Vichaa wawili walilazwa, sasa pale wodini wakajadili jinsi ya kutoroka pale wodini. Wakaafikiana kwamba wakifika getini wampige mlinzi, mlinzi akikimbia wao watoke nje ya geti kisha watoroke. Wakaondoka wakaenda hadi pale getini, walipofika pale wakakuta geti lipo wazi ila mlinzi hayupo. Wakanong'onezana "dah! Dili limeharibika mlinzi mwenyewe hayupo" kisha wakarudi tena wodini!