Eng. Y. Bihagaze
JF-Expert Member
- Sep 8, 2011
- 1,488
- 908
Sidhani
Nimesoma mabandiko humu ndani, na Kwenye vyombo mbalimbalivya habari juu ya Matamshi ya wazi wazi waliyoyatoa na wanayoendelea kuyatoa baadhi yawanachama wa CCM juu ya mageuzi ya kisiasa yanayoendelea ndani ya Chama hicho na pilika za kujikwamua kwa kile kinachodhaniwa ni kupotea kwa mvuto wa Chama mbele ya jamii.
Wanachama hao ambao pia ni kada ya Uongozi wa CCM, wakiwemo watoto wa waliokuwa wanasiasa mashuhuri , William Malecela, Moses Nauye ,January Makamba na wengineo, kwa namna moja au nyingine wamekuwa mstari wa mbele kwa kile kinachotafsirika kwamba ni juhudi za kukinusuru Chama.
William kwa nyakati tofauti amemnanga katibu mkuu wa CCM- W.Mukama kwamba ni mtu aliyepitwa na kasi ya mabadiliko ya Kisiasa Inayoendelea. Nakwa Mara kadhaa amemsifia Katibu mwenezi wa CCM Taifa Nape Nauye, kwamba ni mtu awezaye kutambua tatizo na kulichukulia maamuzi pasipo kumshirikisha au kusubiri ushauri kutoka kwa Mwenyekiti wake.
Kwa nafasi hiyo, nadhani kwenye jamii yetu, mbali na wingi wa mitazamo ya kisiasa hata kiuchumi miongoni mwetu Vijana wa taifa hili, nadhani Bado tuna weledi kamili kushauriana. Vijana Hawa Lazima wajue kwamba si utaratibu wa jamii yetu ya Kitanzania Kutowaheshimu wazee wetu, na pia si-utanzania Kumchamba au kumvua nguo mtu mzima mbele ya mboni za jamii. Ketendo cha vijana hawa kuwashambulia wazee wa Chama kinatafisiriwa kama kuwavua Nguo wazee hawa ambao Hata kama Taifa au Chama hakiwaheshimu lakini Familia na watoto wao bado wanawaheshimu.
Vijana hawa HAWAWEZI kulazimisha Chama kiende kama wao WATAKAVYO Chama kina miiko, kanuni, na taratibu. Na kabla ya kujiunga na Chama chochote Lazima Ujue Miiko yao na kipi unapaswa Utende na Kipi Usitende na si Kukurupuka na kuanza kutumia vyombo vya Habari kukandamizia udhaifu wa wazee wa chama.
Vijana hawa wa Chama lazima wajue Wanaposhutumiana, wasisahau kila mmoja hapo amewekwa na Mamlaka Hiyo moja, na Mamlaka Hiyon ndiyo yenye maamuzi ya kujua nani mzembe imuondoe na nani abaki. Na kama wote wamewekwa na mamlaka Moja, ni mamlaka Hiyo hiyo moja inayotakiwa kuwaadabisha,na kama mamlaka husika inashuhudiaUgomvi huo na yenyewe imekaa kimya basi tatizo kubwa liko kwenye mamlaka Hiyo kwa udhaifu mkubwa wa kutowawajibisha watendaji wake. Hata ndani ya Familia baba asipoisimamia familia yake vyema Lazima watoto watapotea kimaadili.
Vyama vya kisiasa ni kama Dini, Kama imani yako haiendani na Dini au dhehebu uliloko, huna sababu ya kuikashifu dini/dhehebu hilo uliloko,kimyakimya unajiondoa na kutafuta pale unapodhani panafaa imani yako na sikuleta matapishi kwenye ustaarabu wa wengine..
Kama Vijana Hawa wanadhani CCM ni Chama legelege, chama ‘slow' na hakimudu kasi ya vuguvugu la kisiasa nchini kwa sasa, hakuna aliyewabatiza wawe waumini wa CCM wa milele. Nawashauri kuliko kuendelea kuwakosea adabu wazee hawa ni vema wakaangalia kule wanakodhani wao kuna kasi wanayoitaka ya kisiasa na wajiunge huko.
