Vibwanga Vya ATCL;na Viongozi wake!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,139
Tuhuma za wafanyakazi ATCL zifanyiwe kazi haraka


Najivunia kuwa Mtanzania, naipenda nchi yangu, wakati wowote nipo tayari kuitetea sifa ya nchi hii na kamwe sitamuonea haya ye yote aliye kikwazo cha maendeleo ya Tanzania aidha kwa kufahamu au kutofahamu, kwa kutumiwa au kwa maslahi yake binafsi.

Ni kutokana na mtazamo huo, nadiriki kusema kwamba yanayotokea sasa katika Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) yanasikitisha na ni aibu, hivyo serikali inapaswa kuchukua hatua haraka ikiwa ni pamoja na kuzifanyia kazi tuhuma za wafanyakazi wa kampuni hiyo.

Kauli za wafanyakazi hao zimenifurahisha, si kwamba nimethibitisha kuwa ni za kweli, ni kwa sababu wamesema wanachoamini, wameeleza hisia zao na kutoa msimamo, nashawishika kuamini kuwa waliyasema hayo kwa kuongozwa na uzalendo na si chuki binafsi, aidha kwa Mkurugenzi Mtendaji na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, David Mattaka au viongozi wengine.

Naamini kuwa serikali imeelewa, tatizo ATCL si upungufu wa ndege au ukosefu wa fedha tu, wafanyakazi hawana imani na utawala ulio chini ya Mattaka na Bodi ya Wakurugenzi inayoongozwa na Balozi Mustafa Nyang’anyi.

Kuna mambo ya msingi yanayostahili kufanyiwa kazi haraka, hayahitaji uchunguzi au utafiti, hayahitaji mwongozo wa sera au fedha za kigeni, mfano, kurudisha uhusiano mzuri kati ya menejimenti na wafanyakazi.

Hata kama ATCL itakidhi masharti ya usalama, hata kama ndege zake zote zitakuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa asilimia 100, ni ndoto kwa kampuni hiyo kupata mafanikio kama hakuna uhusiano mzuri kati ya utawala na wafanyakazi.

Sina mamlaka ya kusema tuhuma za wafanyakazi wa ATCL ni za kweli au la, lakini nina wajibu wa kuiomba serikali isizipuuze, ufanywe uchunguzi ili kufahamu tatizo ni nini na nani kasababisha. Busara itumike ufumbuzi upatikane haraka iwezekanavyo, Watanzania wana haki ya kujivunia alama hiyo ya Tanzania na si kusononeka.

Upendeleo, kujuana, huyu ni mwenzetu, na rushwa visiwe na nafasi katika mchakato wa kurudisha hadhi ya ATCL, ye yote anayeonekana kuwa ni kikwazo cha mafanikio katika kampuni hiyo awekwe kando kwani ni chombo cha Watanzania, fahari ya Watanzania, mali ya Watanzania na ipo kwa ajili yao, hivyo maslahi ya taifa yazingatiwe.

Ni kwa kuzingatia hilo, ikithibitika kuwa kuna udhaifu wa kiutendaji katika menejimenti, wahusika waondolewe haraka, jukumu hilo wakabidhiwe wenye uwezo wa kuiongoza ATCL kwa ufanisi, watakaoiwezesha kampuni kumudu ushindani kwa kibiashara katika usafiri wa anga ndani na nje ya Tanzania.

Sioni tatizo kumuondoa Mattaka katika uongozi wa kampuni hiyo kama ikithibitika kuwa yeye ni tatizo ATCL, na pia sitashangaa endapo Bodi ya Wakurugenzi itavunjwa kwa manufaa ya umma kama imeshindwa kusimamia menejimenti.

Ninaamini kuwa Rais Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Waziri wa Maendeleo ya Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa; wapo makini kutafuta ufumbuzi wa matatizo ATCL, na sina shaka kuwa uamuzi wa serikali utakuwa wa haki na utazingatia maslahi ya taifa.

Kwa kuwa wafanyakazi wa ATCL wameonyesha nia ya kuandamana kwenda Ikulu, Waziri Kawambwa akazungumze nao, wapewe nafasi ya kusema waliyonayo, na awaeleze serikali inafanya nini ili kurudisha hadhi ya kampuni hiyo.
 
ATCL hali si shwari

Hali si shwari katika Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), baina ya uongozi wa juu na wafanyakazi na kuna taarifa kwamba wafanyakazi wamegoma kwenda likizo bila malipo.Kuna taarifa kwamba Ijumaa wiki hii Mkurugenzi Mkuu na Ofisa Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo, David Mattaka, aliwaeleza wafanyakazi hao kuwa kwa hali ilivyo kampuni haiwezi kuendelea na idadi iliyopo ya wafanyakazi hivyo, aidha itabidi baadhi wapunguzwe au waende likizo bila malipo.

Chanzo cha habari hizi kilidai jana kuwa, katika mkutano huo uliofanyika katika jengo la ATC jijini Dar es Salaam Mattaka alishindwa kujibu baadhi ya hoja za wafanyakazi hao likiwamo swali kwamba, uongozi unataka wafanyakazi wangapi waendel likizo bila malipo na itakoo kiasi gani.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, suala la kupunguza wafanyakazi lilionekana ni gumu kwa sasa kwa madai kuwa Serikali haina uwezo wa kuwalipa mafao watakaopunguzwa, na ikiwezekana mchakato huo utafanyika Juni mwaka huu.

Inadaiwa kuwa, uongozi wa ATCL umeamua baadhi ya wafanyakazi waende likizo bila malipo hadi zitakapopatikana fedha za kuwapunguza wafanyakazi.
Jana alasiri Mattaka hakukanusha kukutana na wafanyakazi hao na akasema kuwa atazungumzia suala hilo kesho Jumatatu.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari hizi, wafanyakazi walipinga kupunguzwa kwa madai kuwa suala hilo halipo katika sheria za kazi na wana mashaka huenda watapoteza nafasi zao za ajira wakati kampuni kutoka China itakapokuja kuwekeza.

Chanzo hicho kilidai kuwa, wafanyakazi walimweleza Mattaka kuwa, kama unaona wapo wengi uongozi wa kampuni utafute fedha za kuwapunguza na si kuwapeleka likizo bila malipo na wakishindwa hilo wairudishe kampuni kwa mwenye mali.

Wafanyakazi hao wanatarajiwa kukutana na uongozi wa chama cha wafanyakazi katika kampuni hiyo kesho au keshokutwa, Jumatano Mattaka atakutana na viongozi wa wafanyakazi ili kufahamu wameamua nini.

Msemaji wa Wizara ya Maendeleo ya Miundombinu, Martin Ntema alisema jana kuwa, mkutano wa Mattaka na wafanyakazi ni mchakato wa ndani wenye lengo la kuboresha huduma za usafiri wa anga.

“Hawajashindwana, wakishindwana ndiyo wanakuja wizarani”alisema Ntemo na akabanisha kwamba kwa nyakati tofauti, Waziri wa wizara hiyo, Dk Shukuru Kawambwa amekuwa akizungumzia suala la wingi wa wafanyakazi ATCL kuwa ni miongoni mwa vikwazo vya ufanisi.
 
ATCL sasa kwafukuta

Hatua ya kusimamishwa kwa Shirika la Ndege Nchini (ATCL) kutoa huduma za usafiri wa anga, imeibua hasira za wafanyakazi, wanaotaka menejimenti na Bodi ya Wakurugenzi wake, kuondolewa madarakani.

Hali hiyo ilijitokeza jana, ikiwa ni siku moja baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL, David Mattaka, kufafanua kuwa, hatua hiyo, ilitokana na ukosefu wa kumbukumbu za maandishi zinazotambuliwa na Mamlaka ya Kimataifa ya Usafiri wa Anga (ICAO).

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika kikao kilichofanyika uwanja wa ndege wa zamani, jijini Dar es Salaam, wafanyakazi hao waliishutumu menejimenti kwa kushindwa kushughulikia kwa wakati, kero zinazoikabili ATCL.

Mmoja wa wafanyakazi hao, Michael William, alisema kutokana na utendaji mbovu wa mamlaka hizo katika ATCL, kuna haja ya kuandamana hadi ofisi ya Rais, ili kumtaka atengue uteuzi wa Mattaka.

``Viongozi wetu wa COTWU (T) watuunge mkono ili tutangaze maandamano ya kwenda Ikulu kesho, kumtaka Rais atengue uteuzi wa Mattaka,`` alisema.

Alisema, kwa hali ilivyo sasa, hakuna sababu ya kuwepo vitendo vya kubaguana miongoni mwa wafanyakazi, bali kuungana kwa lengo la kudai haki itakayofanikisha kuliokoa shirika hilo.

Naye Omar Hamad Omar, alisema ingawa kuna watu watakaovujisha siri za mpango wa wafanyakazi kwa menejimenti, taswira iliyopo ni kuwa, (wafanyakazi) hawaitaki (menejimenti).

``Wapo wafanyakazi, walio wadogo na hata wazee, watakaoenda kubinya pua zao kwa menejimenti na kutoa siri zetu, lakini wallaah, ilivyo sasa ni kwamba hatuitaki hii menejimenti,`` alisema.

Mfanyakazi mwingine, Maurice Mtaza, alidai kuwa, mapungufu mengine yanayoikabili ATCL, ni menejimenti kushindwa kutoa mikataba ya ajira ama barua za uthibitisho kwa baadhi ya wafanyakazi kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita sasa.

Kwa upande wake, Kaleb Samson, alisema wafanyakazi wenye umri mdogo katika ATCL, wana wajibu wa kuhakikisha kuwa, shirika hilo linaendeshwa kwa misingi ya uwazi ili kufikia malengo yake.

Alisema hivi sasa, kiwango cha utendaji wenye kufuata misingi ya uwazi, ni kidogo na hakikidhi uwezo wa kutatua kero za shirika.

Alitoa mfano kuwa, kuna maamuzi yanayofanywa, mathalani katika suala la manunuzi ya mali zinazogharimu fedha nyingi, bila kuwashirikisha wafanyakazi.

Pia, Samson alipendekeza kuwepo vikao vyenye lengo la kufanya mapitio ya utendaji kazi wa menejimenti, Bodi ya Wakurugenzi na wafanyakazi.

Wakati wafanyakazi hao wakisubiri tamko la uongozi wa wafanyakazi kuhusu kuandamana, kuikataa menejimenti na Bodi ya Wakurugenzi, Naibu Katibu wa COTWU (T), tawi la ATC House, Bonaventura Sagamilwa, alisema hoja za wafanyakazi hao zinastahili kujadiliwa katika kamati ya chama hicho.

Alisema kwa hatua hiyo, kamati hiyo itaibua njia bora inayofaa kuwasilisha madai hayo kwa mamlaka husika.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa COTWU(T)-Taifa, Buhari Semvua, alisema kikao cha kamati hiyo kinapaswa kuharakisha majumuisho ya hoja za wafanyakazi , ili kuziwasilisha kwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Mathias Mjema, Jumatatu ijayo.

Alisema tatizo lililopo ATCL, linaonekana kuchagizwa na dhana ya wazalendo wenye tabia za kikaburu katika utendaji kazi wao.
 
Waziri akataa ripoti ya ATCL


Waziri wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa, ameiponda ripoti ya Bodi ya Shirika la Ndege Nchini (ATCL) iliyowasilishwa kwake, kuwa haina maelezo ya kutosha kuhusu matatizo ya shirika.

Badala yake, ameunda kamati ya watu sita kuchunguza kiini cha matatizo yaliyoliyumbisha shirika hilo.

Kadhalika, amesema Shirika hilo limerejeshewa leseni yake ya biashara baada ya kutimiza vigezo vilivyotakiwa na Mamlaka ya Kimataifa ya Usafiri wa Anga (ICAO) na ndege zake zitaanza safari wakati wowote.

Akizungumza na Anga (ICAO) na ndege zake zitaanza safari wakati wowote.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Dk. Kawambwa ambaye pia alikiri kuwa menejimenti ya shirika hilo ina kasoro, alisema ripoti hiyo imemwachia maswali mengi yasiyo na majibu.

Waziri alisema kuna mambo mengi ambayo anahitaji kuyafahamu, lakini hayakuainishwa kwenye ripoti hiyo ambayo alisema ilikuwa na kurasa chache.

Kamati hiyo ilianza kazi Desemba 29 mwaka jana na ameipa siku 21 kukamilisha kazi yake.

Alisema endapo kamati hiyo itamshauri kuvunja menejimenti ya shirika hilo hatasita kufanya hivyo.
Wakati huo huo, alisema tayari ameiagiza menejimenti kuwachukulia hatua za kinidhamu wale waliohusika kulifikisha shirika hapo lilipo.

Aidha, alisema endapo menejimenti itatoa adhabu kwa watumishi wa shirika ambayo hataridhika nayo atawashughulikia yeye mwenyewe.

Aidha, Dk. Kawambwa alisema hadidu za rejea za kamati hiyo inayoongozwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi, Profesa Idrisa Mshoro, ni kujua kwa kina matatizo ya shirika, vyanzo muhimu vya matatizo na baada ya hapo ipendekeze mikakati na hatua za kuchukua kulifanya shirika hilo lijiendeshe bila matatizo.

Alisema awali isingekuwa rahisi kuwashughulikia watu waliohusika na uzembe kwa kuwa ingekuwa vigumu kwa shirika hilo kurekebisha kasoro zilizopo ili kurejeshewa leseni tayari kwa kuendelea na biashara.

``Tungewawajibisha watu waliozembea kabla hatujarudishiwa leseni hivi hizo kasoro angerekebisha nani, tulipokaa kimya maana yetu ilikuwa tuweke mambo sawa kwanza, lakini sasa tunaweza kuwajibishana kwa kuwa leseni tayari tunayo,`` alisema.

Alisema ili shirika hilo liweze kuanza biashara linahitaji Sh. bilioni 3.3 na tayari serikali imeshalipatia Sh. bilioni 2.5 na kwamba linadaiwa zaidi ya Sh. bilioni 9.1 na wadau wanaolipatia huduma mbalimbali.

Alisema serikali italipa mishahara kwa wafanyakazi wote inayokadiriwa kufikia Sh. milioni 320 ikiwa ni hatua ya kulinusuru ili liendelee kufanya biashara.

Alisema serikali itaendelea kuliwezesha shirika hilo kifedha na kuliongezea ndege ili kukidhi mahitaji yaliyopo.

Dk. Kawambwa alisema tayari serikali inafanya mazungumzo na shirika moja la China ili kuangalia uwezekano wa kuingia ubia na ATCL.

Alisema safari hii serikali itakuwa makini zaidi ili isije ikaingia ubia na shirika la kibabaishaji na hatimaye kupata hasara kama ilivyokuwa kwa Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA).

Alisema ATCL inapaswa kujipanga upya ili ndege hizo zianze safari zake kama kawaida na idumishe viwango vya kimataifa ili isije ikapokonywa leseni ya biashara tena.

Alisema ATCL ina ndege mbili tu, lakini wafanyakazi 300 na alisema endapo itabainika wafanyakazi ni mzigo kwa shirika watapunguzwa.

Alisema ndege hizo zinazofanya kazi kati ya Mwanza na Mtwara zina uwezo wa kuchukua abiria 50 kila moja, na ndege moja ya kukodi Air Bus A320 ina uwezo wa kuchukua watu 150.

Wajumbe wa kamati hiyo ni Marcelina Chijoriga, Dk. Ibrahim Juma, Mussa Assad, Dk. Gideon Kaunda, Dk. Hamis Kibola na R. Mango.

Mkurugenzi Mtendaji wa (ATCL), David Mattaka alisema hivi karibuni kuwa shirika hilo limesimama kutoa huduma kutokana na kunyang\'anywa leseni na Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) kutokana na mapungufu mengi ya kiutendaji.

