Vijana wa Shamba - Uaminifu

Dijina40

JF-Expert Member
May 17, 2010
727
242
Nimetafuta nimechoka. Ninaowapata wote wazuri wiki 2 - 4 za mwanzo baadae wanageuka wezi. Wameniibia miaka 2 yote nimekuwa na-invest shambani bila kupata kitu, mayai wanauza, kuku wanauza, vifaranga wakishachangamka wanauza. Shamba ni la wanyama hasa kuku na kanga. Nguruwe niliwaondoa baadae nitaweka tena. Nimejaribu kutoa hadi nyumbani kijijini interior, wakifika wazuri wiki 3 baadae wakishasalimiwa na vijana wa vijiweni wanageuka wezi tena hao ndugu wamekuwa wabaya kuliko watu baki. Vijana wa shamba wanaojituma na kufanya kazi kwa uaminifu wanapatikanaje? Shamba liko nyuma ya Wazo Hill kuleee alikokuwa akikaa marehemu Waziri Mkuu wetu wa zamani.
 
Digina nimegundua tatizo lako huwalipi vizuri na huwathamini kama wafanyakazi.
Wewe mwenyewe umeajiliwa ukiwa huthaminiwi na mshahala kiduchu lazima umwibie mwajili wako.
Tangaza dau nikuletee vijana watiifu na waaminifu ambao hawatashawishika.
 
Nashukuru kwa maelezo yako Fidel. Mshahara wangu huanzia elf 75 kwa single vijana, waliooa huwa naongeza dau kulingana na umri wao. Nawathamini sana, labda inategemea matarajio ya kuthamini na kuthaminiwa yakoje tunayachukuliaje. Wanapata vyumba vya kuishi, kitanda na godoro na neti na vifaa vyote vya kupikia na vya jikoni. Zana za kufanyia kazi zote zipo, mazao wanayolima shambani nawaachia. Kama wanalima bustani sifuatilii wanapouza hela wanazopata, nahesabu ni nyongeza yao binafsi ili wasipende kwenda kwenye vibarua na kuacha shamba bila mtu. Mahindi na mihogo wanayolima nachukua kidogo ya kuchoma na kuchemsha tu ninapokwenda shambani, nawaachia watumie kama chakula chao badala ya kununua ama wakipenda kuuza kujiongezea kipato. Nadhani nawathamini saaaaana ndio maana hujisahau wakauza kila kitu???. Inawezekana nilikoajiriwa sithaminiwi, lakini binafsi sijagundua hivyo. Najiona ninayethaminiwa sana na mwajiri wangu.
 
Kaka Filel, nature ya kazi yangu haina mwanya wowote wa kumwibia mwajiri, hata muda labda nichelewe kidogo tu kuja kazini kutokana na foleni vinginevyo, sina cha kuiba kuanzia kalamu, karatasi n.k. Nachapa mzigo nasubiri mshahara na allowance zangu halali. Thanks.
 
dada dg kwa maelezo uliyotoa kama ni kweli watuuliokuwa unapata wana shida lakini kwa vile hatuwezi kujua upande wa pili wa shilingi.ongea na jamaa wa mbeya wakutafutie wasafwa hapo utatulia
 
dada dg kwa maelezo uliyotoa kama ni kweli watuuliokuwa unapata wana shida lakini kwa vile hatuwezi kujua upande wa pili wa shilingi.ongea na jamaa wa mbeya wakutafutie wasafwa hapo utatulia

hapo umenena, wasafwa au wanyalu, ila usiwapunje mshahara hata mwezi mmoja, ukiwacheleweshea tu wanaanza kuwa na mawazo mbadala. tradition zao hasa wasafwa huwa ni za heshima na uaminifu wa aina fulani ivi.
 
Nashukuru sana kwa ushauri wenu. Huwa sipunji mshahara wa mtu. Nikipokea mshahara wangu mwenyewe hatua ya kwanza huwa nalipa mishahara ya watu wanaonifanyia kazi kabla ya chochote. Kwa kweli sina nililoongeza wala kutia chumvi katika niliyoandika. Sielewi tu tatizo ni nini? Shamba pia liko njiani kwa hiyo ni sehemu yenye ushawishi. Vibosile wanapopita na magari yao wakiona kuku na kanga wamesambaa shambani wanapaki wanawashawishi kuwauzia na hela mkononi. Lakini si wote wanaokubali kurubuniwa. Kwa sasa nilikuwa na kijana toka nyumbani kabisa, amekaa mwaka 1 jana kaniambia amechoka kazi ya kuku anataka kubadili shughuli. Kawaida huwa napendelea kuwa nao 2. Nitafuata ushauri wenu. Kazi njema.
 
Digina nimegundua tatizo lako huwalipi vizuri na huwathamini kama wafanyakazi.
Wewe mwenyewe umeajiliwa ukiwa huthaminiwi na mshahala kiduchu lazima umwibie mwajili wako.
Tangaza dau nikuletee vijana watiifu na waaminifu ambao hawatashawishika.


Unampa uhakika gani endapo wataiba-utamrudishia kilichoibiwa?Ni hatari hawa!hata gari wanaleta majambazi yanakuua yanachukua na wanatokomea.Bora hao wanaliiba mali, wengine wanaweza hata kukuibia vya ajabu.Hili dau lisije likakupoteza ndg yetu Fidel80
 
hapo umenena, wasafwa au wanyalu, ila usiwapunje mshahara hata mwezi mmoja, ukiwacheleweshea tu wanaanza kuwa na mawazo mbadala. tradition zao hasa wasafwa huwa ni za heshima na uaminifu wa aina fulani ivi.
Mimi mke wangu ni msafwa lakini tunaajiri wachaga-sijawahi kuona watu waamiminifu kama hawa jamaa nilionao.
Dada yangu-ukishindwa kupata watu wa uhakika ni PM nikutafutie watu-uaminifu sio kabila wala dini.
La mwisho wewe ni wa TZ tunaowataka -kama ni kweli,mpaka unapata nguvu za kudirki kusema huibi hata muda wa muajiri?HONGERA!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom