Vijana wa Tanzania wanaweza kuleta revolution?

Capital

JF-Expert Member
Oct 12, 2010
1,452
1,038
WanaJF salaam aleiqum

Nimekaa nikafanya taftishi ndogo tu nikagundua kuwa ili mabadiliko yatokee, lazima uwepo mtafaruku hapa Tanzania, tena mkubwa, kupindukia ule wa Libya. Kama watu wa Libya na kwingineko, walisubiri mabadiliko, awali wakidhani maneno ya wanaharakati na wanasiasa yanaweza kuleta mabadiliko, lakini kinyume chake, hali ilikuwa vile vile miaka nenda, miaka rudi. Ndipo wakaamuwa kuchukuwa maisha yao mikononi mwao, kuondoa ushetani (tyrany) uliokuwa umedumu nchini kwao. Kwa upande wetu huku, tutasubiri sana, kwani uzoefu umeonesha kwamba revolution (ambayo mara nyingi huhusisha conflict/strugle) ndiyo option sahihi. Sasa swali, je watanzania wa sasa hasa vijana ambao mustakabal wa maisha yao ni sintofahamu wako tayari kuingia katika revolution? revolution ya maana, ya kuondoa takataka nchini mwetu once and for all? Pia, je vijana wako tayari kuendesha pick-ups kama wale vijana wa Libya kung'oa hawa manyani? naomba tujadili.

Capital
 
Back
Top Bottom