Alisema ukaguzi uliofanywa na taasisi ya Ukaguzi ya Kimataifa ya Usalama wa Anga IOSA Desemba mwaka jana ulibaini mapungufu 482 ya viwango, kwa mujibu wa Mamlaka ya Kimataifa ya Usafiri wa Anga (ICAO).

Alisema mapungufu hayo yalibainika katika idara za oganaizesheni na utawala, miruko ya angani, usafiri, matengenezo, cabin, huduma za ardhini, mizigo na usalama.

Mattaka alisema kasoro hizo hazikuwa kubwa kiasi cha kuweza kuathiri usalama wa ndege na abiria
 
Habari za Kitaifa Habari zaidi!
COTWU yapinga likizo bila malipo ATCL


Chama cha Wafanyakazi wa Mawasiliano na Uchukuzi Tanzania (COTWU) kimepinga mpango wa uongozi wa Kampuni ya Ndege (ATCL) kuwapeleka wafanyakazi likizo bila malipo, ingawa wako tayari kuachishwa kazi.

Taarifa kutoka ndani ya kampuni hiyo zilisema leo kuwa uongozi wa Cotwu ATCL ulitoa msimamo huo kwa Mkurugenzi Mkuu, David Mattaka, katika mkutano uliofanyika leo Dar es Salaam.

Mmoja wa viongozi wa juu wa Cotwu tawi la ATCL ambaye hakuta jina lake liandikwe gazetini, alisema hawakukubaliana chochote na Mattaka, hivyo walimwomba idhini ya kukutana na wafanyakazi leo, ombi ambalo alilikubali.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika mkutano huo, Mattaka aliwaeleza viongozi hao kwamba kinachofanywa na uongozi wa kampuni ni agizo la Serikali la kutaka kupunguzwa kwa idadi ya wafanyakazi ili iweze kujiendesha kwa ufanisi.

Hata hivyo, wafanyakazi kupitia chama chao, walimweleza Mattaka kuwa wako tayari kuachishwa kazi lakini wanapinga kwenda likizo bila malipo kwa kuwa sheria za kazi hazitambui hilo. Gazeti hili halikuweza kumpata Mattaka kuzungumzia suala hili. Ijumaa iliyopita, wafanyakazi hao walipinga mapendekezo ya kutakiwa kwenda likizo bila malipo baada ya kuelezwa na uongozi kwamba kampuni haiwezi kujiendesha kwa idadi ya sasa ya wafanyakazi na haina fedha za kuwaachisha kazi.
 
Watoto na Wajukuu wa Mafisadi-ATCL wazinduka




Wapiganaji, nimepenyezewa taarifa hii na wafanyakazi wa ATCL- Haitii kichefuchefu bali ni kinyefunyefu! Hebu tuijadili!

Sisi wananchi tuliyo ndani na nje ya ATCL tumeona hatuwezi kukaa kimya tukiangalia jinsi kampuni inavyoangamia kwa ufisadi wa kisayansi.

Ufisadi wa kisayansi kwa sababu wanaofanya ufisadi huu ni uongozi wa kampuni kwa kutumia nafasi zao za madaraka na kujifanya huo ndio uongozi.

Tuanze kwa kueleza ni maeneo gani yenye ufisadi halafu tutaje viongozi hao na sifa zao.

Tutataja maeneo yenye ufisadi na matumizi mabaya ya mapato ya kampuni na mikopo toka mabenki mbalimbali. Pia safari zilizo nyingi na za muda mrefu bila kujali gharama na faida za safari hizo.Manunuzi ya magari kwa fedha za mikopo na bila kufuata taratibu. Mwisho ni hila za kuwafukuza ama kuwaondoa katika nafasi nyeti wafanyakazi wa zamani na kuweka wapya ambao huajiriwa kiholela na bila ya sifa zinazolingana na kazi zenyewe au hata na wale waliyoondolewa.

Jopo la viongozi na sifa zao zinazoangamiza kampuni ni:-
1. Mkurugenzi mkuu wa kampuni ni David Mataka.
Yeye aliteuliwa na Rais JK baada ya rais aliyemtangulia kumtimua kwa ufisadi. JK alimuonea huruma DM baada ya kukaa ubaoni kwa muda na pia kushindwa kinyang'anyiro cha ubunge kwa tiketi ya chama tawala. Wananchi wa jimbo lake na wa chama chake hawakumpa kura kwa kuwa alikwisha onekana mbele ya rais BM kuwa ni fisadi wa hali ya juu japo yeye rais BM alikuwa anawakumbatia mafisadi kama Balali.
Mkuu huyu wa kampuni ameanzisha uongozi wa dharura(Management by crisis) ambapo kila asubuhi wakurugenzi na mameneja wateule katika ufisadi hukaa vikao vya kuangamiza kampuni. Amepata Benz ya kisasa katika mgao wa magari yaliyotolewa na wauzaji baada ya kununua magari ya kampuni huko Dubai kwa bei ya juu. Magari hayo ni ya mwaka 1998 japo bei yake ni karibu na mara mbili ya yale yanayouzwa na makampuni mengine ya Dubai. Yeye huwa anasuka jambo halafu anamwachia George, Eliasaph au William walichochee katika kikao cha hao viongozi.

2. MARK MANJI
yeye ni mtu HATARI wa Musoma japo jina lake la kihindi. Huyu ni mshauri wa mkurugenzi mkuu. Alikuwa mkurugenzi wa idara ya operations wakati wa makaburu japo idara hii huwa inaongozwa na marubani. Alipewa cheo hiki na makaburu ili kuwaweka marubani katika himaya ya makundi. Makaburu walipoondoka aliomba kuacha kazi kwa hiari na akastaafu akaomba kuendelea na kazi tena kama mshauri wa mkurugenzi mkuu. Kwa kuwa alikuwa na mapenzi na makaburu na kwa kuwa ameshapata mafao yake, hana huruma na kampuni kwa sasa badala yake yeye ni kichocheo na hujifanya analijua shirika. Anatumia utoto wa mjini kufanya kazi kwani hana shahada hata moja japo amepewa nafasi nyeti.

3. Eliasaph Mathew
aliajiriwa na makaburu kama meneja wa fedha kwa maana hiyo ni mtu wa makaburu. Baada ya mkurugenzi wa fedha aliyekuwa kaburu kuondoka amekaimu nafasi hiyo hadi leo. Huyu ndie kinara wa kupindisha taratibu za matumizi ya fedha na ununuzi. Ni mfuasi namba moja wa DM kwani kwa sasa pesa za kampuni hutolewa kiholela kulipia gharama kwa ufisadi. Mfano kabla ya kufunga mwaka 2007 shillingi millioni mia mbili hamsini zilichotwa kulipa gharama za kutoa magari nane yaliyokuwa katika yadi ya kuweka mgari iliyo ya watu binafsi. Haishi hapo huchota dola elfu tatu taslimu toka kwa mtunza fedha kila mwezi na kumpa huyu mwenye yadi ya kuhifadhi magari. Huidhinisha malipo kwa ankara tu bila kujali taratibu nyingine. Ndiye aliyejumuika katika jopo lililokwenda Dubai kuchagua magari ya kampuni na kuyanunua kwa bei mbaya bila kufuata taratibu za ununuzi. Magari haya ni ya 1998 japo ATCL ni mali ya serikali,hilo halikutiliwa maanani. Yeye amepata zawadi ya VX Landcruiser ya kisasa kama mgao katika hayo manunuzi na sasa ameweka pembeni Vitara yake. Hutumiwa katika mikakati ya kuwaondoa watu wa zamani na wenye sifa kwa kuwazulia kesi na shutuma za matumizi mabaya ya pesa kitu ambacho si kweli.
Waliyoonja joto hilo ni pamoja na Hassani ambaye aliamua kuacha kazi, Hamisi na Mndeme ambao wamesimamishwa kwa suala la bwana Mohamed Makaratasi ambaye ni rafiki wa George Mazula.amebadilishwa cheo baada ya aibu kuikuta atcl

4. George Mazula
yeye eti ndiye rubani kiongozi na mshauri wa DM. Huyu aliwahi kuachishwa kazi wakati mwenyekiti wa bodi alikuwa ni Abasi Sykes. George aliwahi kuunguza injini mbili za Fokker kwa mpigo pale Tanga. Amewahi kuangusha ndege aina ya Fokker hapa Dar es salaam. Amewahi kuua mtu pale uwanja mpya wa JK Nyerere kwa kukatwa na pangaboi baada ya yeye kuzembea kuzima injini. George ni kiungo wa mikakati yote ya ufisadi na kuondolewa watu katika nafasi zao. Alikuwa mfadhili wa DM wakati akiwa ubaoni. Ni rubani mwenye makeke na mikosi mingi. Katika dili ya Dubai yeye amepata Volvo na kujidai amekopa.maskini sasa ni marehemu;walimuingiza kwenye mnyoror wa kifisadi,natumaini aliombamsamaha kwa muumba wake

5. Amin Mziray
Danger zone;huyu ni katibu wa kampuni. Yeye ni chapombe. Alipewa gari ya kampuni na makaburu na kulipindua kwa ulevi. Anayo shahada ya sheria lakini haitumii kwa maslahi ya kampuni. Kampuni imeshindwa kesi nyingi kwa kutokuwa makini huyu mwanasheria. Yumo katika hili jopo la ufisadi wa kampuni. Katika mgao wa magari ya Dubai yeye amepata VX Landcruiser la nguvu. Hayupo tayari kutetea hoja mbovu zinazotolewa ndani ya vikao vya hili jopo la ufisadi.

6. William Haji,
anakaimu nafasi ya mkaguzi mahesabu wa ndani. Aliajiriwa wakati wa makaburu kama mkaguzi wa mahesabu wa ndani chini ya bwana Yakubu. Baada ya muda bwana YAkubu aliwekwa pembeni na huyu bwana kukaimu nafasi yake. Kwa sasa yeye ndiye anayekagua malipo (Pre-audit) hivyo yumo ndani ya mtandao wa ulaji. Ndiye anayetumiwa kutengeneza taarifa za kuzua kesi na uonevu kwa wafanyakazi wa chini. Huchukua nafasi ya afisa usalama wa kampuni ili kupindisha ukweli na hatimaye kuwadhalilisha ama kuwatimua wafanyakazi wasiyo na hatia. Ni hatari sana kwani yupo karibu na DM na Eliasaph katika kila mpango.MASKINI WAMEMPA CHEO CHA ELIACHAFU

7. Sadiki Muze,
Yeye ni mkurugenzi wa idara ya operations kwa sasa. Amepewa nafasi hiyo yeye kwani ndiye aliyekuwa mfadhili mkuu wa DM wakati akiwa ubaoni. Pia ni mshirika wa DM katika vinywaji na mwanachama wa kijiwe kimoja na George. Ni Sadiki na George pekee waliyopewa vyeo na kuenguliwa wengine baada ya DM kuchukuwa uongozi ATCL na ni chapombe. Sadiki na George wamelipwa fadhila.MASKINI AMEONDOLEWA KABISA NA WALA HAWATAKI KUMSIKIA...KILA LA KHERI

8. Heho Mbiru ni Mkenya,
aliajiriwa kwa nguvu enzi za makaburu kama mkurugenzi wa masoko. Aliajiriwa kwa nguvu na aliyekuwa mwenyekiti wa bodi ya ATCL wakati huo Ali Mufuruki kwa kisingizio kuwa hakuna Mtanzania mwenye uwezo wa kushika nafasi hiyo. Ni mzalendo wa Kenya kweli kweli kwani kazi zinazoweza kufanyika hapa (kama Graphics) huzipeleka kwenye kampuni yake. Anayo mapenzi na makaburu hivyo kuleta mabadiliko tunayotaka yeye ni kikwazo na ndiyo maana ni rahisi kutumiwa katika hujuma. Kumbuka tunaushindani na Kenya Airways huyu atatumaliza.AMEONDOKA ZAKE BAADA YA KUIUA ATCL

9. Ajay Gopinath
raia wa India. Aliajiriwa kwa nguvu wakati wa makaburu na aliyekuwa mwenyekiti wa bodi Ali Mufuruki. Ajay aliwahi kufukuzwa nchini lakini kwa sababu zake Ali alifanya juu chini na kumrudisha kama mkurugenzi wa mauzo. Anatumiwa katika upatikanaji wa fedha na kutumika vibaya. Hana sauti ndani ya utawala huu kwani ni mgeni.NAYE KAFUKUZWA

10. Alphonse Mkinga
huyu kinganganizi atoki;ni meneja utumishi. Alistaafu na kuchukua mafao yake baada ya makaburu kutimka. Anafanya kazi kwa mkataba na kuzuia ajira kwa waliomaliza vyuo.
Ameidumaza idara ya utumishi kwa kutoweka muundo wa utumishi na taratibu mbalimbali za ajira. Matokeo yake mkurugenzi mkuu huleta watu wake japo wapo waliofanya usaili. Mfano ni ajira ya mhudumu katika ofisi ya mkurugenzi mkuu,ajira ya afisa majengo na mali ambaye ni jamaa yake. Huyu bwana Peter Gosh anachukua nafasi ya bwana Hassan Kikoko alieandamwa na huu mtandao wa ufisadi na hatimaye kuamua kustaafu mapema. Yupo dereva aliajiriwa kwa hila japo wapo waliofanya usaili na hadi sasa hawajapata ajira. Bwana Mkinga hana sauti kwani yupo kulinda maslahi yake baada ya kupata ajira ya pili.

11. Fidelis Tarimo;
ni mkurugenzi wa uhandisi. Historia yake ni ufisadi mtupu. Aliwahi kusimamishwa kazi na aliyekuwa mwenyekiti wa bodi wakati huo Mzee Abasi Sykes. Tarimo alikwenda kusimamia matengenezo makubwa ya Boeing ya ATC wakati huo (major check) nchini Ireland. Hakuwa anafuatilia gharama halisi za matengenezo na kujali maslahi yake hivyo kusababisha gharama kupanda kwa shilingi bilioni moja na nusu toka ghrama halisi na kulitia shirika hasara na kusimamishwa kazi. Alipata nafasi wakati wa makaburu kwani hakuwa mtetezi wa wazalendo. Kwa sasa wafanyakazi wa idara yake hawamtaki na wameandika barua ya kumkataa na wizara inajua hilo. Ni bingwa wa kuuza ndege za kampuni kwa bei ya kutupwa badala ya ile ya makubaliano ya awali. Ana ukabila na hadi sasa ana jamaa yake anasimamia ujaji wa ndege ya kukodi kwa muda mrefu yuko nje ya nchi. Ni fisadi wa kutupwa kwa ajili ya kutaka pesa za kuendeleza biashara zake.HUYU ANACHOFANYA HAKUNA TOFAUTI NA MAUAJI YA ALBINO,WE ANALETA SPARE NJE YA NCHI AMA TAIRI ZA NDEGE ALAFU UNAKUTA SIZE TOFAUTI NA BADO ANAENDELEA KUKKAA MHH HUYU MATTAKA SIJUI WAMEMLOGA??

