Vijana DAR kuundamana kuunga mkono hotuba ya Kikwete

Maskini ya Mungu inawezekana kabisa hao vijana hata hawakuisikiliza hiyo hotuba ila njaa ndu zinawafanya wafuate mkumbo.
 
Nafikiri ni haki yao kuandamana, waombe kibali Polisi, pia nafikiri maandamano hayataisha salama, kwani wataandamana na baadae watagundua si wamoja, kutakuwa na mafisadi na walala hoi, kwani mafisadi watakuja na magari ya kifahari na walala hoi watahoji wameyapataje magari yale; nao watagundua si wamoja na vurugu kali sana itaanzia pale. nafurahia maandamano haya! Polisi kaa chonjo balaa laja la ukombozi wa kweli.
 
MAANDAMANO ya kuunga mkono hotuba ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa mwishoni mwa mwezi uliopita, yanatarajiwa kufanyika Dar es Salaam Machi 16, mwaka huu, yakiwa na ujumbe ‘amani yetu bado tunaipenda'. Akizungumza na waandishi wa Habari mjini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Vijana wa Tanzania, wapenda amani, Said Mwaipopo alisema, pia maandamano hayo yatahusisha kupinga kauli viongozi wa CHADEMA zinazochochea kutokea kwa vurugu nchini.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti huyo, inaeleza kuwa, vitendo na kauli za viongozi vya chama hicho vina lengo la kupandikiza chuki kwa Watanzania dhidi ya serikali iliyopo madarakani, ambavyo mavuno yake ni umwagikaji wa damu.
Alisema, maandamano yanayofanywa na CHADEMA huvishwa sura ya kupanda kwa gharama za maisha, wakati huohuo yakiwa na lengo la kuipinga na kutaka kuing'oa serikali.
Maandamano hayo yatafanyika kuanzia viwanja vya Mnazi Mmoja mpaka uwanja wa Bakhresa Manzese, na Mwenyekiti wa TLP Augustino Mrema anatarajiwa kuyaongoza.
source: www.uhurupublications.com
wakimaliza tu, CDM nao waandae ya kwao halafu uone vijana wa Dar wako upande upi

we unataka amani hujala, kibanda kimebomolewa, ajira hakuna, wenye mabenzi wanakumwagia vumbi na tope na mkeo anashikishwa ukuta na bosi?

AMANI YA MTANZANIA HAIKULETWA NA CCM NA KAMWE HAITAVUNJWA NA CHADEMA... ILILETWA NA WATANZANIA NA ITAVUNJWA NA WATANZANIA TU!!!!
 
Hiyo kamati ya vijana wapenda amani Tanzania imeundwa lini..? na wajumbe wake ni akina nani? na shughuli zake zingine ukiacha hili la kuratibu haya maandamano ni zipi?

Kama kweli ipo kamati kama hii nadhani ni vizuri ingeshirikisha vijana wengi na iwe wazi yaani isiwe ya mfukoni. na ishughulikie matatizo ya msingi yanayowakabili vijana hapa nchini na kutoa maangalizo kwa Jamii na serikali kwa kwa ujumla juu ya viashiria vya uvunjifu wa amani hapa nchini....mfano ukosefu wa ajira kwa vijana nchini...kutofautiana sana kwa kiwango na ubora wa elimu unaopatikana ktk shule za kata (ambazo watoto/vijana wengi wa kitanzania wanaotoka ktk familia za kawaida wanasoma) na zile shule za kimataifa/Academias/seminaries (ambazo watoto/vijana wengi wa kitanzania wanaotoka ktk familia zenye afadhali wanasoma)... utengwaji wa maeneo ya wazi na uboreshaji wa miundo mbinu katika maeneo ambayo vijana wa kitanzania wameamua kujiajiri....Kitu ambacho ktk hili namuunga sana mkono..Mh Dibogo Wenje kwa kuwatetea na kuwapigania vijana wenzake wa Nyamagana walioamua kujiajiri...Vijana kama vijana wana matatizo mengi sana yanayowakabili ktk nchi yetu hivyo kukurupuka na hoja zisizo na manufaa wala baraka za vijana wenyewe wa taifa hili ni kutowatendea haki..Mwisho pia ningependa nimshauri Bw Said Mwaipopo kama kweli ana nia ya dhati ya kutetea vijana ktk nchi hii aanze harakati zake ktk taasisi zenye vijana wengi nchini ili aweze kupata mawazo ni jinsi gani kamati hiyo ifanye kazi zake na sio kukurupuka na mambo ya kipuuzi ya kudhalilisha vijana wa taifa hili.
 
Hivi Mh. Mrema (Mb. TLP) ni kijana au ndo mlezi wa hao vijana? Anyway, Maandamano ruksa, maana huwalazimishi watu kupokea ujumbe na kuutafsiri kama ulivyolenga. Watu wanaona wenyewe kama ujumbe unawagusa au ni uzushi. Wajiandae, Tz ya sasa c ya mwaka 1961, watu walikuwa wanaimba uhuru tu, sahivi tunataka kuona vitu vikifanyika sio tutafanya hili na lile.
 
