Vigogo wagawana viwanja vya Gezaulole

Kuna list ilitolewa na mdau, lkn nikiangalia majina yaliyotajwa leo 'source Mwananchi' mengine hayapo. Je kuna list mpya??

Kama vipi warudhishe zile 30k. Au ndio posho za madiwani wetu kule??

Kweli Tanzania zaidi ya uijuavyo!!!
 
waacheni wanajiandalia mji wao........

Thats why i hate ccm na system yao......

Bado kuna kigogo kachukua viwanja 30 na jina lake wameliminya.......
 
Nkamia toa maoni yako kuhusu hili au kwa sasa lipo mahakamani?

Watanzania ambaye ni mwananchi wa kawaida asiyekuwa na influence yoyote ktk chochote iwe serikalini, chama especially tawala, taasisi za serikali, mtoto/ndugu/jamaa/rafiki wa kigogo naomba niwaambie ya kwamba usije hata siku moja ukajiingiza kununua viwanja kama hivi wanavyosema vimepimwa na manispaa/halmashauri kwa sababu Uwezekano wa kupata ni 0.00000001%=0 utakuwa unapoteza hela ya kuchukua form na muda na ukicheza unatapeliwa fedha kwa kuuziwa kiwanja feki.

Haya yote nimeyaona mwenyewe na yamenitokea mwenyewe pale Arusha. Wale wanaofahamu viwanja vya burka na vile vya karibu na uwanja mdogo wa ndege Arusha airport majina kama haya ya vigogo, watoto wao, marafiki ndugu jamaa yalikuwepo mengi sana.

Usijisumbue wewe na mimi tusiokuwa n uwezo ktk jambo hili tutakuwa tunapoteza badala ya ku-gain.
 
Ndiyo maana sasa hivi kila mtu mwizi, uza kila kitu hata binadamu kama ana soko unauza tu
 
Viwanja 1800 vimeuzwa kwa wananchi. Kati yao, kuna viongozi wa kada mbali mbali, na kuna ndugu zao ama watoto wao. Majina yaliyoorodheshwa ya "wanene" hao ni kama 50.

1800-50= 1750. Tufikirie tu kwamba "walala hoi" 1,750 au hata 1500 wamepata viwanja, na vigogo 300 wamepata pia. Tunalalamika vigogo wamegawana viwanja!

Katika vigogo hao, wana watoto wakubwa tu...namfahamu Juanita Mramba, anafanya kazi benki moja jijini. Naye amenunua kiwanja. Tunalalamika mtoto wa kigogo kauziwa kiwanja? Hivi, wao hawapaswi kuwa na kiwanja simply because baba yake (tu assume tu) ni kigogo na ana viwanja vingine? Kweli hili ni taifa la walalamishi tu...hata tufanyeje.

Ninadhani pengine kama wamekiuka sheria, kwamba vigogo hawakustahili kuuziwa hata mmoja, na kwamba iwe ni kinyume cha sheria kumiliki kiwanja zaidi ya kimoja Tanzania, basi hawa wangekuwa wana makosa. Wengi wetu tumekuwa tunawekeza mno kwenye kulalamika kuliko kutoa maoni ya namna bora ya kuendesha mambo.
 
Watanzania kwa wivu tumezidi!!!! Ukiangalia hayo majina ya vigogo walio tajwa hayazidi 40 kati ya viwanja 1,800 hivi hatujui kuwa na wao wana haki sawa? Ulitegemea wakapate wapi viwanja?

Kitaalamu unapogawa viwanja hutakiwi kuweka eneo moja watu wa daraja moja lazima uchanganye ili maendeleo yawahi, kwa mfano walala hoi wengi hatuwezi kuvuta umeme zaidi ya nguzo 5, hivyo basi kwenye mtaa wako pakiwa na chagonja mmoja uhakika anaweza kuwasogezea walala hoi na mkafaidika!!!

Asipo saidia ndio maana huwa inachukuwa muda mrefu huduma za kijamii kuwafikia wananchi coz wanashindwa kulipia gharama za huduma mbalimbali kama maji, umeme na barabara!!! Huo ni mtazamo wangu na sina tatizo kabisa na hao watu walio pewa!!!

Swali tujiulize je, taratibu zilifuatwa?
 
Vigogo wagawiwa viwanja Dar



Orodha hiyo pia inaonyesha majina ya ukoo yanayofanana na majina ya baadhi ya viongozi ambao ni Miraji Kikwete, Khalfan Kikwete, Juanita Mramba, Suzan Mkapa, Zainab Mkomwa, George Rupia, Maimuna Mfutakamba, Mary Membe, Pharles Ngeleja, Judith Kahama na Wilfred Mwanri.

