MgungaMiba
JF-Expert Member
- Aug 28, 2011
- 999
- 815
Naomba wahakiki mnisaidie kupanga vizuri mada hii ili iwe na mtiriko mzuri, kwani natumia Cellphone na kuna Advert inanisumbua na kunikatisha, naomba niendelee na kigezo cha pili ambacho kitatumika kumuengua Mwl Kashindye, Kisha mwisho Kama hakutakuwa na interruption yoyote na kama charge itabakia, basi nitasuggest namna ya kupangua, lakini naamini kwa kuanika hadharani njama hizi, basi kutavunja nguvu sana utekelezaji wake.
Kipengele cha pili kitakachotumika kumuengua Mwl Kashindye ni hiki kifuatacho, kwenye form zake za kuwania ubunge alizokwenda kuzichukua kwa Mkurugenzi, kuna kipengele cha udhamini wa chama chake, mbali ya udhamini wa wapiga kura. Kipengele hiki kinatakiwa kujazwa na Katibu wa Wilaya wa chama chake ambacho ni CHADEMA, bila udhamini wa Katbu huyo form hizo zitakuwa hazija kamilika, mgombea ataenguliwa.
Sasa kwa Hali ilivyo CCM wilaya ya Igunga imegundua kuwa Katibu wa Wilaya wa CHADEMA, Bw Christopher, hakuchaguliwa kihalali kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA, kwa hiyo watapinga uhalali wa yeye kuwa na mandate ya kumdhamini mgombea kwa niaba ya CHADEMA, kwa hiyo mgombea wa CHADEMA itabidi aenguliwe kwa kuwa atakuwa amekosa udhamini wa Afisa wa chama ngazi ya wilaya kama sheria inavyotaka.
Vipengele hivi viwili visipofanyiwa kazi (Wanasheria wanajua hivyo) hata kimojawapo tu kikipita kinatosha kuleta maafa na kilio, kulalamika na mikwara mingi baada ya mzinga kulia, havitasaidia. Kwa kuwa nachukia dhulma na kupenda haki itendeke, ingawa sina mamlaka yoyote ndani ya CDM, basi naomba tu wanasheria wa CDM waikague vizuri barua ya likizo ya Mgombea, kisha waiangalie zheria inayohusiana na utaratibu wa utoaji wa barua hiyo, kama vile, je, aliesaini barua hiyo Ana mamlaka hayo?
Maelezo na mihuri yake inakidhi? Chronological factors zimekaa sawa? Hakuna errors zozote (typing or otherwise) ambazo zinaweza kupotosha maana hivyo kutoa mwanya wa barua hiyo kupingwa uhalali wake? Pili, wahakikishe kuwa ni kweli kuwa katibu wa Wilaya wa CDM Bw Christopher hakuchaguliwa katika nafasi yake kwa mujibu wa katiba ya CDM, kama ndivyo, je ni utaratibu gani ulitumika wa kumuinstall, je document zilizomuhalalisha zipo na zipo valid hadi sasa?Kila ilivyo, wanasheria wazipuuze hata chembe ya factor yoyote inayoweza kutumiwa kumkwamisha mgombea, otherwise muda hautatosha kujitetea mahakamani kama ilivyokuwa kwa Wenje kule Mwanza, uchaguzi ule ulikuwa wa miezi mitatu lakini huu utakuwa wa wiki tatu tu, mahakama ikimaliza kusikiliza rufaa kabla haijatoa uamuzi uchaguzi utakuwa umekwisha, ngoma itabidi ije ianze upya!
MIBA YA MGUNGA HAIUCHOMI MGUNGA!
Kipengele cha pili kitakachotumika kumuengua Mwl Kashindye ni hiki kifuatacho, kwenye form zake za kuwania ubunge alizokwenda kuzichukua kwa Mkurugenzi, kuna kipengele cha udhamini wa chama chake, mbali ya udhamini wa wapiga kura. Kipengele hiki kinatakiwa kujazwa na Katibu wa Wilaya wa chama chake ambacho ni CHADEMA, bila udhamini wa Katbu huyo form hizo zitakuwa hazija kamilika, mgombea ataenguliwa.
Sasa kwa Hali ilivyo CCM wilaya ya Igunga imegundua kuwa Katibu wa Wilaya wa CHADEMA, Bw Christopher, hakuchaguliwa kihalali kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA, kwa hiyo watapinga uhalali wa yeye kuwa na mandate ya kumdhamini mgombea kwa niaba ya CHADEMA, kwa hiyo mgombea wa CHADEMA itabidi aenguliwe kwa kuwa atakuwa amekosa udhamini wa Afisa wa chama ngazi ya wilaya kama sheria inavyotaka.
Vipengele hivi viwili visipofanyiwa kazi (Wanasheria wanajua hivyo) hata kimojawapo tu kikipita kinatosha kuleta maafa na kilio, kulalamika na mikwara mingi baada ya mzinga kulia, havitasaidia. Kwa kuwa nachukia dhulma na kupenda haki itendeke, ingawa sina mamlaka yoyote ndani ya CDM, basi naomba tu wanasheria wa CDM waikague vizuri barua ya likizo ya Mgombea, kisha waiangalie zheria inayohusiana na utaratibu wa utoaji wa barua hiyo, kama vile, je, aliesaini barua hiyo Ana mamlaka hayo?
Maelezo na mihuri yake inakidhi? Chronological factors zimekaa sawa? Hakuna errors zozote (typing or otherwise) ambazo zinaweza kupotosha maana hivyo kutoa mwanya wa barua hiyo kupingwa uhalali wake? Pili, wahakikishe kuwa ni kweli kuwa katibu wa Wilaya wa CDM Bw Christopher hakuchaguliwa katika nafasi yake kwa mujibu wa katiba ya CDM, kama ndivyo, je ni utaratibu gani ulitumika wa kumuinstall, je document zilizomuhalalisha zipo na zipo valid hadi sasa?Kila ilivyo, wanasheria wazipuuze hata chembe ya factor yoyote inayoweza kutumiwa kumkwamisha mgombea, otherwise muda hautatosha kujitetea mahakamani kama ilivyokuwa kwa Wenje kule Mwanza, uchaguzi ule ulikuwa wa miezi mitatu lakini huu utakuwa wa wiki tatu tu, mahakama ikimaliza kusikiliza rufaa kabla haijatoa uamuzi uchaguzi utakuwa umekwisha, ngoma itabidi ije ianze upya!
MIBA YA MGUNGA HAIUCHOMI MGUNGA!