12. Rajabu Itambo ni meneja Galileo Tanzania kampuni tanzu ya ATCL. Rajabu alipewa kazi ya ushauri katika kitengo cha Galileo na aliyekuwa meneja wakati huo Maalim Ali. Kaburu mmoja aliyekuwa mkurugenzi wa biashara Mike Bond aliamua kumuondoa Maalim Ali katika nafasi hiyo na kumuweka Rajabu kwa maslahi yake kwani walitaka kuuza Galileo kabla ya kuondoka jambo ambalo hawakufanikiwa. Mpaka sasa Rajabu ana uhasidi na wafanyakazi wa zamani kwani anataka awe mkuu wa kitengo cha ITC (Information and Technology Communication) Ni mmoja wa vibaraka wa DM.
Hadi tunakwenda mitamboni ATCL haina bajeti na hili linatokana na Eliasaph kutayarisha bajeti hiyo kwa usiri mkubwa akiweka vipengele hewa ambavyo bodi ina wasiwasi navyo hivyo kuikataa kila wakati. Bajeti huwa inatengenezwa na kitengo maalum katika idara ya fedha lakini safari hii imekuwa na usiri mkubwa. Ilibidi iwekwe hadharani kwa wafanyakazi kupitia workers council ndiyo iifikie bodi jambo ambalo halikufanyika.
Kama tulivyoeleza awali matumizi mabaya ya pesa yanapeleka kampuni kusikoeleweka. Pesa huchotwa kama za mtu binafsi bila kujali taratibu za kihasibu. Viongozi hawa kwa vikundi huenda safari kila wakati kuliko viongozi wote waliopita. Posho wanayolipana ni kubwa mno kwa kila siku hivyo hata safari za watendaji wa chini huenda wao. Mwenyekiti wa bodi Mustapha Nyang?anyi aliliambia Sunday Citizen tarehe 12 januari 2008 kuwa uzembe wa menejimenti ya ATCL kutoingia mkataba na kampuni iliyokuwa ikodishe ndege kwa ajili ya mahujaji ndiyo chanzo cha sakata zima la hasara katika usafirishaji wa mahujaji. Ukweli ni kuwa menejimenti haikutaka kushirikisha wafanyakazi wa kawaida kuratibu safari hii kama ilvyokuwa miaka iliyopita. Hii ni kwasababu walitaka iwe siri yao kwa kutafuta ndege ya bei poa kuliko hiyo iliyopatikana kitu ambacho hakikuzaa matunda na hatimaye kusema ATCL haiwezi kusafirisha mahujaji. Mbona kabla ya makaburu iliwezekana. Hapa pana ufisadi sio uzembe tuu. Wapo wazoefu wa kazi ndani ya kampuni lakini wamekodi mtu wa nje Mtambalike rafiki yake DM kwenda kusimamia kurejea mahujaji. Tunasema hii ni hujuma na kuwadharau watendaji wa ndani.
Magari ya kampuni yamenunuliwa kwa bei kubwa bila kufuata taratibu na viongozi wanne kupata magari kutokana na gharama hiyo kubwa na bila kufuata utaratibu wa ununuzi. Hivi sasa kampuni ina madeni mengi kutokana na ufisadi.
Wafanyakazi wasiotakiwa hasa wale wa zamani hutafutiwa sababu za kuwaondoa ili ajira wapewe watu wa DM. Mifano hai tumetaja hapo juu na mingine mingi tunayo kama ule wa Said Ibrahimu kufanyiwa visa na Mark Manji hadi kuamua kustaafu ili yeye Manji aongeze muda alipoamua kustaafu kwa kisingizio kuwa hakuna wa kuchukua nafasi yake.

Kwa sababu tumezungumza kwa kifupi tunaomba yafanyike yafuatayo:-

1. Kuleta wakaguzi kama vile Enerst and Young kukagua mahesabu ya ATCL tangu DM awe mkurugenzi mkuu. Hapa panatosha kuona ufisadi katika:-
(i) Mikopo na over draft na kutafuta jinsi pesa hizo zilivyotumika kwa ukamilifu.
(ii) Kupata maelezo kutoka kwa DM kwa nini toka achukue uongozi ATCL hakubadilisha muundo na uongozi wa makaburu tukijua fika viongozi hao wana maslahi na makaburu.
(iii) Uchunguzi juu ya ununuzi wa magari bila kufuata kanuni na taratibu za ununuzi nje ya nchi na kulinganisha bei na makampuni mengine ya Dubai
(iv) Wachunguzwe hawa viongozi wanne walipataje magari hayo toka kwa kampuni iliyouza magari kwa ATCL kwa bei ya juu. Kama ni mikopo waoneshe pesa walipata wapi na utaratibu mzima wa kuyalipia na kuingiza na kuyakomboa.
(v) Zipatikane sababu za viongozi kuomba kustaafu na kujiajiri tena.
(vi) Uchunguzi ufanywe kupata uhalali wa wafanyakazi wa zamani kunyanyaswa na wengine kusimamishwa kazi kwa hila ili kuajiri wengine kwa maslahi ya uongozi.
(vii) Uchunguzi ufanywe kuhusu malipo yote kwenye kampuni iliyohifadhi magari toka yatolewe bandarini.

(ix) Uchunguzi ufanywe kuhusu safari zote walizosafiri hawa viongozi kama zilileta manufaa. Wamesafiri sana na pesa nyingi zimetumika. Kuna wakati menejimenti yote ilikwenda China kwa pamoja japo waliondoka kwa vikundi.
(x) Mwisho serikali ichukue hatua mapema kabla kampuni haijaangamia. Sisi tuliopo nje na ndani tunaona na tunajua, na kama kutahitajika msaada tupo tayari kutoa ushirikiano.
 
Watoto na Wajukuu wa Mafisadi-ATCL wazinduka




Wapiganaji, nimepenyezewa taarifa hii na wafanyakazi wa ATCL- Haitii kichefuchefu bali ni kinyefunyefu! Hebu tuijadili!

Sisi wananchi tuliyo ndani na nje ya ATCL tumeona hatuwezi kukaa kimya tukiangalia jinsi kampuni inavyoangamia kwa ufisadi wa kisayansi.

Ufisadi wa kisayansi kwa sababu wanaofanya ufisadi huu ni uongozi wa kampuni kwa kutumia nafasi zao za madaraka na kujifanya huo ndio uongozi.

Tuanze kwa kueleza ni maeneo gani yenye ufisadi halafu tutaje viongozi hao na sifa zao.

Tutataja maeneo yenye ufisadi na matumizi mabaya ya mapato ya kampuni na mikopo toka mabenki mbalimbali. Pia safari zilizo nyingi na za muda mrefu bila kujali gharama na faida za safari hizo.Manunuzi ya magari kwa fedha za mikopo na bila kufuata taratibu. Mwisho ni hila za kuwafukuza ama kuwaondoa katika nafasi nyeti wafanyakazi wa zamani na kuweka wapya ambao huajiriwa kiholela na bila ya sifa zinazolingana na kazi zenyewe au hata na wale waliyoondolewa.

Jopo la viongozi na sifa zao zinazoangamiza kampuni ni:-
1. Mkurugenzi mkuu wa kampuni ni David Mataka.
Yeye aliteuliwa na Rais JK baada ya rais aliyemtangulia kumtimua kwa ufisadi. JK alimuonea huruma DM baada ya kukaa ubaoni kwa muda na pia kushindwa kinyang’anyiro cha ubunge kwa tiketi ya chama tawala. Wananchi wa jimbo lake na wa chama chake hawakumpa kura kwa kuwa alikwisha onekana mbele ya rais BM kuwa ni fisadi wa hali ya juu japo yeye rais BM alikuwa anawakumbatia mafisadi kama Balali.
Mkuu huyu wa kampuni ameanzisha uongozi wa dharura(Management by crisis) ambapo kila asubuhi wakurugenzi na mameneja wateule katika ufisadi hukaa vikao vya kuangamiza kampuni. Amepata Benz ya kisasa katika mgao wa magari yaliyotolewa na wauzaji baada ya kununua magari ya kampuni huko Dubai kwa bei ya juu. Magari hayo ni ya mwaka 1998 japo bei yake ni karibu na mara mbili ya yale yanayouzwa na makampuni mengine ya Dubai. Yeye huwa anasuka jambo halafu anamwachia George, Eliasaph au William walichochee katika kikao cha hao viongozi.

2. MARK MANJI
yeye ni mtu HATARI wa Musoma japo jina lake la kihindi. Huyu ni mshauri wa mkurugenzi mkuu. Alikuwa mkurugenzi wa idara ya operations wakati wa makaburu japo idara hii huwa inaongozwa na marubani. Alipewa cheo hiki na makaburu ili kuwaweka marubani katika himaya ya makundi. Makaburu walipoondoka aliomba kuacha kazi kwa hiari na akastaafu akaomba kuendelea na kazi tena kama mshauri wa mkurugenzi mkuu. Kwa kuwa alikuwa na mapenzi na makaburu na kwa kuwa ameshapata mafao yake, hana huruma na kampuni kwa sasa badala yake yeye ni kichocheo na hujifanya analijua shirika. Anatumia utoto wa mjini kufanya kazi kwani hana shahada hata moja japo amepewa nafasi nyeti.

3. Eliasaph Mathew
aliajiriwa na makaburu kama meneja wa fedha kwa maana hiyo ni mtu wa makaburu. Baada ya mkurugenzi wa fedha aliyekuwa kaburu kuondoka amekaimu nafasi hiyo hadi leo. Huyu ndie kinara wa kupindisha taratibu za matumizi ya fedha na ununuzi. Ni mfuasi namba moja wa DM kwani kwa sasa pesa za kampuni hutolewa kiholela kulipia gharama kwa ufisadi. Mfano kabla ya kufunga mwaka 2007 shillingi millioni mia mbili hamsini zilichotwa kulipa gharama za kutoa magari nane yaliyokuwa katika yadi ya kuweka mgari iliyo ya watu binafsi. Haishi hapo huchota dola elfu tatu taslimu toka kwa mtunza fedha kila mwezi na kumpa huyu mwenye yadi ya kuhifadhi magari. Huidhinisha malipo kwa ankara tu bila kujali taratibu nyingine. Ndiye aliyejumuika katika jopo lililokwenda Dubai kuchagua magari ya kampuni na kuyanunua kwa bei mbaya bila kufuata taratibu za ununuzi. Magari haya ni ya 1998 japo ATCL ni mali ya serikali,hilo halikutiliwa maanani. Yeye amepata zawadi ya VX Landcruiser ya kisasa kama mgao katika hayo manunuzi na sasa ameweka pembeni Vitara yake. Hutumiwa katika mikakati ya kuwaondoa watu wa zamani na wenye sifa kwa kuwazulia kesi na shutuma za matumizi mabaya ya pesa kitu ambacho si kweli.
Waliyoonja joto hilo ni pamoja na Hassani ambaye aliamua kuacha kazi, Hamisi na Mndeme ambao wamesimamishwa kwa suala la bwana Mohamed Makaratasi ambaye ni rafiki wa George Mazula.amebadilishwa cheo baada ya aibu kuikuta atcl

4. George Mazula
yeye eti ndiye rubani kiongozi na mshauri wa DM. Huyu aliwahi kuachishwa kazi wakati mwenyekiti wa bodi alikuwa ni Abasi Sykes. George aliwahi kuunguza injini mbili za Fokker kwa mpigo pale Tanga. Amewahi kuangusha ndege aina ya Fokker hapa Dar es salaam. Amewahi kuua mtu pale uwanja mpya wa JK Nyerere kwa kukatwa na pangaboi baada ya yeye kuzembea kuzima injini. George ni kiungo wa mikakati yote ya ufisadi na kuondolewa watu katika nafasi zao. Alikuwa mfadhili wa DM wakati akiwa ubaoni. Ni rubani mwenye makeke na mikosi mingi. Katika dili ya Dubai yeye amepata Volvo na kujidai amekopa.maskini sasa ni marehemu;walimuingiza kwenye mnyoror wa kifisadi,natumaini aliombamsamaha kwa muumba wake

5. Amin Mziray
Danger zone;huyu ni katibu wa kampuni. Yeye ni chapombe. Alipewa gari ya kampuni na makaburu na kulipindua kwa ulevi. Anayo shahada ya sheria lakini haitumii kwa maslahi ya kampuni. Kampuni imeshindwa kesi nyingi kwa kutokuwa makini huyu mwanasheria. Yumo katika hili jopo la ufisadi wa kampuni. Katika mgao wa magari ya Dubai yeye amepata VX Landcruiser la nguvu. Hayupo tayari kutetea hoja mbovu zinazotolewa ndani ya vikao vya hili jopo la ufisadi.

6. William Haji,
anakaimu nafasi ya mkaguzi mahesabu wa ndani. Aliajiriwa wakati wa makaburu kama mkaguzi wa mahesabu wa ndani chini ya bwana Yakubu. Baada ya muda bwana YAkubu aliwekwa pembeni na huyu bwana kukaimu nafasi yake. Kwa sasa yeye ndiye anayekagua malipo (Pre-audit) hivyo yumo ndani ya mtandao wa ulaji. Ndiye anayetumiwa kutengeneza taarifa za kuzua kesi na uonevu kwa wafanyakazi wa chini. Huchukua nafasi ya afisa usalama wa kampuni ili kupindisha ukweli na hatimaye kuwadhalilisha ama kuwatimua wafanyakazi wasiyo na hatia. Ni hatari sana kwani yupo karibu na DM na Eliasaph katika kila mpango.MASKINI WAMEMPA CHEO CHA ELIACHAFU

7. Sadiki Muze,
Yeye ni mkurugenzi wa idara ya operations kwa sasa. Amepewa nafasi hiyo yeye kwani ndiye aliyekuwa mfadhili mkuu wa DM wakati akiwa ubaoni. Pia ni mshirika wa DM katika vinywaji na mwanachama wa kijiwe kimoja na George. Ni Sadiki na George pekee waliyopewa vyeo na kuenguliwa wengine baada ya DM kuchukuwa uongozi ATCL na ni chapombe. Sadiki na George wamelipwa fadhila.MASKINI AMEONDOLEWA KABISA NA WALA HAWATAKI KUMSIKIA...KILA LA KHERI

8. Heho Mbiru ni Mkenya,
aliajiriwa kwa nguvu enzi za makaburu kama mkurugenzi wa masoko. Aliajiriwa kwa nguvu na aliyekuwa mwenyekiti wa bodi ya ATCL wakati huo Ali Mufuruki kwa kisingizio kuwa hakuna Mtanzania mwenye uwezo wa kushika nafasi hiyo. Ni mzalendo wa Kenya kweli kweli kwani kazi zinazoweza kufanyika hapa (kama Graphics) huzipeleka kwenye kampuni yake. Anayo mapenzi na makaburu hivyo kuleta mabadiliko tunayotaka yeye ni kikwazo na ndiyo maana ni rahisi kutumiwa katika hujuma. Kumbuka tunaushindani na Kenya Airways huyu atatumaliza.AMEONDOKA ZAKE BAADA YA KUIUA ATCL

9. Ajay Gopinath
raia wa India. Aliajiriwa kwa nguvu wakati wa makaburu na aliyekuwa mwenyekiti wa bodi Ali Mufuruki. Ajay aliwahi kufukuzwa nchini lakini kwa sababu zake Ali alifanya juu chini na kumrudisha kama mkurugenzi wa mauzo. Anatumiwa katika upatikanaji wa fedha na kutumika vibaya. Hana sauti ndani ya utawala huu kwani ni mgeni.NAYE KAFUKUZWA

10. Alphonse Mkinga
huyu kinganganizi atoki;ni meneja utumishi. Alistaafu na kuchukua mafao yake baada ya makaburu kutimka. Anafanya kazi kwa mkataba na kuzuia ajira kwa waliomaliza vyuo.
Ameidumaza idara ya utumishi kwa kutoweka muundo wa utumishi na taratibu mbalimbali za ajira. Matokeo yake mkurugenzi mkuu huleta watu wake japo wapo waliofanya usaili. Mfano ni ajira ya mhudumu katika ofisi ya mkurugenzi mkuu,ajira ya afisa majengo na mali ambaye ni jamaa yake. Huyu bwana Peter Gosh anachukua nafasi ya bwana Hassan Kikoko alieandamwa na huu mtandao wa ufisadi na hatimaye kuamua kustaafu mapema. Yupo dereva aliajiriwa kwa hila japo wapo waliofanya usaili na hadi sasa hawajapata ajira. Bwana Mkinga hana sauti kwani yupo kulinda maslahi yake baada ya kupata ajira ya pili.