Nimelia sana nilipo ona jina la Khalfani Kikwete kwasababu Viwanja vilivyotolewa mara ya Kwanza niliomba naye huyu mtoto lakini yeye alibahatika akapata kiwanja kikubwa, lakini mimi nilikosa japo kuwa mimi ni mtu mzima kuliko yeye na nina uwezo wa kulipia pia sikuumia sana kwasababu ana haki pia. Safari hii nimeomba tena amebahatika yeye tena, hivi jamani huu ni ubinaadam kweli kitoto kidogo kurundikiwa viwanja ili vimfae akikuwa halafu mimi mtu mzima nikose pa kujenga sitaki Kumzungumzia Miraji kwasababu na yeye hiki ni cha kwanza nitaumia iwapo awamu ya pili watampa Miraji tena kiwanja cha pili ilihali mimi nataka kimoja tu sipati. Nina hasira sana sina cha kuifanya hii Serikali
 
Pole sana

Nimelia sana nilipo ona jina la Khalfani Kikwete kwasababu Viwanja vilivyotolewa mara ya Kwanza niliomba naye huyu mtoto lakini yeye alibahatika akapata kiwanja kikubwa, lakini mimi nilikosa japo kuwa mimi ni mtu mzima kuliko yeye na nina uwezo wa kulipia pia sikuumia sana kwasababu ana haki pia. Safari hii nimeomba tena amebahatika yeye tena, hivi jamani huu ni ubinaadam kweli kitoto kidogo kurundikiwa viwanja ili vimfae akikuwa halafu mimi mtu mzima nikose pa kujenga sitaki Kumzungumzia Miraji kwasababu na yeye hiki ni cha kwanza nitaumia iwapo awamu ya pili watampa Miraji tena kiwanja cha pili ilihali mimi nataka kimoja tu sipati. Nina hasira sana sina cha kuifanya hii Serikali
 
Kama wamefuata masharti na ni watanzania, sioni tatizo.

You can be right lakini kunapokuwa na majina hayo automatic Mkurugenzi wa Wilaya hawezi kuyatoa patupu. Tatizo tulilonalo kama TMK wangemnyima kiwanja Miraji Kikwete basi angeweza kabisa kumwambia baba yake amtimulie mbali. Ni vigumu sana mlala hao kushindana na majina ya akina Membe na Kikwete kwenye kupata viwanja. Mlalahoi hana chake kwa sasa.
 
Siku hizi ukiwa kiongozi hata ukinunua ardhi kihalali kabisa kama hawa waliotajwa basi inakuwa na 'walakini'!
 
Mimi nilienda kuchukua form nikafika pale nashangaa shangaa nikaambiwa watu wamekesha toka saa kumi alfajiri wapo pale kuchukua namba tu hapo hujapata form. Yule dada wa dirishani akanihurumia akaniambia hapo kama huna ki memo cha diwani au hujuani na mkurugenzi basi bora hela yako ukafanyie mambo mengine ya maendeleo.

Nikamwambia dada ahsante sana nikapangusa buttocks nikaondoka zangu.
 
sishangai kabisa kuona hayo majina. Bei ya hivyo viwanja ilikuwa ni tshs 12,000,000/=, mwananchi gani wa kawaida angemudu hiyo bei?


ndug freema agyeman: Huu ni uongo ulio wazi mkuu. Mita moja ya mrabaa kwa viwanja vya makazi ilikuwa ikiuzwa kwa shilingi 6000 na kiwanja kidogo kabisa walau kilikuwa na size ya mita 400 za mraba ambazo ni sawa na shilingi 2,400,000/= . Sasa wewe ni nani amekudanganya mabo haya. Kama huna uhakika au hujui ni vyeam ukawasikiliza wenye kuelewa masuala hayo la sivyo waweza ingia katika matatizo ya uchochezi. Cha msingi cha kusema ni kwamba pamoja na hayo bado bei ni kubwa
 
ndug freema agyeman: Huu ni uongo ulio wazi mkuu. Mita moja ya mrabaa kwa viwanja vya makazi ilikuwa ikiuzwa kwa shilingi 6000 na kiwanja kidogo kabisa walau kilikuwa na size ya mita 400 za mraba ambazo ni sawa na shilingi 2,400,000/= . Sasa wewe ni nani amekudanganya mabo haya. Kama huna uhakika au hujui ni vyeam ukawasikiliza wenye kuelewa masuala hayo la sivyo waweza ingia katika matatizo ya uchochezi. Cha msingi cha kusema ni kwamba pamoja na hayo bado bei ni kubwa

The Listener,

Mita moja ya mraba iliuzwa kwa kama sh 8000 sasa kama unataka sqm 400 manake hapo ni 3,200,000, sasa hapa kweli mlalahoi amezingatiwa?
 
Acheni kupiga kelele kuhusu viwanja vya gezaulole.

Utaratibu uliofutwa ni kutoa kipaumbele kwa yule aliyeonyesha uwezo mkubwa wa kununua kiwanja; katika fomu za maombi kulikuwa na kipengele cha kuonyesha WEWE UKO TAYARI KUNUNUA KIWANJA KWA KIASI GANI??
Hivyo mwenye kuweka KIWANGO KIKUBWA KAPEWA KIPAUMBELE, katika hali ya kawaida KATIBU MKUU HAZINA hawezi kuweka dau ndogo!!! Kwa hiyo usishangae Bw. Khija Kupata kipaumbele
 
Back
Top Bottom