Mpanda Merikebu
Senior Member
- Dec 27, 2007
- 170
- 2
Hey, mimi ni bro....
Good lookin out bro!
Hey, mimi ni bro....
Aaaaw! Thank you so much! I feel so lonely sometimes. I feel like everybody hates me. Yes, I know I'm hard to deal with but really, I'm a good natured person. Nobody loves me. Nobody listens to me. I just call things as I see them. No need to be complicated. Sorry I'm rambling but I just had to get things off my chest. I hate to see people being mistreated and when you call out the whole society people get mad at you. I'm just mad. Mad at even myself. If I had my way, no one would die violently like that. Everyone would be treated with dignity and respect. But I'm just Nyani, a monkey. What can a monkey possibly do to change the world?
Kitila, nasema hivi, sisi Miafrika ni ndivyo tulivyo! Narudia tena, sisi Miafrika ni ndivyo tulivyo. Nitukaneni, nikasirikieni, fanyeni mnalotaka kunifanyia, uzuri wa ukweli ni kuwa ukweli hubaki kuwa ni ukweli hata iweje.
Haya ya kujichukulia sheria mkononi na kutoa roho za watu kisa wameiba hayajaanza leo. Tokea niko darasa la kwanza nilipoanza kujua kusoma na kuandika nimekuwa nikiyasoma na nimeyashuhudia mimi mwenyewe yakitokea. Usiombee mtaani mtu apige kelele za wewe mwizi! Kitakachofuatia nadhani unakijua.
Nina uhakika kabisa, kulingana na simulizi za wakubwa zangu kuwa haya ya kujichukulia sheria mkononi yamekuwepo kabla ya hata mimi kuzaliwa (I'm a seventies baby, by the way). Miaka yote hii hakuna la maana lilifanyika kukabiliana na unyama huu, why? Yaani hivi sasa tumekuwa desensitized mpaka tunaona kuwa ni kawaida ukikamatwa unaiba wewe ni kibano mpaka ufe. Ustaarabu wetu sisi kama jamii uko wapi? Tukiambiwa wazungu walikuja kutustaarabisha tunang'aka na kuwa wakali kwa wakati huo huo tunafanya mambo yasiyo ya kistaarabu.
Man, I've had it up to here. We are a joke, beyond a joke when it comes to the rule of law. Hivi wakati wa mkoloni yalikuwepo kweli haya? Nyie vidingi humu ndani hebu tuambieni?
I really don't care what y'all think of me. None of you know me like that anyway. To hell with political correctness. Miafrika Ndivyo Tulivyo. Deal with it
Asante sana...wakati nikiwa umri wa hao watoto nilikuwa natakiwa niwe nyumbani mara moja ifikapo saa kumi na mbili jioni!! Hao watoto ni vibaka na kwa taratibu za bongo, kabla hata ya mkoloni kuingia, kibaka akikamatwa anapewa "kisago" mpaka kufa!
Hata Serikali ikiwa ya Rais Mbowe, mambo yatakuwa vivyo hivyo kwani ndio utaratibu wenyewe.....watu wanajisahau sana hapa JF, kuna mwingine ati yupo outraged kwasababu Nipashe wameweka picha ya Mbusi akichinjwa kwikwikwikwi, utafikiri ni jambo geni!!! Mwingine ana compare issue ya hawa "vibaka makinda" na "known-unknowns" wa Greece au yanayotokea Thailand. Hivi haya mambo yanafanana hata kidogo au ndio uchu wa kutaka kuona bongo kunawaka moto? Moto mnaoutaka uwake bongo, ukiwaka mtauzima au ndio yengele ukiwa kwa comforts za Gov. Granholm??
Bongolander, kimantiki si sahihi kujichukulia sheria mkononi.Mbaya zaidi kama walivyochangia wengine hapo juu watanzania ndivyo tulivyo kwani mtaani watu huchoma wezi moto kwa kuwavisha matairi bila ya huruma yoyote badala ya kuacha sheria ichukue mkondo wake.Wakati umefika wananchi tuachane na upotovu huu.Nakubaliana na Nyani Ngabu ya kwamba "Miafrika Ndivyo Tulivyo"Sielewi nini lengo la mwandishi kutumia kichwa cha habari "watoto wa shule" baada ya wezi au vibaka. Inaonekana kama anataka kutumia shule ya msingi kama defence kwa wezi hao. Mwizi ni mwizi tu, hao ambao wameiba mabilioni kama wanavyosema members wengine, nafasi ikipatikana sheria ya kundi itafuata mkondo wake, kama sheria ya mahakamani itabanangwa na kuchezewa kuna uwezekano watu waka-act.
Umma waua watoto wa shule kwa mawe
2008-12-10 16:16:56
Na Godfrey Monyo
Quote:
Watoto wawili wa Shule ya Msingi Manzese jijini Dar es Salaam wameuawa kikatili na watu wenye hasira kwa tuhuma za kuiba vioo viwili vya pembeni mwa gari.
