Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Niko mitaa Tabata Ubaya Ubaya na washkaji wa A Town....
Kinachoendelea katika eneo hili ni nyama choma na bia, lakini hawa masharobaro wa A Town nawaona wakipena kitu kilichofungwa kwenye nailoni kwa umahiri. Awali nilidhani ni ile kitu maarufu kwa jina la CHA ARUSHA, lakini nimeshangaa wanabwia na kisha kutema mate...
Nimeshikwa na udadisi na nilipouliza wakaniambia hiyo kitu inaitwa NGISUGI au UGORO.
Yaani wanaubwia kama hawana akili nzuri, na wameniambia hiyo kitu nimaarufu sana huko A TOWN....
Mimi nilijua hii kitu inatumiwa na wazee tu na vibibi vizee, kumbe hata vijana...!