Jumuiya ya Vichaa Tanzania (JUVITA) imetishia kuitisha maandamano ya vichaa nchi nzima kupinga kazi yao ya kuokota makopo kuingiliwa na watu wenye akili timamu. Tukio hili limejitokeza baada ya mamia ya makundi ya watu wenye akili timamu kuanza kuokota chupa za maji safi pamoja na makorokoro mengine na kwenda kuyauza ili kujipatia chochote kitu.
JUVITA wanaamini watu hao (waokota makopo) wamenukuu vibaya kauli ya mkazi wa magogoni aliposema kuwa atatoa ajira milioni moja kila mwaka, hivyo wamedhamiria kuandamana hadi magogoni ili kumuomba mkazi huyo kuitolea ufafanuzi kauli yake na hivyo kuinusuru kazi yao ya kuokota makopo kwani bila ya kuokota makopo ukichaa wao utapoteza maana.
JUVITA wanaamini watu hao (waokota makopo) wamenukuu vibaya kauli ya mkazi wa magogoni aliposema kuwa atatoa ajira milioni moja kila mwaka, hivyo wamedhamiria kuandamana hadi magogoni ili kumuomba mkazi huyo kuitolea ufafanuzi kauli yake na hivyo kuinusuru kazi yao ya kuokota makopo kwani bila ya kuokota makopo ukichaa wao utapoteza maana.