Marehemu hao ni Emmanuel Malobya (16) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la sita na Bakari Ramadhani (14) anayesoma darasa la tano.
Tukio hilo linadaiwa kufanyika usiku wa Jumamosi katika eneo la Legho, Barabara ya Shekilango na watoto hao kupigwa na watu wenye hasira hadi kufa kwa kutumia silaha mbalimbali yakiwamo mawe na fimbo.
Wakizungumza na Nipashe wazazi wa watoto hao kwa nyakati tofauti, walisema watoto wao hawakuwa na tabia za wizi.
Khalifan Nkinga mjomba wa Emanuel alisema kuwa siku ya Jumapili aliletewa taarifa za kuuawa kwa watoto wawili na kuamua kufuatilia kwa sababu mtoto huyo hakurudi nyumbani siku hiyo na sio kawaida yake.
Alisema baada ya kufanya utafiti wa kutosha ilibainiki kuwa watoto hao walipelekwa katika Hospital ya Mwananyamala na alipofika huko alikuta tayari wamehifadhiwa katika chumba cha maiti.
Nkinga alisema kuwa mtoto huyo ni yatima na alimleta kutoka Shinyanga kwa lengo la kumsomesha na alikuwa anatarajia keshokutwa amsafirishe kwenda Shinyanga kwa ajili ya mapumziko.
Hata hivyo, mlezi huyo amelilalamikia Jeshi la Polisi kwa kuwataka kuandika barua maalum zinayoonyesha kuwa watoto hao waliuawa na watu wenye hasira kali.
Alisema kuwa anaamini kuwa mtoto wake aliuawa na askari walikokuwa lindoni katika hoteli moja iliyopo katika eneo hilo la Legho.
Mjomba huyo alisema kuwa anachotaka yeye ni lifunguliwe faili la mauaji na ufanyike uchunguzi na sio kuanza kulazimishwa kukubali jambo ambalo halijafanyiwa uchunguzi.
``Hapa kuna ukweli unataka kufichwa, sasa itawezekana vipi tuambiwe tuandike maelezo ambayo sisi hatukuwepo wakati tukio linatokea,`` alisema mjomba huyo.
Baba mzazi wa Bakari, Ramadhani Bakari, alisema kitendo cha kutakiwa kuandika barua ya kukiri kuuawa kwa mtoto wao na watu wenye hasira kali kimewashangaza.
Alisema kuwa nafsi yake ingeweza kutulia kama polisi wangempa mwili wa mtoto wake ili amzike na mambo mengine yafuate.
Baba huyo akiongea kwa huzuni, alisema kuwa kamwe hawezi kushindana na serikali bali atafanya kama anavyoelekezwa ili mradi apewe mwili wa mwanaye.
``Nategemea kama wakinipa mtoto wangu nimsafirishe kwenda Morogoro eneo la Konga, lakini nikishamaliza mazishi yake nitakuja kujua nini kilitokea`` alisema Ramadhani.
Nipashe ilipomuuliza Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mwananyamala, Dk Suleiman Mutani, kuhusu kuwepo na taarifa zozote kuhusiana na miili ya watoto hao kupelekwa hospitalini kwake alithibitisha kuwako kwa miili hiyo.
Alisema kuwa watoto hao wanakadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 14 na 15 na waliowaleta walisema walipigwa na watu wenye hasira kali.
``Siwezi kusema wameumizwa eneo gani kwa kuwa bado miili hiyo haijafanyiwa uchunguzi, ninachoweza kusema ni kwamba kweli miili hiyo ipo,`` alisema.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Mark Kalunguyeye, alipoulizwa na Nipashe alisema hawezi kuzungumzia tukio hilo kwa kuwa yuko mbali na ofisi.
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alipotafutwa kwa simu kuzungumzia mauaji hayo, alisema kwa sasa yuko likizo.
Hili ni tukio la aina yake kwa watoto wa shule ya msingi kuuawa na wananchi wanaojichukulia sheria mkononi kwa tuhuma za kuhusika katika tukio la wizi.
Kadhalika, tukio hili linatokea wakati kwa nyakati mbalimbali vyombo vya usalama na viongozi wamewaasa wananchi kujiepusha na tabia ya kuchukua sheria mkononi na badala yake watuhumiwa wote wa makosa ya jinai wafikishwe polisi.
"Tukio hilo linadaiwa kufanyika usiku wa Jumamosi katika eneo la Legho, Barabara ya Shekilango na watoto hao kupigwa na watu wenye hasira hadi kufa kwa kutumia silaha mbalimbali yakiwamo mawe na fimbo."
Watoto wawili wa Shule ya Msingi Manzese jijini Dar es Salaam wameuawa kikatili na watu wenye hasira kwa tuhuma za kuiba vioo viwili vya pembeni mwa gari.