Mimi si mwanachama wa CCM lakini pia si mwanachama wa Kutukana wazee.. nacholenga hapa ni kuwahakikishia wazee wetu wote kwamba si-vijana wote wa taifa hili wanaafiki mkumbo wa majibizano haya ndani ya Chama,na jamii kwa ujumla
Nimesoma mabandiko humu ndani, na Kwenye vyombo mbalimbalivya habari juu ya Matamshi ya wazi wazi waliyoyatoa na wanayoendelea kuyatoa baadhi yawanachama wa CCM juu ya mageuzi ya kisiasa yanayoendelea ndani ya Chama hicho na pilika za kujikwamua kwa kile kinachodhaniwa ni kupotea kwa mvuto wa Chama mbele ya jamii.
Wanachama hao ambao pia ni kada ya Uongozi wa CCM, wakiwemo watoto wa waliokuwa wanasiasa mashuhuri , William Malecela, Moses Nauye ,January Makamba na wengineo, kwa namna moja au nyingine wamekuwa mstari wa mbele kwa kile kinachotafsirika kwamba ni juhudi za kukinusuru Chama.
William kwa nyakati tofauti amemnanga katibu mkuu wa CCM- W.Mukama kwamba ni mtu aliyepitwa na kasi ya mabadiliko ya Kisiasa Inayoendelea. Nakwa Mara kadhaa amemsifia Katibu mwenezi wa CCM Taifa Nape Nauye, kwamba ni mtu awezaye kutambua tatizo na kulichukulia maamuzi pasipo kumshirikisha au kusubiri ushauri kutoka kwa Mwenyekiti wake.
Kwa nafasi hiyo, nadhani kwenye jamii yetu, mbali na wingi wa mitazamo ya kisiasa hata kiuchumi miongoni mwetu Vijana wa taifa hili, nadhani Bado tuna weledi kamili kushauriana. Vijana Hawa Lazima wajue kwamba si utaratibu wa jamii yetu ya Kitanzania Kutowaheshimu wazee wetu, na pia si-utanzania Kumchamba au kumvua nguo mtu mzima mbele ya mboni za jamii. Ketendo cha vijana hawa kuwashambulia wazee wa Chama kinatafisiriwa kama kuwavua Nguo wazee hawa ambao Hata kama Taifa au Chama hakiwaheshimu lakini Familia na watoto wao bado wanawaheshimu.
Vijana hawa HAWAWEZI kulazimisha Chama kiende kama wao WATAKAVYO Chama kina miiko, kanuni, na taratibu. Na kabla ya kujiunga na Chama chochote Lazima Ujue Miiko yao na kipi unapaswa Utende na Kipi Usitende na si Kukurupuka na kuanza kutumia vyombo vya Habari kukandamizia udhaifu wa wazee wa chama.
Vijana hawa wa Chama lazima wajue Wanaposhutumiana, wasisahau kila mmoja hapo amewekwa na Mamlaka Hiyo moja, na Mamlaka Hiyon ndiyo yenye maamuzi ya kujua nani mzembe imuondoe na nani abaki. Na kama wote wamewekwa na mamlaka Moja, ni mamlaka Hiyo hiyo moja inayotakiwa kuwaadabisha,na kama mamlaka husika inashuhudiaUgomvi huo na yenyewe imekaa kimya basi tatizo kubwa liko kwenye mamlaka Hiyo kwa udhaifu mkubwa wa kutowawajibisha watendaji wake. Hata ndani ya Familia baba asipoisimamia familia yake vyema Lazima watoto watapotea kimaadili.
Vyama vya kisiasa ni kama Dini, Kama imani yako haiendani na Dini au dhehebu uliloko, huna sababu ya kuikashifu dini/dhehebu hilo uliloko,kimyakimya unajiondoa na kutafuta pale unapodhani panafaa imani yako na sikuleta matapishi kwenye ustaarabu wa wengine..
Kama Vijana Hawa wanadhani CCM ni Chama legelege, chama ‘slow' na hakimudu kasi ya vuguvugu la kisiasa nchini kwa sasa, hakuna aliyewabatiza wawe waumini wa CCM wa milele. Nawashauri kuliko kuendelea kuwakosea adabu wazee hawa ni vema wakaangalia kule wanakodhani wao kuna kasi wanayoitaka ya kisiasa na wajiunge huko.
Mimi si mwanachama wa CCM lakini pia si mwanachama wa Kutukana wazee.. nacholenga hapa ni kuwahakikishia wazee wetu wote kwamba si-vijana wote wa taifa hili wanaafiki mkumbo wa majibizano haya ndani ya Chama,na jamii kwa ujumla