Vigogo wa Uhamiaji Wapanguliwa

Shadow

JF-Expert Member
May 19, 2008
2,897
671
Leon BahatiMAKAMISHNA watatu wa Idara ya Uhamiaji nchini, wamesimamishwa kazi ikiwa ni siku 20 tangu Waziri wa Mambo ya Ndani , Shamsi Vuai Nahodha atangaze kufanya mabadiliko ya kiutendaji ndani ya idara hiyo.

Januari 17 mwaka huu, Nahodha alitangaza kufanya mabadiliko katika idara hiyo ili kuongeza tija na kukabiliana na mambo mbalimbali ikiwemo kudhibiti uingiaji nchini wa wahamiaji haramu.

Uchunguzi uliofanywa na Mwananchi, umebaini kwamba makamishna hao watatu (majina tunayo) jana walipewa barua za kuondoka kwenye nafasi zao na kutakiwa kuripoti wizarani ili kupangiwa kazi nyingine.

Hata hivyo, baadhi ya watumishi wa idara hiyo wamechukulia uamuzi huo wa kusimamishwa kazi makamishna hao kama wa kisiasa."Uamuzi huu umefanywa kisiasa.

Nafikiri hawa wakubwa wana watu wao ambao wanataka kuja kuwaweka kwenye nafasi hizo," alisema mmoja wa watumishi wa Idara ya Uhamiaji, kwa ombi la kutotajwa gazetini.


Source: Mwananchi
 
Wanao fanya kazi uhamiaji tupeni habari Pls.
Na sikia mmoja wapo ni Bashiri.m. Kapelekwa Mtwara.
Alikuwa anahusika na utoaji vibali vya kuishi.
Cha ajabu kama kweli Ni kuruka mkojo na kukanyaga kinyesi.
Maana mtwara ni mpakani na ataendelea na libeneke yake.
 
Wanao fanya kazi uhamiaji tupeni habari Pls.<BR>Na sikia mmoja wapo ni Bashiri.m. Kapelekwa Mtwara.<BR>Alikuwa anahusika na utoaji vibali vya kuishi.<BR>Cha ajabu kama kweli Ni kuruka mkojo na kukanyaga kinyesi.<BR>Maana mtwara ni mpakani na ataendelea na libeneke yake.
 
jamani waziri alisema wale wote waliokaa kituo kimoja cha kazi kwa zaidi ya miaka 8 watahamishawa, sasa tunaona kimya vp? mliopo jikoni tupaeni habari kama kuna barua za uhamisho zinakuja.
 
Kapigwa changa Mpemba nivisasi tu wengi walio hamishwa ni kwa husda tu si kwa tija kama anavyo tarajia:Mfereji vuta subira nadhani utakuwa Mtwara wewe Rukwa tayari
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom