Rihanadiya
New Member
- Jun 14, 2012
- 1
- 0
Nimekuwa nikifatilia maisha ya watoto waishio mitaani kwa muda mrefu sasa na kujikuta nikijiuliza maswali mengi ambayo kwa nyakati tofauti nimekuwa nikikosa majibu juu ya hawa watoto na serikali kwa ujumla. Wimbi la watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu limekuwa likiongezeka siku hadi siku kwa chanzo kinachosemekana ni ugumu wa maisha wanaopata kutoka katika familia zao na wengine ni kutokana na malezi mabaya wanayoyapata toka kwa wazazi wao. Lakini kadiri siku zinavyokwenda wimbi hili la vijana linazidi ongezeka na kwa mtazamo wangu ni kama serikali yetu inatengeneza bomu la nyuklia kwa baadae ambalo likija lipuka litakuwa ni tatizo kubwa sana kwa amani ya nchi yetu. Tumeweza ona wiki chache zilizopita huko zanzibar jinsi vijana ambao ndio nguvu kazi ya taifa wakiongozwa katika kuhatarisha amani ya nchi. Ni siku moja tangu bajeti ya nchi kusomwa lakini katika kusikiliza bajeti hiyo sijaona ni namna gani serikali imepanga kuwasaidia vijana hawa ambao kwa sasa wamekuwa wengi. Ni mahala gani bajeti hii itawasaidi vijana hawa na kuwaondoa katika wimbi la kuishi barabarani. Kwa ujumla vijana hawa tusipowaangalia na kuweza kuwawekea mikakati ya namna ya wao kuweza kuishai japo kwa kiasi kidogo maisha yaliyo bora tutaishia kufukuzana nao barabarani kwa kutuchomolea side mirrow za magari na kuiba hand bag za wakina mama.
Ushauri wangu kwa serikali inabidi kuwafikiria kwani na wao ni part ya watanzania.
Ushauri wangu kwa serikali inabidi kuwafikiria kwani na wao ni part ya watanzania.