Vijana vipi katika ajira

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Miezi Michache iliyopita nilianzisha Blogu ya kutangaza na fasi za kazi East African Career and Job-Hunting Blog imekuwa hewani kwa muda mfupi kidogo na imepata mafanikio makubwa haswa katika matangazo na secta zingine zinazohusu mtandao huo nashukuru wote kwa wale ambao kwa namna moja au nyingine walinipa moyo wakati ule nakumbuka wa kwanza ni Jackson mbogela ( mwaka huu sijamsikia sijui yuko wapi )

Wakati nimeanzisha na kuendeleza vitu kadhaa nilifikiri watanzania wanahitaji sana ajira , wanahitaji sana nafasi hizi pamoja na mengine mengi yaliyokatika blogu hiyo , muda ulivyozidi kwenda nikagundua mawazo yangu sio sawa kabisa kuna vitu zaidi watanzania hawajui , au labda hawajafundishwa au sijui kuna tatizo gani

Blogu hiyo niliiunganisha katika mtandao wa blogu za kiafrika katika afrigator pia nikaunganisha katika mtandao wa blogu za Kenya katika kenyaunlimited , kila siku Napata email karibu 200 na zaidi kutoka kwa wakazi wa afrika mashariki asilimia 90 kati yao ni wakenya wengine ni Rwanda huko , na wengine walio katika nchi za mbali ila wanapenda kuja kufanya kazi nchini Tanzania

Inasikitisha sana pamoja na kwamba magazeti na idara za serikali zinatoa nafasi nyingi za kazi na kuzitangaza muamko wa Tanzania haswa vijana umekuwa mdogo sana katika kuchangamkia nafasi hizi wengi wanaochangamkia ni wa nchi za jirani haswa Kenya wako shap sana na waelewa sana mtu yuko radhi kuagiza gazeti kutoka dar kwenda Nairobi kupata nafasi hizo za kazi .

Watanzania haswa vijana wanatakiwa waelewe nafasi waliyonayo sasa na huko mbeleni haswa tunapoingia katika mambo ya afrika ya mashariki soko letu la ajira linajaa watu wengine badala ya sisi , wajukuu zetu sijui watakimbilia wapi

Naamini katika ajira hakuna kupendeleana kama wengi wanavyodhani na kuaminishwa hivyo na baadhi ya makundi ya jamii .

Mchana mwema
 
Link ya nini ? Hiyo blogu ? Tembelea East African Career and Job-Hunting Blog

alfajiri njema
 
Kaka SHY Mimi nipo, Majukumu tu yamebana.
Ningeshauri mambo 2 yapewe mkazo 2009.
1. Kuwafahamisha waTz juu ya uwepo wa habari katika net (Itangaze Blog yako mara kwa mara Kama kwa akina Michuzi hata kwenye magazeti, maana kujua kuwa kuna blog inayohusu ajira ni jmabo moja, wengi hawana habari za blog zetu,)
2. Kuwapa ujasiri wa ku- Access kama kutembelea i-net cafe (Kusoma habari katika net ni jambo la pili gumu wengi huwa hawaamini kama habari za i-net zina ukweli, wamekuwa spolied na wanasiasa ukikumbuka siku zote wanasisa wa Bongo utawasikia hizi ni habri za kwenye i-net, kwa sababu ya u-old fashioned wao)

Tupo pamoja. Tutafanikiwa tu.
 
Vijana wengi wa sasa hivi hawana spirit ya ushindani.
wamezoea chuma ulete.

Wenzetu wa nchi jirani ni wazuri katika ushindani tangu wakiwa wadogo wanashiriki kwenye michezo mingi ya ushindani na kushindana kwenye mambo ya elimu.

Huku bongo vijana wanaamka asubuhi wanakaa kijiweni wanasubiri mtu apite waeleze shida zao.

Angalia wapiga Debe kutwa kashinda kwenye kituo anasubiri kuomba, watoto wa kishua ndo usiseme, ni TV na movie siku nzima. i-net ataenda sa ngap wakat jion ni starehe.

Wapiganaji wa kweli ni wachache sana. Mi nalaumu Malezi na Shule tulizosoma.
 
Back
Top Bottom