11. Fidelis Tarimo;
ni mkurugenzi wa uhandisi. Historia yake ni ufisadi mtupu. Aliwahi kusimamishwa kazi na aliyekuwa mwenyekiti wa bodi wakati huo Mzee Abasi Sykes. Tarimo alikwenda kusimamia matengenezo makubwa ya Boeing ya ATC wakati huo (major check) nchini Ireland. Hakuwa anafuatilia gharama halisi za matengenezo na kujali maslahi yake hivyo kusababisha gharama kupanda kwa shilingi bilioni moja na nusu toka ghrama halisi na kulitia shirika hasara na kusimamishwa kazi. Alipata nafasi wakati wa makaburu kwani hakuwa mtetezi wa wazalendo. Kwa sasa wafanyakazi wa idara yake hawamtaki na wameandika barua ya kumkataa na wizara inajua hilo. Ni bingwa wa kuuza ndege za kampuni kwa bei ya kutupwa badala ya ile ya makubaliano ya awali. Ana ukabila na hadi sasa ana jamaa yake anasimamia ujaji wa ndege ya kukodi kwa muda mrefu yuko nje ya nchi. Ni fisadi wa kutupwa kwa ajili ya kutaka pesa za kuendeleza biashara zake.HUYU ANACHOFANYA HAKUNA TOFAUTI NA MAUAJI YA ALBINO,WE ANALETA SPARE NJE YA NCHI AMA TAIRI ZA NDEGE ALAFU UNAKUTA SIZE TOFAUTI NA BADO ANAENDELEA KUKKAA MHH HUYU MATTAKA SIJUI WAMEMLOGA??

12. Rajabu Itambo ni meneja Galileo Tanzania kampuni tanzu ya ATCL. Rajabu alipewa kazi ya ushauri katika kitengo cha Galileo na aliyekuwa meneja wakati huo Maalim Ali. Kaburu mmoja aliyekuwa mkurugenzi wa biashara Mike Bond aliamua kumuondoa Maalim Ali katika nafasi hiyo na kumuweka Rajabu kwa maslahi yake kwani walitaka kuuza Galileo kabla ya kuondoka jambo ambalo hawakufanikiwa. Mpaka sasa Rajabu ana uhasidi na wafanyakazi wa zamani kwani anataka awe mkuu wa kitengo cha ITC (Information and Technology Communication) Ni mmoja wa vibaraka wa DM.
Hadi tunakwenda mitamboni ATCL haina bajeti na hili linatokana na Eliasaph kutayarisha bajeti hiyo kwa usiri mkubwa akiweka vipengele hewa ambavyo bodi ina wasiwasi navyo hivyo kuikataa kila wakati. Bajeti huwa inatengenezwa na kitengo maalum katika idara ya fedha lakini safari hii imekuwa na usiri mkubwa. Ilibidi iwekwe hadharani kwa wafanyakazi kupitia workers council ndiyo iifikie bodi jambo ambalo halikufanyika.
Kama tulivyoeleza awali matumizi mabaya ya pesa yanapeleka kampuni kusikoeleweka. Pesa huchotwa kama za mtu binafsi bila kujali taratibu za kihasibu. Viongozi hawa kwa vikundi huenda safari kila wakati kuliko viongozi wote waliopita. Posho wanayolipana ni kubwa mno kwa kila siku hivyo hata safari za watendaji wa chini huenda wao. Mwenyekiti wa bodi Mustapha Nyang?anyi aliliambia Sunday Citizen tarehe 12 januari 2008 kuwa uzembe wa menejimenti ya ATCL kutoingia mkataba na kampuni iliyokuwa ikodishe ndege kwa ajili ya mahujaji ndiyo chanzo cha sakata zima la hasara katika usafirishaji wa mahujaji. Ukweli ni kuwa menejimenti haikutaka kushirikisha wafanyakazi wa kawaida kuratibu safari hii kama ilvyokuwa miaka iliyopita. Hii ni kwasababu walitaka iwe siri yao kwa kutafuta ndege ya bei poa kuliko hiyo iliyopatikana kitu ambacho hakikuzaa matunda na hatimaye kusema ATCL haiwezi kusafirisha mahujaji. Mbona kabla ya makaburu iliwezekana. Hapa pana ufisadi sio uzembe tuu. Wapo wazoefu wa kazi ndani ya kampuni lakini wamekodi mtu wa nje Mtambalike rafiki yake DM kwenda kusimamia kurejea mahujaji. Tunasema hii ni hujuma na kuwadharau watendaji wa ndani.
Magari ya kampuni yamenunuliwa kwa bei kubwa bila kufuata taratibu na viongozi wanne kupata magari kutokana na gharama hiyo kubwa na bila kufuata utaratibu wa ununuzi. Hivi sasa kampuni ina madeni mengi kutokana na ufisadi.
Wafanyakazi wasiotakiwa hasa wale wa zamani hutafutiwa sababu za kuwaondoa ili ajira wapewe watu wa DM. Mifano hai tumetaja hapo juu na mingine mingi tunayo kama ule wa Said Ibrahimu kufanyiwa visa na Mark Manji hadi kuamua kustaafu ili yeye Manji aongeze muda alipoamua kustaafu kwa kisingizio kuwa hakuna wa kuchukua nafasi yake.

Kwa sababu tumezungumza kwa kifupi tunaomba yafanyike yafuatayo:-

1. Kuleta wakaguzi kama vile Enerst and Young kukagua mahesabu ya ATCL tangu DM awe mkurugenzi mkuu. Hapa panatosha kuona ufisadi katika:-
(i) Mikopo na over draft na kutafuta jinsi pesa hizo zilivyotumika kwa ukamilifu.
(ii) Kupata maelezo kutoka kwa DM kwa nini toka achukue uongozi ATCL hakubadilisha muundo na uongozi wa makaburu tukijua fika viongozi hao wana maslahi na makaburu.
(iii) Uchunguzi juu ya ununuzi wa magari bila kufuata kanuni na taratibu za ununuzi nje ya nchi na kulinganisha bei na makampuni mengine ya Dubai
(iv) Wachunguzwe hawa viongozi wanne walipataje magari hayo toka kwa kampuni iliyouza magari kwa ATCL kwa bei ya juu. Kama ni mikopo waoneshe pesa walipata wapi na utaratibu mzima wa kuyalipia na kuingiza na kuyakomboa.
(v) Zipatikane sababu za viongozi kuomba kustaafu na kujiajiri tena.
(vi) Uchunguzi ufanywe kupata uhalali wa wafanyakazi wa zamani kunyanyaswa na wengine kusimamishwa kazi kwa hila ili kuajiri wengine kwa maslahi ya uongozi.
(vii) Uchunguzi ufanywe kuhusu malipo yote kwenye kampuni iliyohifadhi magari toka yatolewe bandarini.

(ix) Uchunguzi ufanywe kuhusu safari zote walizosafiri hawa viongozi kama zilileta manufaa. Wamesafiri sana na pesa nyingi zimetumika. Kuna wakati menejimenti yote ilikwenda China kwa pamoja japo waliondoka kwa vikundi.
(x) Mwisho serikali ichukue hatua mapema kabla kampuni haijaangamia. Sisi tuliopo nje na ndani tunaona na tunajua, na kama kutahitajika msaada tupo tayari kutoa ushirikiano.
 
ATCL KUSHTAKIWA

Habari zilizoingia hivi punde zinasema wafanyakazi wa kampuni ya ndege ya Precision wanajiandaa kuipeleka menejimenti ta ATCL mahakamani kutokana na kukaidi kulipa pesa za SACCOS ambazo wafanyakazi hao wamekuwa wanachama kwa miaka mingi pamoja na wafanyakazi wa ATCL.

Chanzo cha habari kilichokataa kutajwa jina kilisema kuwa baadhi ya wafanyakazi walikusanyika jana wakiwepo wafanyakazi wa Swissport na BP na kuamua kwa pamoja kuipeleka menejimenti ya ATCL majhakamani ili kuweza kupata haki zao akizungumza kwa jazba mmoja wa wafanyakazi wa SWISSPORT alisema na kunukuliwa " Unajua sisi ni wanachama wa chama kimoja cha kukopa na kulipa kijulikanacho kama wanahewa sasa kila tukienda kwa viongozi wetu wa chama wanatuambia wanaidai ATCL milioni 425 kila tukiomba pesa kidogo tunakataliwa kabisa wakati ni haki yetu" aliendelea kusema kuwa pesa zote wameshikilia menejiment ya ATCL...

Chanzo kinaeleza kuwa juhudi za kumtafuta mkurugenzi wa ATCL Bwana Mattaka ziligonga mwamba kwani ilielezwa kuwa yuko kwenye kikao. Habari zinaeleza zaidi kuwa baadhi ya wafanyakazi wa Swissport na Precision leo hii waliamua kwenda kumuona mkurugenzi na kukosa ushirikiano na kibaya zaidi hata wafanyakazi walikataa kabisa kujibu na kusema kuwa anayejua masuala hayo ya pesa ni Mattaka na menejimenti yake. Kibaya zaidi inaonekana kwenye mishahara ya wafanyakazi hao kuna makato ambayo yanasemekana hayajapelekwa kunako husika. Mfanyakazi mmoja alipoulizwa endapo alitambua kuwa ni kosa la jinai kwa kampuni kukata mshahara wa mfanyakazi bila ya ridhaa yake pasipo kujulishwa . Alisema na kukiri kukiri kuwa hakuna kitu kama hicho na kudai pia hata makato ya PPF hayajapelekwa tangu mwezi wa tano.


Hoja

Hivi PPF mnalijua hili? Na kama ni kweli ilivyosemwa kuna hatua gani zaidi zinafanyika kuhakikisha malipo ya kila mfanyakazi yanawafikia katika muda unaotakiwa?

Iweje kampuni ya MO ENTEPRISES ikae mwezi mmoja bila kulipa wafanyakazi wake ifikishwe mahakamani na kuwaachia viongozi wa ATCL wakicheza na maisha ya watu?

Je hamjui hivi sasa wafanyakazi ikatokea wakaomba kustaafu hamuoni usumbufu utakaojitokeza kwa mfanyakazi aliyeitumikia kampuni kwa takribani miaka 25 atakaoupata?

Je wafanyakazi wanampango gani kuhakikisha pesa zao zinazokatwa zinalipwa sehemu husika?

Serikali kabla ya kuamua kupunguza kazi wafanyakazi wa ATCL ni vema wakapata malimbikizo yao ya posho na marupurupu ambayo menejiment ya ATCL iliamua kuzichukua pesa zao bila taarifa na kushindwa kuzifikisha panapohitajika. Kuliko kuwapunguza na kuanza kuwapa usumbufu wakati wa kudai haki zao.

Kwa hao wafanyakazi wanaojipanga kwenda mahakamani hakikisheni mnapata wakili anayejua sheria za kazi ili aweze kuwasaidia kwani hili halina tofauti na kuwaibia wafanyakazi.

Habari hii Imehakikiwa
 
YA ATCL....

Hatimaye katika kile kinachoonekana na uongozi wa ATCL kulinusuru shirika hilo, wamekuja na hoja ya kuwataka wafanyakazi waende likizo isiyokuwa na malipo. Hata hivyo wafanyakazi kupitia chama chao cha COTWU wamesema mtu anayestahili kuanza likizo hiyo ni mtendaji kwanza ndugu David Mattaka.

Hoja
Hivi wewe unakaa na kuwaambia watu wenye akili zao timamu na familia zao waende likizo isiyokuwa na malipo kwa uzembe ambao hawahusiki, uzembe ambao umesababishwa na tamaa za viongozi wao , uzembe wa kupenda asilimia kumi kwa zabuni zisizo na macho wala miguu, posho ambazo hazina msingi, kujikopesha magari ya shirika huku thamani ya magari hayo haiwiani na ubora wake, kimeo cha airbus. Anza wewe kwanza ..... waache watu wasio na hatia wenye kutegemewa na familia zao wasio kuwa na chanzo chochote cha kipato isipokuwa kibarua hicho.
 
Wafanyakazi waeleza kilichoimaliza ATCL

Na Waandishi Wetu

SIRI zaidi za Shirika la Ndege (ATCL), kufanya vibaya zimezidi kubainika baada ya wafanyakazi kutaja baadhi ya vigogo kwamba hawawezi kukwepa lawama za kufilisika kwa shirika hilo.


Hatua ya wafanyakazi wa ATCL kutoboa siri zaidi za kufilisika kwa shirika hilo imekuja wakati tayari shirika hilo, likiwa limesimamishiwa leseni ya kuruka angani na Shirika la Usafiri wa Anga la Kimataifa (ICAO); na Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini (TCAA).


Kupitia mtandao wa kompyuta, jana wafanyakazi hao wametuma waraka kwa gazeti hili wakieleza matatizo ya ATCL na sababu mbalimbali za shirika hilo kufilisika huku baadhi ya vigogo ndani ya kampuni hiyo, wakitajwa kuhusika.


"Sisi wafanyakazi wa ATCL tunapenda umma utambue kiundani matatizo ya shirika letu. Desemba nane, ATCL ilizuiwa kurusha ndege zake na TCAA kutokana na mambo yasiyo ya kawaida katika leseni ya uendeshaji wa shughuli zake.


Ni aibu ya karne kwa ATCL iliyofanya kazi kwa zaidi ya miaka 30," ulieleza waraka huo.


Kwa ufafanuzi, walisema Mkurugenzi wa Uendeshaji wa shirika hilo pamoja na wakuu mbalimbali hawawezi kukwepa lawama na kuhusika kwao, hali ya sasa ya ATCL inayowagharimu wao na taifa kwa ujumla kwa kuhusika na mikataba ya shirika hilo.


Wafanyakazi katika kuonyesha msisitizo, walisema ukosefu wa uwajibikaji na udhaifu katika utoaji maamuzi ni chanzo kikubwa cha matatizo ya ATCL tangu kuondoka kwa uongozi wa mbia Shirikala Ndege la Afrika Kusini (SAA), pamoja na uingiaji mikataba walioiita ya kifisadi kulifanywa na baadhi ya watendaji wakuu na menejimenti ya shirika hilo.


Kwa kutaja uozo zaidi, walisema ni kulipwa mshahara wa dola za Marekani 10,000 kwa marubani wanne wa kigeni, wakati kimsingi hawana kazi ya kufanya kwa muda mrefu sasa na kwamba pesa hizo zingetosha kulipia mafuzo ya marubani wa kizalendo.


Wamebainisha uonzo mwingine kwamba, ni ule wa kulipia dola za Kimarekani 370,000 kila mwezi kwa ndege iliyokodiwa na shirika hilo, kwa miezi saba bila ndege hiyo kufanya kazi nchini.


Ufafanuzi zaidi wa wafanyakazi hao unaonyesha kwamba, menejimenti ilifanya ufisadi katika ukodishaji wa ndege hiyo aina ya Airbus A320 kwa kuanza kulipia kiasi hicho Novemba 2007 wakati ndege hiyo ilikuwa bado nchini El Salvadore kwa matengenezo.


Ndege hiyo iliwasili nchini Mei Mosi mwaka huu, lakini hata hivyo, haikufanya kazi hadi Mei 30 kutokana na kukosa wataalam wa kuiendesha, hivyo kusababisha zaidi ya dola 2,590,000 za Kimarekani kupotea bure bila ndege hiyo kufanya kazi kwa kipindi cha miezi saba, Novemba 2007 hadi Mei 2008.


