SAYANSIKIMU
JF-Expert Member
- Feb 27, 2014
- 1,132
- 260
Siku hizi imekuwa kawaida kwa baadhi ya vijana wanapokuwa mashuleni wanatafuta wasichana baada ya hapo wanawapa mimba na akigundua aliyefanya nae mapenzi ana mimba basi msichana huyo anatelekezwa.Imekuwa ni tabia ya vijana na hata baadhi ya wababa kutia mimba na kutelekeza msichana aliyempa mimba.Tatizo linakuwa kwa hawa watoto wanaozaliwa.Watoto hawa wakati mwingine wanakuwa na maisha magumu wanaishia kula mabaki au makombo kwenye mashule mbalimbali ya serikali.Huwa najiuliza mtu anajua kabisa hana uwezo wa KUTUNZA MTOTO lakini hilo hajali anafanya mapenzi na kupeana MIMBA na huyo mtoto aliyezaliwa anabaki kuhangaika,.Mtu unajua kabisa uwezo wa kulea huna kwa nini sasa ufanye mapenzi? .Kwani usipofanya mapenzi utakufa.Wengine utakuta wanawatoto lakini wapo kwa wazazi wao .Ingekuwa kama kweli wana akili wafanyapo mapenzi wawe wanatumia uzazi wa mpango kuzuia mimba zisizo tarajiwa lakini hawajali hilo wanataka hivihivi.Wahusika mjirekebisha.Najua baadhi yenu wahusika mtauchukia huu ujumbe .Vijana mjerekebishe