Bluray
JF-Expert Member
- Mar 25, 2008
- 3,449
- 127
Mnyasa please! Unataka kutuambia hayati baba Kanyama Chiume alikimbia udikteta wa Banda kule Malawi/Nyasaland kuja kuomba hifadhi kwa dikteta JKN, siyo? Dude, does it make any sense to anyone?
Ama kweli fadhila za punda...wewe kweli ungekuwa humu ndani unalumbana kwa Kiswahili (na Kiingereza chako cha mbwembwe nyingi) na kushiriki kama Mtanzania yeyote isingekuwa kwa utu na huruma Mwalimu aliyoonyesha juu ya babako na familia yake?
Umshukuru JKN kwa hicho kiburi na majivuno unayoonyesha hivi leo dhidi yake maana isingekuwa JKN wewe na familia yenu yote mngekuwa wapi maana hata kule Malawi hali hivi sasa ni balaa Ukimwi na dhiki ya ajabu imetawala jamii...Damn you dude!
Kwa masikitiko makubwa nakutaka waombe radhi familia ya Chiume na watu wa Malawi, ambao wengine wanasoma humu, kwa kuchukua irresponsible license na kuwachanganya na mtu asiyewahusu kabisa.
Papara zako hizi za kufakamia watu na mambo bila ya kuwa na werevu wa kutosha zinatosha kumfahamisha mtu yeyote mwenye uwezo wa kutanabahi kuwa wewe huna ujualo zaidi ya kupayuka.
Familia ya Chiume wana historia na deference kubwa kwa Nyerere, maandishi yako ya papara yanadhihirisha huijui familia ya Chiume wala mimi.
Kama umeweza kufanya a serious assumption, wrong one at that, na kuvunja kanuni ya anonymity ya JF, na kupakazia familia ya watu mambo yasiyowahusu kwa nini tufikiri unajua lingine lolote unalotaka kusema?
Huo u bully wako nenda kawafanyie wengine, hapa umekumbana na Blu-Magic mpaka unaona maluweluwe kunifananisha na mtu siye!