Sehemu ya waraka huo imefafanua zaidi kwamba, uongozi wa ATCL ulijua mapema utatumia ndege hiyo ya kukodi kuhudumia abiria wake, lakini haukuchukua hatua za maandalizi kwa wafanyakazi wake ikiwemo mafunzo kwa marubani tayari kufanya kazi katika Airbus A320.


Katika kufafanua zaidi, sehemu ya waraka huo inasema kuwa, tatizo kubwa ndani ya ATCL ni Mkurugenzi na Afisa Mtendaji Mkuu wake kuzungukwa na watu wasiotimiza vema wajibu wao wa kazi, kuwashauri viongozi hao ambao ni wageni katika medani ya usafirishaji wa anga.


Wakati wafanyakazi wakisema hayo, serikali imeonya kwamba, watu wote watakaobainika kulifikisha shirika hilo hapo lilipo watachukuliwa hatua kali za kisheria.


Serikali imefikia uamuzi huo siku tano baada ya Waziri wa Miundombinu, Dk Shukuru Kawambwa, kumpa siku saba Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa ATCL, Balozi Mustapha Nyang'anyi kuwasilisha vielelezo kamili juu suala la shirika hilo.


Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Afisa Habari wa Wizara ya Miundombinu Issah Mbura, alisema kama itabainika kwamba kuna watu walihusika kwa njia moja ama nyingine kuifikisha ATCL hapo ilipo, ni lazima wachukuliwe hatua kali za kisheria.


"Suala hili lilipofika ni pana na ripoti ya Balozi Nyang’anyi imeshaletwa, hivyo chochote kitakachobainika kutoka ndani ya ripoti hiyo kitafanyiwa kazi mara moja," alisema Mbura na kuongeza:


"Ama ikibainika kwamba kuna watu wamechangia kufika hapo ilipo wawe wanafanya kazi hivi sasa ama hawapo kazini, hatua kali itakayochukuliwa dhidi yao iko pale pale," aliongeza.


Kwa msisitizo, alisema ingawa ripoti hiyo bado inafanyiwa kazi serikali pia imeanza kufanya jitihada za kuhakikisha ATCL inaanza kazi haraka iwezekanavyo.


Alifafanua kwamba, moja ya jitihada hizo ni kuhakikisha vifaa vyote muhimu kama vile vipuri na spea zingine za ndege zinapatikana haraka.


"Serikali ilikwishaanza kutatua suala la ATCL hata kabla ya ripoti hiyo kuwasilishwa na moja ya maeneo ambayo tulishafanyia kazi ni suala la vipuri, kumleta mtaalam wa masuala ya mfumo wa usalama wa ndege," alizidi kufafanua Mbura.


"Eneo lingine ni suala la wataalam waliokwenda kufanya ukaguzi katika karakana za ngede ambazo awali zilikuwa zinatumika kutengenezea ndege za ATCL kama vile Nairobi nchini Kenya na Afrika Kusini."


ATCL imekuwa katika misukosuko tangu kipindi cha ndoa yake na lililokuwa Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA), ambayo baada ya kuvunjika, serikali iliamua kuliweka chini ya mikono ya wazalendo likiongozwa na Mkurugenzi Mkuu, Daud Mattaka na Mwenyekiti wa Bodi, Balozi Mustafa Nyang'anyi.
 
Makala
Nakala chapishi
Mtumie mwenzio
Jiandikishe utaarifiwe



Bodi ya ATCL yamkandamiza Balozi Nyang’anyi

Mwandishi Wetu Disemba 26, 2007




Kwa siku 12 Mahujaji wa Tanzania na baadhi ya wengine kutoka nchi jirani, walikwama kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, baada ya taratibu za kuwasafirisha hadi Saudia kukwama. Hatimaye, walisafiri lakini baada ya Serikali kuingilia kati. Sasa jitihada zinafanyika waweze kurejea bila matatizo makubwa. Baada ya sakata hiyo, Serikali iliagiza ipewe taarifa ya hali ya mambo. Raia Mwema imefanikiwa kupata nakala ya taarifa hiyo ya Bodi ya ATCL na inaichapisha kwa faida ya wasomaji.

1.0 UTANGULIZI

Kuanzia Desemba 10 , 2007 hadi Desemba 14, 2007 Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) lilikuwa katika msukosuko mkubwa. Hiyo ilitokana na matatizo ya kukwama kwa Mahujaji kwenda Hijja Saudi Arabia. Tatizo hilo lilianza kama tukio la kawaida la kiutendaji, lakini taratibu lilianza kuchukua sura mpya kiasi cha kuihusisha Serikali wakiwamo viongozi wa juu kabisa wa nchi.

Tatizo hilo kwa kiasi kikubwa limeleta usumbufu usio kifani kwa Mahujaji ikiwamo aibu na fedheha kwa shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), Taifa kwa ujumla, Serikali na viongozi wake wakuu.

Kutokana na hayo, Mheshimiwa Andrew Chenge (Mb), Waziri wa Miundombinu, aliiagiza Bodi kwa kupitia barua yake Kumb. Na. MC 62/2270/01 ya Desemba 17, 2007, kwamba iundwe kamati ya Bodi ya ATCL kufanya uchunguzi juu ya suala la kukwama kwa Mahujaji, na kutoa taarifa yake siku ya Ijumaa, 21 Desemba, 2007.

1.1 UAANDAAJI WA TAARIFA

Kamati ya Bodi katika maandalizi ya taarifa yake ilizingatia yafuatayo:-

Maelezo ya mdomo ya wahusika wakuu wakiwamo wafuatao:-
- Mwenyekiti wa Bodi ya ATCL
- Mkurugenzi Mkuu, ATCL na
- Manager Flight Operations

maelezo yaliyotolewa katika kikao cha dharura cha 14 cha Bodi ya Wakurugenzi cha Desemba 17, 2007

Maelezo ya maandishi ya wahusika muhimu katika suala hili yaliwahusu wafuatao:-
Mwenyekiti wa Bodi – ATCL (Balozi M. Nyang’anyi)
Mkurugenzi Mtendaji - ATCL (D. Mattaka)
Manager, Flight Operations – (M. Manji)
Kaimu Mkurugenzi wa Operations (Capt. S. Muze)
Afisa Masoko - (J. Kagirwa)
Katibu Muhtasi – (M. El-Hady)
Mwanasheria wa Kampuni – (A. Mziray)
Maoni ya Wajumbe wa Bodi ya ATCL
2.0 MAELEZO YA AWALI (BACK GROUND)

Kufuatana na maelezo ya Menejimenti ya ATCL, mnamo mwezi Julai, 2007, Mwenyekiti wa Bodi ya ATCL, aliwaomba viongozi mbalimbali wa Jumuiya za Kiislamu zinazoshughulika na safari za Mahujaji kulipatia shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) biashara ya kusafirisha Mahujaji kwenda Makka na Madina, Saudi Arabia (Lakini Mwenyekiti anasema ni viongozi wa Mahujaji ndio waliomfuata na kumuomba).

Mnamo Julai 19, 2007 Mwenyekiti wa Bodi ya ATCL alimwita ofisini kwake Mkurugenzi wa Uendeshaji, Capt. Sadiki Muze, na kumtambulisha kwa viongozi mbalimbali wa Taasisi za Kiislamu, na kumueleza kwamba mwaka huu ATCL itaandaa safari za Mahujaji. Mkurugenzi huyo alitoa taarifa hiyo kwa Mkurugenzi Mkuu wa ATCL kuhusu maongezi yake na Mwenyekiti wa Bodi. Baada ya majadiliano marefu na wataalamu wahusika kwenye Shirika ilionekana kuwa shirika halina uwezo (ndege) wa kuandaa safari hizo.

2.1 HATUA ZILIZOFUATIA

Mkurugenzi Mkuu aliandika barua kwa Mwenyekiti wa HAJJ Trust, ya Julai 26, 2007, ikimuelezea kuwa ATCL haina uwezo wa kuandaa safari za Hijja. Hata hivyo barua hiyo haikupelekwa kwa walengwa, kwani wakati Katibu Muhtasi anatafuta ofisi za Hajj Trust ili barua iwasilishwe huko, Mwenyekiti wa Bodi aliagiza kuwa barua hiyo isipelekwe mpaka afanye mawasiliano na Menejimenti. Katibu Muhtasi aliwajulisha Mkurugenzi Mtendaji na Mkurugenzi wa Uendeshaji (Capt. Muze) kuwa barua haikupelekwa kutokana na maagizo ya Mwenyekiti wa Bodi.

Mwenyekiti wa Bodi aliwasiliana na Mkurugenzi wa Uendeshaji na kumhakikishia kwamba ATCL ingeliweza kufanya safari hizo, kwani ndege zingeweza kupatikana, hususan kutoka katika kampuni ya RAK Leasing ya Dubai. Pia Mwenyekiti alimpatia Mkurugenzi wa Uendeshaji jina na namba ya simu za mhusika ili awasiliane naye kuhusu upatikanaji wa ndege.

Captain Muze aliwasiliana na kampuni ya RAK Leasing ambao walimwambia kuwa wanayo ndege aina ya Boeing 747-200 yenye uwezo wa kubeba abiria 489, ambayo kwa wakati huo ilikuwa katika matengenezo ya Check “C” na kwamba ingekuwa tayari mwezi wa Septemba, 2007. Capt. Muze aliwaomba wamletee “Documents” za ndege hiyo ili aweze kufanya maandalizi ya kupata vibali muhimu, zikiwemo “slots”. Pia aliwasiliana na kampuni ya Al-Wassam ambao ni “Ground Handling Agent” wa Makka na Madina (ambao hapo zamani walikuwa wana “handle flights” za Hijja za Air Tanzania Corporation) ili wafanye matayarisho muhimu, ikiwamo utafutaji wa “slots”.

Hata hivyo, “documents” za ndege zilichelewa kufika na ilibainika kuwa zilikuwa zinaisha muda wake Novemba 30, 2007, na hivyo zisingefaa kutumika kuombea vibali pamoja na “slots”. Kampuni ya RAK Leasing iliahidi kuwa ingepata “documents” zingine na kuahidi kuitafutia ATCL kampuni nyingine za “ku-handle” ATCL. Pamoja na ahadi hizo kampuni hiyo haikufanya hivyo.

Wakati huo huo Capt. Muze alisafiri kikazi kwa muda mrefu na kumuachia shughuli hii Afisa Masoko, Josephat Kagirwa.

Kadiri muda ulivyopita, na safari za Mahujaji kukaribia ilidhihirika kuwa ndege isingepatikana kutoka kampuni ya RAK Leasing. Hii ilithibitika baada ya wafanyakazi wa ATCL, akiwamo mwanasheria wa ATCL Mziray kwenda Dubai, na kurudi mikono mitupu bila mikataba na au “documents” za ndege ya RAK Leasing na hiyo ilikuwa mwishoni mwa mwezi Novemba, 2007, zikiwa zimebakia siku chache mno kabla ya safari za Mahujaji kuanza.

Baada ya hapo Mwenyekiti wa Bodi na Capt. Muze walianza kufanya mipango mipya ya kutafuta ndege nyingine. Walifanikiwa kupata ndege kupitia msaada wa Al-Wassam, wa Jeddah. Ndege hiyo ni aina ya DC 10 inayomilikiwa na Global Aviation ya Afrika Kusini. Hata hivyo, ndege hiyo ilipatikana kupitia kwa wakala mwingine ambaye ni SAMEK Aviation Services wa Jeddah, (Ground Handling Agent).

Katika mikataba ATCL iliyoingia na SAMEK AVIATION ilijumuisha pia kuipatia ATCL “slots” za ndege hiyo. Mkataba huo ilibidi usainiwe Saudi Arabia na Balozi Hamis Msumi kwa niaba ya ATCL, kutokana na ucheleweshaji wa maandalizi na ufupi wa muda. Wakati haya yanakamilika ilikuwa 6/12/07 na tayari Mahujaji kutoka sehemu mbali mbali walikwisha kuwasili ikizingatiwa kuwa ratiba ya awali ya Mahujaji ingelikuwa 4/12/07.

SAMEK Aviation Services, waliahidi kuwa safari za Hijja zingeanza 8/12/07, na ahadi hii ilithibitishwa kwa Balozi wetu nchini Saudi Arabia, kwamba ndege husika ilikuwa inakuja. Kwa bahati mbaya haikufika kama ilivyoahidiwa, pamoja na ATCL kutimiza masharti yote, ikiwamo kulipa malipo ya awali ya Dola za Kimarekani 550,000.

Kufuatia kutowasili ndege hiyo kama ilivyokuwa imetarajiwa, na Mahujaji kuzidi kusongamana uwanja wa ndege wakati wanasubiri ndege ambayo haikuwa na uhakika, ndipo hali ya wasiwasi na mtafaruku kwa Mahujaji ilitanda na kuanza kuongelewa na vyombo mbalimbali vya habari, hadi Serikali kufahamu kuwa kulikuwa na tatizo.

Kuanzia 9/12/07 Mwenyekiti wa Bodi na Mkurugenzi Mtendaji, ilibidi wahamie uwanja wa ndege ili kuwafariji Mahujaji na kutafuta ufumbuzi kadri hali ilivyokuwa ikijitokeza. Hata hivyo, ndege haikufika kati ya tarehe 9 na 10/12/07 kama ilivyo ahidiwa na SAMEK Aviation Services kwa visingizio mbalimbali. Baadaye iligundulika kuwa sababu za ucheleweshaji wa ndege hii ni kwamba:-

Ndege hiyo ilikuwa inaendelea kufanya kazi nyingine za kusafirisha Mahujaji kutoka Baghdad kwenda Saudi Arabia.
Mawakala waliokodisha ndege hiyo walishindwa kupata “Slots”.
Hatimaye ndege hiyo ilifika nchini 11/12/2007 bila kuwa na “slots” kama ilivyotarajiwa.

3.0 UUZAJI WA TIKETI KWA MAHUJAJI

Mnamo 20/08/07 Capt. Muze kwa niaba ya Menejimenti aliwasiliana na Taasisi ya Waislam, Tanzania, akiwafahamisha upatikanani wa ndege aina ya Boeing 747-200 na nauli ya kiasi cha dola za Marekani 950 ambayo kila abiria angetakiwa kulipa.

Baada ya majadiliano baina ya ATCL na viongozi wa Taasisi ya Waislam Tanzania, mambo yafuatayo yaliendelea kufanyika:-

Alichaguliwa Afisa Masoko ili ku-“coordinate” uuzaji wa tiketi kwa Mahujaji
Viongozi wa Mahujaji walimchagua Wakala FAST TRACK kuwa wakala wao wa usafiri, hivyo fedha zote kwa mauzo ya Dar es Salaam zilipitia FAST TRACK.
Afisa Masoko alipata kibali toka kwa Mkurugenzi wa Masoko, Ajay, kuingiza ratiba ya safari za Mahujaji kwenye mtandao (Reservation System).
Afisa Masoko alipata kibali kingine kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Fedha, Eliasaph, cha kuuza tiketi kwa Mahujaji.
Nauli halisi iliyopokelewa na ATCL ilikuwa ni Dola za kimarekani 870 kwa kila Hujaji na pesa taslimu kwa Mahujaji wote ni Dola za Kimarekani 1,248,013 kiasi ambacho ni baada ya makato yote (commission).
Kuweka ratiba ya Hajj Charters kwenye mtandao (Reservation System) ni kuwezesha safari hizi kuuzwa mahali popote ndani na nje ya nchi, hususan Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Comoro, Malawi na kadhalika.
3.1 MAPUNGUFU YA NAULI

Baada ya kukosekana kwa ndege toka kampuni ya RAK Leasing, ndege ya DC10 ambayo ilisafirisha Mahujaji imegharimu dola za kimarekani, 1,450 kwa kila Hujaji, wakati nauli iliyotozwa na ATCL ilikuwa ni dola za Kimarekani 870 kwa kila Hujaji. Kwa sababu hiyo, ulitokea upungufu wa dola za Kimarekani 580 kwa kila Hujaji. Baada ya majadiliano kati ya Mwenyekiti wa Bodi na Viongozi wa Mahujaji walikubaliana kwamba Mahujaji walipie dola za Marekani 230 kila mmoja na zilizobaki zitafidiwa na ATCL. Hata hivyo, Mahujaji waliahidi kwamba fedha hizo watazilipa watakaporudi kutoka kwenye Hijja.
Imedhihirika kwamba upo utata katika mkataba kati ya SAMEK AVIATION SERVICES na ATCL kuhusu gharama za nauli. Upande wa ATCL imeeleweka kuwa gharama za nauli ni za kwenda na kurudi, japo katika mkataba suala hilo halijawekwa wazi. ATCL kwa ushirikiano na ubalozi wetu nchini Saudi Arabia wanawasiliana ili kuhakikisha swala hili linaeleweka vizuri kabla ya safari za kurudi kuanza.
4.0 SERIKALI KUINGILIA KATI

Baada ya ndege kuwasili 11/12/07, Manager Flight Operations, Mark Manji aliwasiliana na mwakilishi wa SAMEK AVIATION SERVICES kuhusu suala la “Slots” na alihakikishiwa kuwa “slots” zipo. Wakati wanatayarisha utaratibu wa ndege kuondoka Mark Manji vile vile aliwasiliana na kapteni wa ndege ambaye alimjulisha kuwa kila kitu kilikuwa tayari.