Hivi Mh. Mrema (Mb. TLP) ni kijana au ndo mlezi wa hao vijana? Anyway, Maandamano ruksa, maana huwalazimishi watu kupokea ujumbe na kuutafsiri kama ulivyolenga. Watu wanaona wenyewe kama ujumbe unawagusa au ni uzushi. Wajiandae, Tz ya sasa c ya mwaka 1961, watu walikuwa wanaimba uhuru tu, sahivi tunataka kuona vitu vikifanyika sio tutafanya hili na lile.
Tatizo langu si kuandamana waacheni waandamane, wasiwasi wangu ni kwa Mh. Mrema kweli ataweza kutembea toka Mnazi Mmoja hadi uwanja wa Bakhresa Manzese, akiweza nitaamini dawa ya mzee wa Lindo inaponya.
 
Maandamano yataongozwa na Mwenyekiti wa TLP hahaha! let the deads bury their own deads!
 
KIpindi cha nyuma baadhiyetu tuliposema Mrema ni SISIEM tulikejeliwa sana.....HAYA SASA ONENI!!!!!
Mzee mageuzi1992 hata karatasi nyeupe ilitengenezwa kwa magome ya mti ukiicha maktaba kwa miaka mingi itarudia rangi yake.
 
Huwa najiuliza hawa watu wanatoka wapi sipati jibu! JK aliongea na "wazee wa DSM" wakamshangilia wakati getini kuna wazee wa DSM (waliokuwa EAC) wanalilia haki zao. Hao sijui aliwatoa wapi. How do they represent wenzao. Nami kawatuma? Sasa wameibuka vijana, wa dar hiyohiyo! Wametoka wapi? Taasisi gani? Nani kawatuma? Kwa kikao gani? Wanawakilishaje vijana wa Dar? Wanawasilisha kile vijana wa Dar wanataka? Au wameokotwa okotwa tu kama wale wazee kwenda kuuza sura na kugaiwa t shirt na kofia kisha wanarudi home masikini vlevle!? Mungu awasaidie tu, macho yao "yaone" na masikio "yasikie!"
 
maandamano ya kuunga mkono hotuba ya rais jakaya kikwete aliyoitoa mwishoni mwa mwezi uliopita, yanatarajiwa kufanyika dar es salaam machi 16, mwaka huu, yakiwa na ujumbe ‘amani yetu bado tunaipenda’. Akizungumza na waandishi wa habari mjini dar es salaam, mwenyekiti wa kamati ya vijana wa tanzania, wapenda amani, said mwaipopo alisema, pia maandamano hayo yatahusisha kupinga kauli viongozi wa chadema zinazochochea kutokea kwa vurugu nchini.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mwenyekiti huyo, inaeleza kuwa, vitendo na kauli za viongozi vya chama hicho vina lengo la kupandikiza chuki kwa watanzania dhidi ya serikali iliyopo madarakani, ambavyo mavuno yake ni umwagikaji wa damu.
Alisema, maandamano yanayofanywa na chadema huvishwa sura ya kupanda kwa gharama za maisha, wakati huohuo yakiwa na lengo la kuipinga na kutaka kuing’oa serikali.
maandamano hayo yatafanyika kuanzia viwanja vya mnazi mmoja mpaka uwanja wa bakhresa manzese, na mwenyekiti wa tlp augustino mrema anatarajiwa kuyaongoza.
Source: www.uhurupublications.com

ni haki yao waitumie tu
 
hoja zako zimejaa mashiko
Ukombozi wa Tanzania na watu wake ni ngumu kwa sababu ya baadhi ya aina yako........! Pengine jina lako lilikosewa kuandikwa vema; "Kash_ga"; Penye ____ panahitaji herufi "o".....!
 
Hawa waacheni tu. Watakosa watu na baadaye watasema polisi wamekataa na wao wanatii.
 
Ukombozi wa Tanzania na watu wake ni ngumu kwa sababu ya baadhi ya aina yako........! Pengine jina lako lilikosewa kuandikwa vema; "Kash_ga"; Penye ____ panahitaji herufi "o".....!

achana naye huyo.

amekuja jf kupost contents za habari leo na uhuru.

atafulia soon
 
Naona kama wamekulia Mombasa vile, hawaeleweki eleweki.

haaahaaa ikiuma sana semeni nitoe maana naona nawagusa kuliko mpaka mnashindwa kaa vizuri,kimsingi nimekuja kuwashika aluta continua! Mungu Ibariki Tanzania,mungu ibariki CCM,mungu ibariki Chadema wafike salama 2015 tushuhudie tena mtu mtanange
 
maandamano ya vibaraka wa mafisadi na ccm yao, kwanza waache kusingizia baraza la vijana Tanzania, wawe wazi kwamba ni baraza la vijana mafisadi watarajiwa wa ccm
 
Back
Top Bottom