Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,082
Damu ya nguruwe kwenye sakafu ya eneo la msikiti | Thursday, August 02, 2012 5:50 AM Wakati waislamu wakiendelea na mfungo wa mwezi mtukufu wa ramadhani, waislamu nchini Ufaransa wameelezea kusikitishwa na vichwa viwili vya nguruwe vilivyotundikwa kwenye geti la kuingia msikitini huku damu ya nguruwe ikitawanywa kwenye sakafu. |
Umoja wa wanafunzi wa Kiyahudi nchini Ufaransa wameungana na jumuiya ya kiislamu nchini Ufaransa kulaani kitendo cha vichwa viwili vya nguruwe kutundikwa kwenye geti la kuingilia msikitini. Tukio hilo limetokea kwenye mji wa Montauban ambako mwezi machi mwaka huu mwanaume aliyejitangaza kuwa yeye ni gaidi wa Al-Qaeda, Mohamed Merah aliwaua wanajeshi wawili wa Ufaransa. Vichwa viwili vya nguruwe vilining'inizwa kwenye geti la kuingilia msikitini huku kiasi kikubwa cha damu ya nguruwe kilimwagwa kwenye sakafu ya kuingia msikitini. Waislamu walioenda msikitini kusali sala ya alfajiri jana jumatano walikumbana na vichwa hivyo vya nguruwe vikiwa tayari vimeishatundikwa kwenye geti la kuingia msikitini. Rais wa msikiti huo uliopo kwenye kitongoji cha Tarn-et-Garonne, Hajii Mohamed alilaani tukio hilo akisema haamini kama mtu mwenye akili zake anaweza akafanya kitendo cha kuishambulia dini ya kiislamu tena katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani. "Tukio kama hili kutokea ndani ya mwezi mtukufu wa Ramadhani kusema kweli halielezeki, ni tukio la kueneza chuki", aliongeza. Umoja wa wanafunzi wa Kiyahudi nchini Ufaransa nao umeungana na waislamu kulaani tukio hilo. Ufaransa ndio nchi yenye waislamu wengi kuliko zote barani Ulaya ikiwa na jumla ya waislamu zaidi ya milioni 4. |
<tbody>
</tbody>
Vichwa Vya Nguruwe Vatundikwa Msikitini