Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
- Thread starter
- #381
Hii bado haijampa uhalali yeyote kuishi na mke wa mtu. Mahakama inapotaka kujiridhisha ili itupe kesi kwa kifungu hiki, inatazama kama matendo ya mlalamikaji yamesabibisha mke/mume akimbie. "matendo"hapa yanaweza kuwa ya namna nyingi, makubwa ikiwa ni ukatili (cruelty),kukosa huduma za kifamilia (maintanance) au kukimbia (desertion) n.k...mahakama haijiridhi kwa kuambiwa maneno matupu panataka ushahidi...kwa kawaida yanapotekea mambo hayo katika ndoa hualeta migogoro, ambayo kabla ya mke/mume kwenda mahakamani kutaka, mathalani kutengua ndoa au usuluhishi, lazima apitie katika mabaraza ya usuluhishi, ambayo yakishindwa ndiyo anaweza kwenda mahakamani. Mahakama inapotaka kujiridhisha "matendo" ya malalamikaji kama yamechangia kitendo cha mlalamikiwa, inaangalia hali zote hizo.
Junius.. naona unakwepa kipengele cha kwanza.. hakuna kosa la kuishi na mke wa mtu...