Mark Manji aliwajulisha viongozi wenzake wa ATCL kuwa ndege ilikuwa tayari na abiria waruhusiwe kupanda kwa ajili ya safari. Kabla ya hapo muwakilishi wa SAMEK AVIATION SERVICES, alidai na kukabidhiwa fedha kiasi cha dola za Marekani 160,000 kama malipo ya ziada ya safari ya kwanza.

Abiria walipopanda kwenye ndege uongozi wa ATCL uligundua kwamba ndege hiyo haikuwa na kibali “slots” cha kutua Saudi Arabia. Suala hili lilipojitokeza ungozi wa ATCL haukuwa na namna nyingine yeyote ila kuwashusha abiria waliokuwa wamepanda kwenye ndege. Itakumbukwa kwamba tukio hili lilitokea baada ya Rais na Waziri Mkuu pamoja na viongozi wengine wa Serikali kuwaaga Mahujaji ambao tayari walikwisha hakikishiwa kuwa safari ingekuwapo.

Kadri muda ulivyopita ilidhihirika kuwa SAMEK AVIATION SERVICES walikuwa na mikakati ya ubabaishaji kuhusu upatikanaji wa “slots” na hivyo Serikali iliamua kuingilia kati suala hili. Hatimaye “slots” zilipatikana na ndege ya kwanza iliondoka na kundi la kwanza la Mahujai 11/12/2007.

Bahati mbaya kundi la pili halikuweza kuondoka kwa muda uliopangwa kutokana na ndege kuharibika ilipotokea Madina. Hata hivyo, kundi hilo liliondoka 12/12/2007 saa 11.30 jioni badala ya saa 1.30 asubuhi. Kundi la tatu lilisafiri 14/12/2007 mnamo saa 3.30 asubuhi.

5.0 USHIRIKI WA BODI

Bodi ya Wakurugenzi ya ATCL ilipanga kuwa na kikao chake cha 16 cha kawaida kuanzia 9/12/07 huko Bagamoyo. Tarehe 10/12/07 asubuhi baadhi ya wajumbe walipokutana iligundulika kwamba Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji hawakuwapo. Wajumbe walifahamishwa kwamba kulikuwa na tatizo kubwa lililohusu kukwama kwa Mahujaji uwanja wa ndege, hivyo Mwenyekiti wa Bodi pamoja na Menejimenti walikuwa uwanja wa ndege wa Mwl. Nyerere wakishughulikia suala hilo. Wajumbe walifanya kikao cha dharura chini ya uenyekiti wa Balozi (Ami) Mpungwe na kuamua yafuatayo:-

Kuahirishwa kikao cha kawaida cha 16 kutokana na dharura hiyo na hivyo kurudi Dar es Salaam.
Kuagiza Mwenyekiti wa Bodi na Mkurugenzi Mtendaji waitishe kikao cha dharura, siku iliyofuata yaani 11/12/2007 ili Bodi ipewe maelezo juu ya suala hilo, ambalo wajumbe wa Bodi walikuwa hawana taarifa yeyote; na
Wajumbe walikubaliana kwa kuwa suala hili walikuwa hawalijui, wasiliongelee popote, hasa kwenye vyombo vya habari.
Kikao hicho cha dharura hakikuweza kuitishwa kutokana na hali halisi ilivyokuwa, hadi ilipofika 17/12/2007.

6.0 ATHARI ZA KIUTENDAJI KWA ATCL

Kutokana na sakata hili la ATCL na Mahujaji, maneno mengi ya kejeli na kashfa dhidi ya Uongozi wa ATCL yamekuwa yakitolewa na baadhi ya Viongozi wa Mahujaji ambayo yanatia dosari kwa Shirika hili.
Kuanzia 10/12/2007 vyombo vya habari vimekuwa vikitoa maoni na maneno yasemwayo na Mahujaji. Mifano michache ni pamoja na:-
- Katibu wa kundi la Mahujaji la AL-BIZ Abdallah Mohamed alikaririwa akisema “Safari hii imeandaliwa na kundi la kisanii – kisanii …. Tutadai haki na fidia kwa ATC”

- Kiongozi wa Taasisi ya MUSLIM Hajj Trust Juma Nchia alisema “watu waliotenda kosa kubwa wanapaswa kukatwa kichwa kwa mujibu wa Dini yao ……….. tutajadili hukumu yake baada ya safari hii kushidikana kabisa”.

- Katibu wa Taasisi ya Alh-Bir Abdallah Harith Mohamed alisema kuwa “waliingia mkataba na ATC baada ya Nyang’anyi ambaye ni Muislamu mwenzetu na mtu aliyewahi kuwa Balozi wa Saudia Arabia, ambaye aliwaomba Waislam wasafiri na ndege yao….”

Aliendelea kusema “sisi tulikuwa tumeachana na Shirika hili kwa miaka 10 … Taasisi zote ziliambiwa kuwa ATC ina ndege ya kukodi Boeing 747-200 yenye uwezo wa kubeba abiria 480”.
Akalalamika kuwa ATC imewatia hasara kubwa na lazima walipe gharama zote hizi pamoja na fidia ya usumbufu.

- Uzembe huu wa ATC ulitaka kuwasha moto wa hasira ya maandamano kwenye RUN WAY ya ndege ili kuzuia ndege zozote zisiondoke wala kutua uwanjani hapo.

Yote haya yanaashiria kuwa bado Mahujaji kupitia viongozi wao wanatarajia kufanya mamabo yafuatayo:-
Kudai fidia na gharama ya usumbufu.
` (ii) Kuishitaki ATCL kwa kukiuka mkataba.

Kuitaka Serikali kuwachukulia hatua wale wote waliohusika na kuvuruga safari yao ya Hijja.
Serikali kuwaomba radhi Hadharani kwa usumbufu wowote ule uliotokea.
Kuitaka ATCL kupitia Serikali kuwahakikishia kuwa kosa hili halitarudiwa tena wakati wa kuwarejesha nyumbani Mahujaji.
7.0 HATUA ZILIZOCHUKULIWA NA BODI

Katika kikao cha dharura kilichofanyika 10/12/2007 huko Bagamoyo na baadaye kuhitimishwa kwa pamoja 17/12/2007 katika Ofisi za ATCL Dar es Salaam, Wajumbe wa Bodi walimtaka Mwenyekiti na Menejimenti ya ATC itoe maelezo ya kina kuhusiana na sakata lote hili kuanzia mwanzo lilipojitokeza hadi tarehe ya kikao hicho. Pia Bodi ilitakiwa kutoa majibu ya masuala yaliyojitokeza kama barua ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu ilivyokuwa imeelekeza Menejimenti na Bodi kufuatilia kwa undani nini kiliathiri mpango mzima wa safari za Hijja.

7.1 MAELEZO YA MWENYEKITI WA BODI

Bodi ilipata maelezo ya kina toka kwa Mwenyekiti wa Bodi Balozi Mustafa Nyang’anyi na baadaye akayaweka kwenye maandishi.

7.2 MAONI YA BODI

Wajumbe pamoja na kukubaliana na Mwenyekiti kukubali kuwajibika kwa kushawishi Menejimenti kuidhinisha kuingia Mkataba wa ukodishaji wa ndege; Wajumbe waliona kuwa ilikuwa ni kosa kwa kuwaingiza watendaji katika mikataba mizito kama hii, bila Bodi kuhusishwa.

Pamoja na nia nzuri ya Mwenyekiti kutaka kufanikisha safari hii, lakini wasiwasi wa kuwatumia mawakala wa ndege za kukodi bila kutumia taratibu zetu za nchi na Sheria za manunuzi n.k. zinatia dosari utendaji wa Bodi katika kusimamia taratibu hizi.

Ni kutokana na hilo Bodi inaona kuwa Mwenyekiti anastahili kuwajibika na kutoa maelezo hayo kwa chombo cha uteuzi wake ili kusisafisha Bodi na Wajumbe wake ambao hawakuhusika kabisa katika sakata zima la ukiukaji wa taratibu zote za maandalizi ya safari za Hijja.

7.3 MAELEZO YA MKURUGENZI MTENDAJI

Pamoja na maelezo ya kina yaliyojitokeza kama ilivyoainishwa kwenye taarifa yake, kama Mtendaji Mkuu wa Shirika na Mshauri Mkuu wa Bodi, angeweza kukataa ushauri wa Mwenyekiti na kuleta suala hili kwenye Bodi kwa maamuzi. Inaonekana hakufanya hilo na badala yake alikubaliana waendelee na utekelezaji wa ushauri huo kinyume cha sheria, kanuni na maelekezo ya Bodi.

Tatizo hili lilichukua sura mbaya baada ya ATCL kuendelea kuvurugwa na ratiba za ndege hizo za kukodi hata bila Bodi kuwa na taarifa.. Maji yalikuwa yamefika shingoni, hakukuwa na nafasi ya kukwepa mzigo huu.
Mkurugenzi Mtendaji kwa hili, pamoja na barua ya awali ya kutaka kupinga ATCL isijihusishe katika ukodishaji wa ndege za Mahujaji, hawezi kukataa kuwajibika kwa kuwa alikuwa na kila sababu ya kuwajulisha Wajumbe wa Bodi kuhusu mapatano hayo ambayo kiutaratibu yalitakiwa yapate kibali cha Bodi.
Pamoja na uwezo wake mzuri wa kikazi lakini kwa hili anastahili kukiri kosa kwa tabia kama hii.

8.0 MAJUKUMU YA BODI

Kwa mujibu wa majukumu ya Bodi kama yalivyoainishwa kwenye Waraka wenye Kumb. Na. SHC/B.40/6/21 imedhihirika kuwa Menejimenti imesahau na pengine haikufuatilia maelekezo kwenye waraka huo ambao ulifafanua yafuatayo:-

Majukumu ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi
Majukumu ya Wakurugenzi wa Bodi
Majukumu ya Watendaji Wakuu


Imedhihirika kuwa, wajumbe wamesahau na pengine hawakuyafuatilia maelekezo yaliyomo katika waraka huo. Matukio ya hivi karibuni ya SAKATA la ATCL na Mahujaji, yamedhihirisha udhaifu huo kwa kutozingatia maelekezo na utendaji wa kazi za kila siku.

Bado hatujachelewa, hili ni fundisho kubwa kwa Shirika letu la ATCL katika kusimamia maelekezo yale yote yaliyomo kwenye waraka huo.

9.0 MAJUMUISHO

Katika sakata hili, Bodi imebaini kuwa:-

Utaratibu mzima wa kushughulikia suala hili ulikosewa baada ya Mwenyekiti kuanza kujiingiza kwenye utendaji.
Mkurugenzi Mtendaji hakuwajibika ipasavyo baada ya kuandika barua ya kutoridhia maombi ya Mahujaji na kushindwa kuhakikisha kwamba maamuzi yake ya awali ya kukataa yanatekelezwa.
Uongozi wa ATCL haukuwajibika ipasavyo kwa kuliacha suala hili liwe “one man show” badala ya kushughulikiwa na kamati maalum ya Hijja, yaani “Hijja Committee” ambayo ingehusisha idara ya Masoko, Uendeshaji, (Operations) Fedha na Mwanasheria wa Shirika. Kamati hii ingesaidia sana kugundua mapema kasoro za upatikanaji wa ndege “slots” na vibali vingine na kutafuta mipango mbadala ya kuokoa hali hiyo.
Makabidhiano yaliyofanyika kati ya Mkurugenzi wa Uendeshaji na Afisa Masoko hayakuzingatia taratibu za kiutawala. Kazi hii muhimu ilipaswa ikabidhiwe kwa Mkurugenzi Masoko, ambaye angeweza yeye kwa wadhifa wake kutumia maafisa wengine waliochini yao.
Mwenyekiti wa Bodi alikosea kukutana na Mahujaji na kuwaahidi kuwa ATCL itabeba mzigo wa kutoa ruzuku bila kibali cha Bodi ya Wakurugenzi. Jambo hili lina athari ya kifedha na Bodi ndiyo yenye maamuzi ya mwisho juu ya masuala ya fedha na haswa ambayo hayamo kwenye Bajeti ya Shirika.
10.0 MAPENDEKEZO

Bodi inasisitiza kuwa mamlaka yake ya kiutendaji yasiingilie kamwe shughuli za uendeshaji wa Shirika kama ilivyoainishwa katika Waraka wenye Kumb. Na. SHC/B.40/6/21 wa tarehe 28/3/1994.
Vile vile na Menejimenti isijichukulie mamlaka ya kufanya maamuzi kwa niaba ya Bodi.

Kwa vile kuna uwezekano mkubwa wa Shirika kufikishwa kwenye vyombo vya sheria (kushitakiwa) na Mahujaji ni vyema ifanywe mikakati ya kukutana na uongozi wa Mahujaji walioko nchini ili kutafuta muafaka mapema kabla Mahujaji hawajarudi nchini.
Shirika lisijihusishe tena na usafirishaji wa Mahujaji hadi hapo litakapokuwa na uwezo wa kufanya hivyo baada ya kupata idhini ya Bodi ya ATCL na Serikali.
Kutokana na uzito wa suala lenyewe lilivyojitokeza kwa umma wa Tanzania na ulimwengu kwa ujumla Bodi inapendekeza kuwa Mwenyekiti alitolee maelezo bayana kwa umma kwa jinsi alivyohusika.
Kutokana na kutosimamia kikamilifu suala hili Bodi inapendekeza kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL apewe karipio ili iwe fundisho kwake.
Bodi itachukua hatua itakazoona zinafaa kwa kuwawajibisha waliohusika katika Menejimenti.
11.0 MWISHO

Bodi ya ATCL inaishukuru Serikali ambayo ndiye mwenye hisa zote za Shirika hili kwa jinsi walivyoingilia kati.

Shukurani ziende kwa Rais Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu Edward Lowassa, Waziri wa Miundombinu Andrew Chenge, Katibu Mkuu wa Kamati rasmi ya Komandi ya kuokoa ATCL, Dr. Enos Bukuku kwa kazi nzuri sana waliyoifanya kupunguza aibu ambayo ingetupata.

