Vijana hii imekaaje?

Mwanajamii

JF-Expert Member
Mar 5, 2008
7,063
68
Nchi yetu ina vijana wengi sana Wasomi , wengine wanaendelea kusoma, vijana wenye nguvu za kufanyakazi za ujenzi wa Taifa la Tanzania. Jambo la kushangaza ni kwamba elimu yote tuliyo nayo kama vijana, nguvu zote tulizonazo pamoja na fursa nyingine nyingi kama vijana , vyote hivyo vimeingiliwa na watu ambao aidha wanaonekana wana uelewa zaidi kuliko sisi vijana ama wanafanya makusudi ili mradi tu malengo yao yaweze kutimia. Vijana tumekuwa msatari wa mbele kuhamasishwa kutumia nguvu zetu, elimu tuliyo nao kufanya mambo ambayo kwa namna moja au nyingine ni wachache watakaonufaika nayo. Tumekuwa mstari wa mbele kujihusisha katika migomo ambayo siyo ya lazima, maandamano yasiyo ya lazima na hata kufikia hatua ya kutoa lugha chafu kwa Wazazi wetu, wakubwa zetu, viongozi wetu wa dini na hata wa Serikali. Je Mwisho wa siku tutamlaumu nani? ni mara ngapi tumetumia elimu na nguvu tulizonazo kushiriki kwenye makongamano, shughuli za uzalishaji mali, ushauri , ili nafasi yetu kama vijana iweze kuonekana katika jamii? Tutafakari hili vijana wenzangu ili nafasi yetu katika jamii iwe chachu ya maendeleo, amani na utulivu katika Taifa letu la Tanzania. Tutambue kuwa itikadi za kidini, kisiasa hupata msukumo wa nje kwenda kwa watu maarufu lakini kupitia kwa vijana kama ngazi ili mradi tu hawa watu wa nje pamoja na wafuasi wao watimize haja zao huku wakiacha kundi hili likiangamia.
 
Hujaeleweka unachotaka ni nini? ni kama mtu kakutuma useme jambo flani bahati mbaya ukaingia chaka,unaanza kukatisha tamaa kama we ni mmojawapo ya vijana halafu unaanza kwa kutumiwa
 
vijana gan hao unaowamaanisha?!... maana wengine fursa ya kupata elimu 2meikoxa na mixemo yenu ya
>NO LOAN
>PREVIOUS LOANEES
>BUDGET DEFICITY e.t.c. xaxa unataka 2fanye nn na wazaz hatuna,
hebu nenda zako huko kalale!...
"oooh vijana, vijana...."
UNATULISHA WW?!....
 
umekosa uwezo wa kufikiri , alianza vizuri, amemaliza vibaya. ana mawazo mgando kwa vile inaonyesha ni mtoto wa fisadi mmoja, hajui shida, wala hajui kwa nini vijana wanakuwa hivyo kwa hivyo tumsamehe.
 
we unajifanya kijana? uskute we ni kingunge au mukama unatuzuga tu hapa, utajua nguvu ya vijana 2015 p.u.m.b.a.f. wewe
 
Unaungana na ile kauli ya hujui kwann watanzania masikini?na ww hujui kwann vijana wanaandamana?wakae kimya fursa na rasilimal zilizopo zinatumia na wachache?wasiandamane kwa kunyimwa na kucheleweshewa mikopo pesa walipwe dowans,wakiwa kama wajasilia mali wakae kimya wasizalishe na kuendeleza biashara zao huku umeme wa mgao?mbona una mawazo kama ya kingunge na chiligati,tutakaa kimya cku moja kama mambo yataenda sawa usindanganywe na hiyo ajira yako unayomiliki leo kuna vijana wengi sana wamemaliza vyuo vikuu hawana ajira na wao wakae kimya?
 
Topic ni nzuri inahitaji kuondoa ushabiki ili kurespond hata hivyo uhuru wa kujieleza ni muhimu kuuzingatia. na kazi tufanye
 
Back
Top Bottom