VIDEO Mpya ya Maiti Ya Gaddafi Ilivyochezewa

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,080
6522426.jpg

Maiti ya Gaddafi
Video mpya imetolewa ikionyesha kwa

ukaribu zaidi jinsi mwili wa aliyekuwa

kiongozi wa Libya, Kanali Muammar

Gaddafi ukichezewa na kuburuzwa

buruzwa ndani ya gari huku watu wakiupiga picha kwa simu zao.
Baada ya kukamatwa na kuuliwa kwa kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi mwezi oktoba mwaka jana, video nyingi zilitolewa zikimuonyesha akiwa hai kabla ya kuuliwa huku shati lake likiwa limejaa damu.

Katika video hii mpya ambayo imeingizwa kwenye internet wiki hii na kuwa gumzo duniani, maiti ya Gaddafi ikiwa kifua wazi inaonyeshwa kwa ukaribu zaidi huku wanajeshi wa kundi la waasi wakiichezea na kupiga nayo picha.

Haijajulikana ni kwa nini VIDEO hiyo imetolewa sasa lakini video hiyo imekuwa gumzo duniani kufuatia mwanaharakati Sami al-Hamwi kuweka linki kwenye Twitter akisema kuwa rais wa Syria Bashar Assad aiangalie video hiyo kwa ukaribu ili ajifunze yaliyomkuta dikteta mwenzake wa Libya.

Gaddafi aliitawala Libya kwa miaka 42 kabla ya utawala wake kupinduliwa mwaka jana na yeye mwenyewe kuuliwa na maiti yake kuzikwa jangwani.

Angalia VIDEO ya maiti ya Gaddafi chini.

<tbody>
</tbody>



VIDEO Mpya ya Maiti Ya Gaddafi Ilivyochezewa
 
Last edited by a moderator:
Ni burdani tosha na somo kwa watawala wetu wezi na wajinga. Nimeiangalia zaidi ya mara saba na kujisikia furaha ingawa si vizuri kushabikia kifo cha binadamu. Hakuna film zenye kufurahisha na kufundisha kama ile ya mauaji ya Samuel Doe, kunyongwa kwa jahid Saddam na hii ya kufilishwa kwa Gaddafii. Malipo ni hapa hapa duniani. Heri mbwa kama Mobutu, Bongo, Eyadema, Banda, Kenyatta, Mengistu, Mugabe, Abacha na wengine yangewakuta haya.
 
Duh, watu walikuwa wamekula si milungula au bangi! Lol kweli matendo ya mtu yana impact kwenye aina ya kifo.
 
Sasa hebu uliza maisha ya libya baada ya kifo cha gadaffi yakoje??
watamkumbuka milele kenge maji hawa.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Ni burdani tosha na somo kwa watawala wetu wezi na wajinga. Nimeiangalia zaidi ya mara saba na kujisikia furaha ingawa si vizuri kushabikia kifo cha binadamu. Hakuna film zenye kufurahisha na kufundisha kama ile ya mauaji ya Samuel Doe, kunyongwa kwa jahid Saddam na hii ya kufilishwa kwa Gaddafii. Malipo ni hapa hapa duniani. Heri mbwa kama Mobutu, Bongo, Eyadema, Banda, Kenyatta, Mengistu, Mugabe, Abacha na wengine yangewakuta haya.
nakushauri sherehekea kila anapokufa mtawala mbaya maana ni njia ya ziada kuukomboa umma unaoonewa wakati wowote kifo cha muonezi ni kizuri na tuzidi kuwaombea umauti hata viongozi wetu wa kitanzania kwa maana ndio njia rahisi ya adhabu itakayowaondoa huku ikiliacha taifa likiwa salama bado.tofauti na sasa kama tukiamua kutumia nguvu tutaathiri hata watoto na mama zetu maana baadhi ya viongozi wetu hulinda madaraka hata kwa damu za watu mungu akubariki kwa kiboresha siku yangu.
 
....dunia mapito jamani...tusijisahau na kuanza kuhukumu wenzetu...nasi hukumu yatungoja!!!!
 
Nyinyi walibya hamkumuua gaddafi mmejiua wenyewe . Poleni sana ndugu zangu mtakufa njaa sasa kama wasomali.
 
Mimi nina mawazo tofautikidogo kuhusu kuuawa kwa Muammar Gadaffi.Mabeberu wa magharibi na washirika wao,walitumia kisingizio cha kukaa kwa muda mrefu madarakani kwa mtawala huyo.Lakini walinyang'anywa akili na muda mfupi baadaye Waingereza walisherehekea kwa mbwembwe nyingi kutimiza miaka 60 ya kiutawala ya malkia Elizabeth anayepoteza kumbukumbu kwa umri aliokuwa nao.Walishasahau kwamba Muamar Gadaffi alitawala miaka 42 tu.Nikimjibu member wa JF,Father of All,ni kwamba asifurahie hali hii kwani nyuma ya hili kuna uozo mkubwa sana.
Magenge ya siri ulimwenguni yakitumia watawala walafi duniani wanaendesha kampeni chafu za kupora maliasili za watu,kwa kisingizio cha demokrasia na utawala bora.Ukirudi nyuma mwaka 1776 tarehe 01/05 ndipo Genge hili lilipoasisi katiba yake (GREAT SEAL).Ndani ya katiba hiyo haramu kuna maazimio mengi na taratibu nyingi walizoziandika ili kufanikisha azma yao ya kutawala kwa mabavu na dhuluma.Sisi huku tunaambiwa ni siku ya wafanyakazi duniani (May Day)!!Bila ya sisi kujua ya kwamba genge hili limetupatia jina la "USELESS EATERS"!Genge hili linalojulikana kama ILLUMINATI ni hatari kuliko unavyojua.Kwa kifupi Genge hili na mengineyo kama FREEMASON n.k ndiyo yanayodhibiti karibu kila kitu kisiasa,kiuchumi n.k.Hata vyombo vya habari na propaganda zote zinafanywa na magenge hayo.Pointi yangu ni kwamba sisi nchi maskini afrika tunaona yanayoendelea ni mageuzi ya kisiasa kwa faida yetu,lakini kumbe ni maangamizo yetu sisi na vizazi vijavyo.
Tumeelezwa ya hao mahayawani kwamba wameanzisha gereza maarufu la GUANTENAMO kwa ajili ya magaidi,lakini ukweli hapo ni chuo cha kuwafundisha magaidi wanaotumiwa na mataifa makubwa kuingia na kuanzisha vurugu katika mataifa yale yenye raslimali kama mafuta na madini.Wakishaingia katika nchi fulani wanajulikana kama WAASI.Waasi hawa wanatokea kuwa na nguvu sana kisilaha na katika medani za kivita!Kwa kifupi ni kwamba LIBYA,MISRI ALGERIA na SYRIA ni katika wahanga wa operation hii ya kinyama.Mengine ni BOKO HARAM,AL QAEDA,JANJAWID na AL SHABAB.Yote haya ni magenge madogo yaliyotengenezwa na mataifa makubwa kwa maslahi yao.AMKENI JAMANI!!!Msishangilie tu mambo bila kuyaelewa kilichopo katika hilo.
Vyombo vingi vya habari vipo chini ya Genge hili ILLUMINATI.
Jaribu kutazama ni kwa nini wakati Gadaffi ameuawa walionekana wanaofurahia kifo chake!!Je ina maan ahakuna binadamu yoyote aliyehuzunika????Hili ni jambo la kufikiri kabla ya kushangilia.
 
Back
Top Bottom