Tunawapongeza na kuwashukuru Viongozi wa dini ya Kiislamu na Mahujaji wote kwa utulivu na uelewa waliouonyesha wakati wote huu wa usumbufu wa safari yao ya Hijja. Tunaiomba Serikali kwa wakati huu ambao Bodi inajaribu kusawazisha athari hizi mbele ya watumishi na mbele ya Umma wote wa Tanzania, iendelee na Kamati yake (Command Post) hadi Mahujaji watakaporejea.

Ni ukweli usiopingika kuwa Bodi nzima imechafuliwa mbele ya uso wa Watanzania; ni kweli pia Mwenyekiti wa Bodi aliwatenga wajumbe wa Bodi kutowahusisha katika maamuzi makubwa kama haya. Ni kweli pia Mkurugenzi Mtendaji alishindwa kumkatalia Mwenyekiti wa Bodi juu ya ATCL kutokuwa na uwezo wa kuingia katika mikataba ya ukodishaji wa ndege kwa ajili ya Mahujaji.

Lakini ni kweli pia katika hali hii wajumbe wamesononeshwa na kitendo hiki cha Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji kwa kutokutoa taarifa yeyote hata sakata lilipoanza hadi lilipotolewa na vyombo vya habari. Ni matarajio yetu kuwa Serikali italifafanua suala hili vizuri ili UKUNGU uliotanda mbele ya uso wa ATCL uondolewe.
 
Balozi Nyang’anyi asema yupo tayari kujiuzulu ATCL

--------------------------------------------------------------------------------

Na Leon Bahati
MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), Balozi Mustafa Nyang’anyi amesema kuwa yupo tayari kujiuzulu iwapo itathibitika kuwa, bodi yake ndiyo chanzo cha ndege zake kuzuiwa kuruka.

Alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na Mwananchi Jumapili kufuatia wafanyakazi wapatao 200 wa ATCL kuazimia kwenye mkutano wao jijini Dar es Salaam juzi kuwa, wataishinikiza bodi na menejimenti kujiuzulu kwa kuwa walishindwa kukabiliana na dosari ndani ya shirika hadi kulazimishwa kusimamisha huduma za safari.

Hasira za wafanyakazi hao zilitokana na hatua iliyochukuliwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Anga (TCAA) ya kuzuia shirika hilo kwa siku kadhaa baada ya kugundua dosari 482 ambazo ni kinyume na kanuni za Umoja wa Mashirika ya Ndege ya Kimataifa (IATA).

“Kama bodi ndio tatizo, hata leo niko tayari kujiuzulu,” alisema Balozi Nyang’anyi ambaye aliwahi kuwa waziri katika serikali ya Awamu ya Pili katika wizara ambayo wakati huo ilikuwa inajulikana kama Mawasiliano na Uchukuzi mwaka 1985 hadi 1989.

Vilevile alisema kuwa, yupo tayari kujiuzulu iwapo watajitokeza watu ambao wakichukua mamlaka ya bodi wataweza kuiendesha ATCL bila matatizo yoyote katika mazingira ambayo shirika lipo kwa sasa.

Alipotakiwa kueleza kiini cha matatizo ya ATCL, Balozi Nyang’anyi alisema kuwa ni uwezo mdogo wa fedha unaoikabili serikali ambao umekwamisha mipango ya kulisuka upya shirika hilo baada ya kuvunja ndoa na shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) mwaka jana.

Alifafanua kuwa baada ya kuvunja ndoa hiyo, shirika hilo lilikuwa na deni la Sh19 bilioni na serikali ikaahidi kuwa itabeba jukumu la kulilipa na hadi hii leo bado halijalipwa.

Kwa mujibu wa Nyang’anyi ahadi hiyo ilitolewa na serikali kupitia Wizara ya Miundombinu Machi 2007 na pia iliahidi kulisaidia shirika hilo mtaji wa kuanzia kutokana na hali mbaya ya kifedha iliyokuwepo baada ya kuachana na SAA.

Katika kutekeleza hilo, alisema serikali iliiagiza bodi kufanya kikao haraka ili kufanya tahmini ya kufufua shirika na kulirejeshea hadhi yake, jambo ambalo walilifanya na kabla ya kufika mwisho wa Aprili 2007, wakawa wamewasilisha mchanganuo ulioonyesha ATC itafufuliwa kwa dola za Marekani 60 milioni sawa na Sh76.2 bilioni, kwa ajili ya kukodisha ndege.

Alifafanua kuwa hadi leo serikali haijalipa deni kama ilivyoahidi na wala haijatekeleza maombi ya fedha hizo kulingana na mchanganuo waliowapeleka na mara kadhaa wamewakumbusha lakini wameambulia patupu.

“Mpaka sasa deni waliloahidi kulipa bado. Mtaji wa dola 60 milioni bado. Sasa katika mazingira kama hayo, unadhani shirika litajiendesha vipi,” alihoji Balozi Nyang’anyi akielezea kuwa suala hilo walishalifanyia kikao na mawaziri wa Fedha na Uchumi na wa Miundombinu ikashindikana.

Baadaye, alisema walimwendea Waziri Mkuu ambaye aliagiza wakutane na Katibu Mkuu Kiongozi, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Uchumi pamoja na Katibu Mkuu Miundombinu, lakini vile vile ikashindikana.

Alipotakiwa kueleza hali ya ATCL wakati wanaipokea kutoka kwa SAA na hali halisi ilivyo ndani ya ATC kwa sasa, Balozi Nyang’anyi alisema yeye amekuwa karibu na shirika hilo kwa muda mrefu na kwamba miaka ya 1980, lilikuwa ni shirika imara lakini walipolipokea kutoka kwa SAA lilikuwa katika hali mbaya.

“Wakati nikiwa namaliza kipindi changu cha uwaziri wa Mawasiliano na Uchukuzi mwaka 1989 nililiacha likiwa linamiliki ndege 13, lakini tulipolipokea Machi 2007 tulilikuta bila ndege hata moja,” alifafanua.

Alibainisha kuwa kwa sasa limeshindwa kununua ndege zake lenyewe kutokana na kutokuwa na fedha na badala yake linajiendesha kwa kukodisha.

Kwa sasa alisema kuwa ATC ina ndege tatu za kukodi, ambazo ili ziweze kuruka mara moja kwa siku inabidi watumie Sh84 milioni wakati fedha za nauli za abiria zinakuwa hazijapatikana kwa kuwa makusanyo hayo hukamilika baada ya wiki mbili kutoka kwa mawakala wanaouza tiketi.

Ucheleweshaji huo, aliuelezea kama moja ya matatizo katika kuendesha shirika hilo lenye mtaji mdogo na lisiloweza kukopeshwa na benki kutokana na kuwa na deni kubwa la fedha.

Kwa sababu hiyo, alisema kuwa hasira za wafanyakazi hao zinatokana na hofu juu ya ajira zao kutokana na shirika kujiendesha katika mazingira magumu, hivyo akawataka wawe na subira kwa sababu mambo yatakuwa mazuri katika siku chache zijazo.

Alisema kuwa bodi inatarajia kukutana wiki ijayo, ambapo pamoja na mambo mengine itaainisha mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na msimamo wao kuhusu hali ilivyo sasa ndani ya shirika.
 
Pichani ni Moja ya gari la Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL) linaloshikiliwa na Benki ya Stanbic Tanzania, likiwa limeegeshwa katika Makao Makuu ya benki hiyo, Dar es Salaam
Benki ya Stanbic Tanzania Limited, Makao Makuu ya Kinondoni, Dar es Salaam, inayashikilia magari sita ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), baada ya kushindwa kulipa deni la Sh bilioni mbili iliyochukua kama mkopo. Fedha hizo zinazodaiwa kushindwa kulipwa kwa miezi miwili sasa zilikopwa na wafanyakazi wa kampuni kwa mikopo na kutokana na kushindwa kuwalipa mishahara watumishi wake, makato ya kila mwezi yameshindikana kukatwa.
Taarifa zilizopatikana kutoka ATCL na katika benki hiyo jana zilithibitisha kushikiliwa kwa magari matano aina ya Toyota Land Cruiser VX, na gari la sita limekamatwa likiwa mjini Moshi, Kilimanjaro na lilipelekwa katika benki hiyo jana na kufanya idadi ya magari hayo kuwa sita.
Waandishi wa habari walitaka habari zaidi kwa undani, lakini uongozi wa benki uliokuwapo haukuwa tayari kuzungumza kwa madai kuwa msemaji wa benki hiyo yupo likizo.
Aidha, inasemekana ndege za ATCL zimefunguliwa mbawa zake kuanza kazi ya kurusha abiria, lakini wafanyakazi wamekosa mshiko wa mwezi mzima wa Disemba.
 
Habari


ATCL yajirusha na ndege moja tu
ATCL kwa maana ya Shirika la Ndege la Bongo hivi sasa lina ndege moja tu kati ya nyingine 12 ilizokuwa nazo enzi zake.

Ndege iliyopo ni B737-200 na hadi sasa ATCL ina wafanyakazi 300. Waziri wa Miundombinu Andrew Chenge alisema hivi sasa shirika hilo linafanya biashara kwa kutumia ndege za kukodi kutoka nchi na mashirika mbalimbali.

Waziri aliteta hayo wakati akizindua bodi mpya ya shirika hilo na kuwapa changamoto ya vimeo hivyo na kuwataka wavibadilishe ili ATCL ianze kupata faida tena.

pumbafu na ndege 4 mnashindwa kuzirusha
 
HEBU SOMA KWANZA HABARI IFUATAYO KISHA TUIJADILI PAMOJA.
Mali za ATCL zakamatwa

Benki ya Stanbic Tanzania Limited, Makao Makuu ya Kinondoni, Dar es Salaam, inayashikilia magari sita ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), baada ya kushindwa kulipa deni la Sh bilioni mbili iliyochukua kama mkopo.



Fedha hizo zinazodaiwa kushindwa kulipwa kwa miezi miwili sasa zilikopwa na wafanyakazi wa kampuni kwa mikopo na kutokana na kushindwa kuwalipa mishahara watumishi wake, makato ya kila mwezi yameshindikana kukatwa.



Taarifa zilizopatikana kutoka ATCL na katika benki hiyo jana zilithibitisha kushikiliwa kwa magari matano aina ya Toyota Land Cruiser VX, kuanzia Jumanne jioni wiki iliyopita na gari la sita limekamatwa likiwa mjini Moshi, Kilimanjaro na lilipelekwa katika benki hiyo jana na kufanya idadi ya magari hayo kuwa sita.



Namba za magari hayo ambazo ‘HabariLeo’ jana ilizipata katika eneo la chini la maegesho yalikohifadhiwa magari hayo japo uongozi wa benki uliokuwapo haukuwa tayari kuzungumza kwa madai kuwa msemaji yupo likizo, ni SU 37079, SU 37081, SU 37082, SU 37086, SU 37083 na lililofikishwa jana ni SU 37084.



Habari zaidi kutoka eneo la benki yalikohifadhiwa magari hayo zilieleza jana kuwa yataendelea kushikiliwa mpaka deni hilo lililipwe na uamuzi huo ulifikiwa baada ya hofu kuwa huenda kampuni hiyo ikafa na hivyo benki hiyo ikakosa kila kitu.



Gazeti hili lilifika makao makuu ya Stanbic makutano ya barabara za Ali Hassan Mwinyi na Kinondoni, na mhudumu wa mapokezi alieleza kuwa wasemaji waliokuwapo hawakuwa tayari kulizungumzia, na mwenye dhamana ya kutoa taarifa hiyo ni Mkurugenzi Mkuu, Bashir Awale, yuko likizo.



Hata hivyo, taarifa za ndani ya benki hiyo zililieleza gazeti hili kuwa deni wanaloidai ATCL ni Sh bilioni mbili kwa mwezi huu na kwamba uamuzi wa haraka ulichukuliwa baada ya akaunti ya kampuni hiyo kwa benki hiyo kuonyesha haina fedha za kulipa deni hilo wala haitarajii kuwa nazo kwa siku za karibuni.



Chanzo chetu cha habari ndani ya ATCL kilieleza kuwa magari hayo yalikamatwa tangu wiki iliyopita isipokuwa la Mkurugenzi Mtendaji ATCL, David Mattaka. Hata hivyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya ATCL, Balozi Mustafa Nyang’anyi, alithibitisha jana kupata taarifa ya kukamatwa kwa magari hayo na ameitisha kikao cha dharura kitakachokaa leo makao makuu ya kampuni hiyo.



Alisema pamoja na suala hilo, pia watajadili mambo mengine likiwamo la kurejeshewa leseni ya kurusha ndege waliyonyang’anywa na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Desemba 8, mwaka huu.



ATCL ilinyan’ganywa leseni hiyo baada ya kubainika kuwa na dosari za kiufundi zinazosababisha kutokuwa na viwango stahili vya kiusalama vya kuwaruhusu kurusha ndege; ukaguzi uliowataka warekebishe dosari hizo ulifanywa Oktoba mwaka jana na leseni hiyo iliisha kazi tangu Aprili mwaka huu, lakini walikuwa wakiongezewa muda mpaka iliposhindikana wakanyang’anywa leseni hiyo.



“Hilo jambo na mimi nimepewa taarifa, lakini kusema ni kiasi gani au ni deni linahusu nini, mimi siyo menejimenti, mpigie Mattaka, ila ninachoweza kusema ni kwamba deni hilo si kitu cha ajabu maana tulikabidhiwa kampuni na deni la shilingi bilioni kumi na tisa,” alisema Balozi Nyang’anyi na kuongeza: “Ufafanuzi zaidi sina.



Mnashangaa hilo, kuna na la BP, pia waliokuwa wanatusambazia chakula kwenye ndege… na mengine mengi, yote hayo tutayajadili kesho katika kikao cha dharura na menejimenti nilichokiitisha, tutazungumza hayo na mengine mengi.”



Alisema katika kikao hicho pia watazungumzia mishahara ya wafanyakazi ambayo mpaka jana walikuwa hawajapata na pia kupanga namna ya kurudi tena katika uzalishaji mara watakaporejeshewa leseni ya kurusha ndege tena.



Mattaka alipoulizwa jana kuhusu kushikiliwa kwa magari, alikanusha kwa kudai taarifa hizo si za kweli, lakini alikiri kuwapo kwa kikao cha Bodi na Menejimenti alichokiita kuwa ni kikao cha kawaida si cha dharura. “Hizo habari umetoa wapi? Si kweli, nasema si kweli?” alisema huku mwandishi akiendelea kumhoji.



“Kuhusu kikao ni kweli kipo, lakini si cha dharura, ni cha kawaida……naomba unitafute kesho baada ya kikao kuhusu hilo unalotaka kujua,” alisema Mattaka. Hivi sasa TCAA inaendelea kupitia nyaraka za ATCL na kuna taarifa kuwa leo w.anaenda kukagua namna ya wafanyakazi wa kitengo cha dharura ndani ya ndege wanavyoweza kuchukua hatua pindi tatizo linapotokea.

CHANZO: Habari Leo


NI DHAHIRI KWAMBA UONGOZI WA SASA WA ATCL HAUWEZI KULIREJESHA SHIRIKA HILO KATIKA UHAI WAKE.KINACHOSHANGAZA NI KWANINI HADI LEO HAWAJAWAJIBISHWA.LAST WEEK ZILITOLEWA SIKU 7 ZA KUTOA MAELEZO.BINAFSI SIDHANI HATA KAMA KULIKUWA NA HAJA YA KUFANYA HIVYO KWA SABABU YEYOTE ATAKAYEPEWA NAFASI YA KUELEZEA UDHAIFU WAKE ATAJITETEA KWA VISINGIZIO LUKUKI.TATIZO HAPA SIO KWAMBA KUJITETEA NI KITU KIBAYA BALI UKWELI KUWA WAKATI SIKU 7 ZINATOLEWA (NA SI AJABU ZIKAONGEZWA) ATCL INAZIDI KUJIWEKA KATIKA HALI MBAYA YA KUREJEA TENA KATIKA OPERESHENI ZAKE.IKUMBUKWE KUWA CHANZO PEKEE CHA MAPATO KWA ATCL (NA SABABU YA KUANZISHWA KWAKE) NI BIASHARA YA USAFIRI WA ANGA.SIKU ZINAZIDI KUKATIKA TANGU SHIRIKA HILO LIPIGWE FULL STOP KUSAFIRISHA ABIRIA,NA HIYO INAMAANISHA KWAMBA ATCL INATENGENEZA HASARA KILA SIKU KWA VILE WAKATI HAKUNA MAPATO YANAYOINGIA,MATUMIZI LAZIMA YAFANYIKE KATIKA KILA SIKU YA UHAI WA SHIRIKA HILO.


