadema? Maana nimeona post zote mtu akiwa tofauti na Chadema basi atashambuliwa kwa matusi,kebehi na kila neno la dharau jamani wanabodi mfumo wa vyama vingi unaturuhusu kutofautiana kwa hoja bila kupigana,hivi mtu akieleza hisia zake kuwa anaipenda CCM basi liwe ni kosa? Tujifunze kuwa wavumilivu ikiwa mmoja wetu hapendi kile wanachokipenda watu wengine! Na hakuna haja ya kuitana majina yasiyofaa inaonekana watu hawako tayari kufanya siasa za kiustaarabu tujirekebishe.

Hemed; Ni kweli humu JF kuna hali kama hiyo uliyoigundua. Lakini kumbuka hizi chuki zinatokana na hasira za maovu mengi yanayofanywa na viongozi wako wa magamba. Wizi wa kodi zetu umekithiri lakini mmekuwa mkilindana hadi watu wapige mayowe ndio mna2pa viinimacho. Magamba na nyie mmekuwa na chuki mbaya sana kwa wafuasi wa vyama vya upinzani hadi mmefikia mnaanzisha mauaji (Hii ni chuki mbaya zaidi kuliko haya matusi unayoambulia humu JF).
 
hawajui nini wanakifanya haiwezekani kupongeza jambo lililo kwenye mabano je, akiwachateua walewale kwenye wizara nyingine watasemaje??
 
Inatia aibu kwa kweli...
kuna kama vijana kumi hivi wameandamana eti kuunga mkono jitihada za serikali za JK kupangua baraza la mawaziri na kupokelewa na Vuvuzela la ccm Nape
Kwa harakaharaka ukiangalia ni kama kichekesho lakini vilevile ni aibu kwa vijana kuandamana kupongeza wajibu wa mtu! hawaoni kama huyo Jk ndiyo kikwazo kwa utendaji na ustawi wa nchi hii na ni aibu kwa yeye kuteua watu ambao mwisho wake wanakuwa waizi wa rasilimali za nchi hii!
Shame on you vijana kama kmi mlioandamana!

Waandamanaji halali hawakua kumi walikua tisa mkuu.
 
Jaman msiwalaumu hali ya vyuoni ni mbaya, bumu haitoshi ndo mana utakuta kuna wanafunzi wanajiuza mili yao,. Ko hawa wametumia haki yao kuuza utu naelimu yao kwa nape kuepusha j2 ya leo kushindia mihogo,. Kama umemwona rafiki ako shauri mwambie elimu yake ni kubwa kuliko hata ya nape,.iweje azalilishwe hivo
 
Leo mchana nape amepokea maandamano ya wale wanaojiita Wana cccm wa vyuo vikuu,lengo Lao ni kupongeza Kamati kuu.(source Chanel ten)
Haiwezekani na ni vigumu kuamini kwamba bado kuna wasomi vyuoni ambao wanaweza kupoteza muda wao kwa ajili ya kuunga mkono ubadhirifu unaofanywa na mawaziri wa jk,

hata vyuo vikuu mahanithi wapo. we amini tu.
 
Maandamano ya NAPE, kaya anzisha mwenyewe na kuyapokea mwenyewe.

Hovyoooo!
 
idadi yao ktk hayo maandamano ni ndogo mno ukilinganisha na vijana walioko vyuoni hii ni ishara kuwa CCM inakufa.
 
Sheria ya Vyuo vikuu ya inakataza kabisa suala la vyuo kujihusisha na mambo ya siasa, hao vijana wameandamana wakitokea chuoni au wamejikusanya nje ya chuo. kama ni kutokea chuoni hao na chuo chao inapaswa wachukuliwe hatua kwa kuingiza siasa mahali pasiporuhusiwa. Huu sio wakati wa kujipendekeza, ila tujue hata afae hakosi wa kumsindikiza...
 
nafikiri hawajajua wanachikifanya,ngoja wamalize maandamano njaa itawauma wanafikiri kwa kumfurahisha mwenyekiti wao wataongezewa posho za mkopo.
 
Back
Top Bottom