HIVI HAKUNA WATU WENGINE WANAOWEZA KUTEULIWA KWENYE NYADHIFA ZA UENYEKITI WA BODI YA ATCL NA MKURUGENZI MKUU BADALA YA NYANG'ANYI NA MATTAKA,RESPECTIVELY?JE HAWA NDIO WATU PEKEE WANAOWEZA KUIOKOA ATCL?KUNA USHAHIDI WOWOTE WA WANANCHI HAWA KUWA NA UWEZO HUO?JE KUSUASUA KWA ATCL HAKUNA MAHUSIANO NA MAPUNGUFU KATIKA UWEZO WAO WA KUONGOZA SHIRIKA HILO?


NA BWANA MATAAKA AMEZUA TABIA MBAYA YA KUKANUSHA KILA TAARIFA ZISIZOPENDEZA ZINAZOELEKEZWA KWA ATCL.LAST TIME,ALIKANUSHA TAARIFA KWAMBA MAMLAKA YA MAWASILIANO IMEZUIA SHIRKA HILO KURUSHA NDEGE ZAKE,LAKINI BAADAYE AKALAMBA MATAPISHI YAKE NA KUKIRI HABARI HIYO.SASA TENA ANAKANUSHA HABARI YA KUKAMATWA KWA MAGARI HAYO WAKATI GAZETI HUSIKA LIMESHUHUDIA MAGARI HAYO YAKIWA KWENYE YADI YA BENKI YA STANBIC.AU MATTAKA ANATAKA KUTUAMINISHA KWAMBA PARKING YA MAGARI YA ATCL SASA NI HAPO STANBIC?


HIVI HII SERA YA KULINDANA ITAENDELEA MPAKA LINI?VIONGOZI WETU HAWAJISKII UCHUNGU WANAPOONA WENZETU WA KENYA AU ETHIOPIA,KWA MFANO,WANAVYOPASUA ANGA NA MASHIRIKA YAO YA NDEGE YENYE HADHI YA KIMATAIFA?KWA KWELI INATIA UCHUNGU NA KUUDHI HASA UNAPOONA VIONGOZI WA SHIRIKA LILILOKO A.C.U WAKISHINDWA KUONYESHA UCHUNGU KWA MATATIZO YALIYOPO HADI KUDIRIKI KUONYESHA KUWA "na kuna deni la BP...madeni ni jambo la kawaida".HIVI WAUNGWANA HAWA WANAWEZA KUTUELEZA WANAFANYA NINI HASA KUIKWAMUA ATCL?NA KAMA UTETEZI WAO PEKEE NI KUTOPEWA FEDHA NA SERIKALI,KWANINI BASI WASIACHIE NGAZI KUONYESHA KUTORIDHISHWA KWAO?KUNA MASLAHI WANAYOPATA VINGENEVYO WANGESHAJIUZULU ILI LAWAMA ZISIWAANGUKIE WAO PINDI ATCL IKIFA.
 
Saturday, December 20, 2008
RAIS KIKWETE AWASHUTUMU WATENDAJI ATCL KWA UZEMBE
WAKATI Rais Jakaya Kikwete amesema kuwa kufungiwa kwa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), kumetokana na uzembe wa watendaji wa shirika hilo, Waziri wa Miundombinu, Shukuru Kawambwa ameipa bodi ya shirika hilo siku saba kueleza chanzo cha kudorora kwake. ATCL imefungiwa kurusha ndege zake ndani na nje ya nchi baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Anga (TCAA), kuipokonya cheti cha usalama wa anga (AOB) kutokana na uzembe katika kujaza nyaraka za usalama wa anga kulingana na sheria za mamlaka hiyo.
Hatua ya TCAA ilifuatiwa na uamuzi wa Umoja wa Mashirika ya Ndege Duniani (IATA) kuizuia kufanya shughuli zozote za biashara ya usafiri wa anga.
Kikwete, ambaye yuko nchini Msumbiji kwa ziara ya siku tatu ya kikazi, alisema katika utaratibu wa kawaida shirika hilo na mengine hufanyiwa ukaguzi na TCAA na kwamba, katika kipindi hicho ATCL ilipewa notisi ya miezi mitatu na muda wa ziada kuwasilisha nyaraka zake kwa ukaguzi.
Lakini akaongeza kuwa pamoja na kuongezewa muda, shirika hilo lilishindwa kufanya hivyo na badala yake ATCL ikawasilisha TCAA nyaraka zenye mapungufu na kusababisha kufungiwa.
Rais Kikwete aliyekaririwa na kituo cha televisheni cha TBC1 kutoka Msumbiji juzi usiku na jana, amemtaka Waziri wa Miundombinu kukutana na bodi ya ATCL haraka, kuhakikisha bodi hiyo na menejimenti inatoa maelezo kuhusu uzembe huo pamoja na kuchukua hatua kuiwezesha ATCL kuanza kazi ndani ya siku 10.
Kwa mujibu wa TBC1, sambamba na hatua hiyo, serikali pia ipo mbioni kuiongezea mtaji ATCL kwa lengo la kuiwezesha kuboresha huduma zake na kujiendesha kibiashara.
Katika miezi ya karibuni ATCL imekumbwa na wimbi la matatizo mbalimbali, ikiwemo hali mbaya kifedha iliyosababisha wafanyakazi wake kulipwa kwa mafungu mshahara wao wa mwezi Novemba.
Hata hivyo, bodi ya ATCL imesisitiza kuwa serikali isipolipa deni la Sh20 bilioni na kuongeza mtaji wa Sh70 bilioni, itakuwa ndoto kufanikisha mipango ya kuliunda upya shirika hilo, anaripoti Leon Bahati.
Mwenyekiti wa bodi hiyo, Balozi Mustapha Nyang’anyi alisema dawa ya ATCL ni kulipa deni hilo na kuongeza mtaji kwa dola 67 milioni za Kimarekani.
Alikanusha madai kuwa kuyumba kwa ATCL kumetokana na uzembe wa watendaji, akisema tatizo kuu ni serikali kutotekeleza ahadi za kulifufua shirika mara baada ya kuvunja mkataba na Shirika la Ndege la Afrika Kusini (SAA) Machi, 2007.
“Hata tukirudishiwa leseni bado hatuwezi kutatua matatizo hayo. Kama serikali ingelipa deni, angalau tungeweza kukopa benki. Lakini katika mazingira ya deni hili hatuwezi kukopeshwa,” alisema waziri huyo wa zamani wa mawasiliano na uchukuzi.
“Udhaifu wote unaoonekana sasa tuliuona tangu awali na ndio maana tuliiambia serikali watupe fedha hizo za kulisuka upya shirika. Uzuri, wao (serikali) ndio waliotuomba tufanye tathmini na Aprili 30 mwaka 2007 tukaikabidhi Wizara ya Miundombinu mpango wa biashara wa miaka mitano pamoja na kiwango cha fedha kinachohitajika. Hadi leo hatujapewa chochote,” alilalamika Balozi Nyang’anyi.
Katika hatua nyingine, serikali imempa siku saba mwenyekiti wa bodi ya ATCL kutoa maelezo ya kina yaliyosababisha shirika hilo kupoteza mwelekeo na kusimamishiwa leseni ya kuruka angani- siku zinazoisha Desemba 22, anaripoti Peter Edson.
Serikali pia imesema ili ATCL iweze kurudishiwa leseni yake na kuanza kufanya kazi kama ilivyokuwa mwanzo ikizingatia taratibu zote za Mamlaka ya anga duniani, inahitaji kiasi cha Dola 273 milioni za Kimarekani.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam jana, Waziri wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa alisema serikali imesikitishwa sana na kitendo cha ATCL kusimamishiwa leseni, akisema suala hilo linaathiri uchumi wa nchi.
“Hatuwezi kuoneana aibu mambo ya nchi yanapoharibika, tumempa mwenyekiti wa bodi siku saba kutoa maelezo ya kina, ili waliohusika kuliangamiza shirika waweze kuwajibishwa,” alisema Dk. Kawambwa.
Alisema fedha ambazo zinatakiwa ili kuirudisha ATCL katika shughuli zake za kawaida ni nyingi, ikizingatiwa kuwa hazikuwa kwenye bajeti yoyote ile.
Alisema serikali kwa kushirikiana na bodi ya wakurugenzi tayari imeshazipata fedha hizo na tayari juhudi za kupitia upya kanuni na sheria za uendeshaji wa ndege zimeanza kufanyika ili kulinusuru shirika hilo.
Dk. Kawambwa alisema utekelezaji wa mpango huo wa kuboresha shughuli za shirika, kwa lengo la kukidhi kanuni na sheria stahili za mamlaka ya anga ulishaanza tangu Desemba 11 na unategemewa kuisha Desemba 24 wakati ndege za ATCL zitakaporejea angani.
Aliongeza kuwa mkurugenzi huyo akishapeleka maelezo ya kina kuhusu sakata hilo, watendaji wote watakaobainika kuwa kwa namna moja au nyingine walihusika kulihujumu shirika hilo watawajibishwa kwa kanuni na sheria.
“Katika jambo hili hatuna masihara hata kidogo, tutahakikisha tunapata ufafanuzi wa kutosha na kuchukua hatua kwa masilahi ya taifa,” alisema Dk. Kawambwa
Alisema haitawezekana watu wachache kuharibu kazi na uchumi wa taifa wakati serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi kwa ajili ya kuliboresha shirika hilo ili liweze kumudu shughuli zake.
Alisema kusimamishwa kwa ATCL kuruka angani ni changamoto kwa nchi, kwani athari zake ni kubwa kutokana na ukweli kuwa litakuwa haliingizi fedha yoyote.
“Watumishi wa ATCL wataendelea kudai mishahara yao kwa mujibu wa taratibu, lakini shirika halizalishi, fedha za mishahara zitatoka wapi?” Dk. Kawambwa alihoji.
Alisema pamoja na changamoto hiyo, bodi ya wakurugenzi pamoja na shirika hilo wanawajibika kutafuta fedha za mishahara ya wafanyakazi wao katika kipindi hiki ambacho huduma zimesitishwa.
“Tumewaeleza kuwa serikali haitapenda kusikia wafanyakazi wanakosa mishahara “
Alisema nia ya serikali ni kuhakikisha kuwa ATCL inarudia kazi zake mapema iwezekanavyo na kwa ufanisi, ikiwa ni pamoja na kuleta maendeleo ya taifa badala ya kuwanufaisha watu wachache.
Hatua ya TCAA kuipokonya cheti cha usalama wa anga ilichukuliwa baada ya Kitengo cha Ukaguzi cha Umoja wa Mashirika ya Ndege Duniani (IOSA) kulikagua shirika hilo mwaka jana na kubaini mapungufu 482, lakini ATCL haikurekebisha makosa hayo.
Novemba mwaka huu, Mamlaka ya Kimataifa ya Usafiri wa Anga (ICAO) iliikagua TCAA na kubaini kuwa nyaraka zilizojazwa na ATCL zilikuwa haziendani na sheria za mamlaka hiyo ya Tanzania na hivyo kuishauri iipokonye cheti hicho cha usafiri wa anga.
Tayari ATCL imeshasema kuwa imerekebisha mapungufu hayo na kuziwasilisha nyaraka hizo TCAA, ambayo iliahidi kuzishughulikia katika muda wa siku 10 za kikazi.
Mwandishi wetu, Salim Said anaripoti kuwa baadhi ya Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, ambazo ni kati ya waathirika wa matatizo ya usafiri ya ATCL, zimepongeza uamuzi wa IATA wa kulifungia shirika hilo la ndege.
Wakizungumza na Mwananchi kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam jana, makatibu Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) na Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu wamesema hatua hiyo ni stahili ya ATCL na wala si uonevu.
Katibu mkuu wa Bakwata, Sheikh Ally Juma Mzee alisema kutokana na utendaji mbovu wa ATCL, Waislamu 1,500 walipata usumbufu wa kulala Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere kwa zaidi ya siku 11 mwaka jana wakati wakielekea Maka kwenye ibada ya Hija.
Licha ya Usumbufu huo lakini Waislamu/mahujaji hao hawakulipwa fidia pamoja na serikali kuwaahidi kifuta jasho, jambo lililozipelekea baadhi ya Taasisi za Kiislamu kuingilia kati na kuahidi kuwa wataliburuza mahakamani shirika hilo.
“Waislamu nchini ndio waathirika wakuu wa uzembe wa viongozi wa ATCL, hatua ya kuifungia si uonevu bali ni stahili yao kutokana na uzembe unaofanywa na uongozi wa shirika hilo,” alisema Sheikh Mzee.
“Hili ni fundisho kwanza kwa uongozi wa ATCL na ni aibu kwa shirika linaloongozwa na wasomi na watu ambao walishashika nafasi kubwa serikalini kufanya uzembe wa hali ya juu katika utendaji wao,” alisema.
Naye katibu mkuu wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislaam Tanzania, Sheikh Ramadhan Sanze alisema hatua hiyo ni sahihi na kulaumu kuwa imechelewa kwa kuwa ilistahili kuchukuliwa tangu mwaka jana wakati shirika hilo lilipokwamisha safari za mahujaji.
“Hii ilikuwa ichukuliwe tangu mwaka jana imechelewa sana, lakini tatizo si ATCL bali tatizo ni viongozi wake ambao ni wazembe na hawana historia nzuri ya utendaji katika sehemu zote wanazoongoza,” alisema Sheikh Sanze.
Sheikh Sanze alisema mwenyekiti wa bodi ya ATCL, Mustapha Nyang’anyi ana kashfa ya kununua kivuko kibovu cha Kigamboni katika miaka ya tisini wakati huo akiwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi.
 
It is indeed shameful. Yaani pamoja na mlolongo wote huu wa vimbwanga viongozi wa ATCL bado wanaachiwa waiue kabisa
 
ATCL haiko kwenye priorities za Serikali japo kwenye ilani ya uchaguzi ilielezwa kuwa ATCL itaimarishwa.

It is very sad kuona resources zilizopo pale ATCL zinaangamia, ni heri serikali baada ya kuona haina mpango wowote wa maana kwa ATCL ingeliwaachia wafanyakazi waliendeshe kwani nina hakika within wafanyakazi wangeliweza kuliendesha hilo shirika tena kwa ufanisi mkubwa. Lakini ndiyo hivyo tena maamuzi ya minority ndiyo factor kubwa inayotukwamisha kufikia maendeleo ya kweli.

What I see, ATCL workers will suffer kupata mafao yao / haki zao na watahangaishwa kama wanavyohangaika wastaafu wa EAC.

Ninawashauri wafanyakazi waendelee kutafakari nini kifanyike sasa.
 
Just for your info;nyie mnaotarajia kustaafu kwenye hiyo kakampuni chenu viongozi wameandika msaafu wa kubadilisha maslahi yoote mliokuwa mnatakiwa kupata;;na draft iko nyuma ya jf;
watchout
 
Back
Top Bottom