V. Putin sworn in as a Russian president in capital city Moscow

Unajua hii model ya kukabidhiana walitaka kuitumia JK na EL wakati huo, bahati mbaya/nzuri wakakosea taratibu

hawa waliyataka wenyewe wangekuwa wanapiga kazi inayoeleweka bila shaka wangeweza ila wanaiba wanatorosha wanyama , umeme hakuna maisha magumu ,migomo ,ajira hakuna , basi taifa linaenda enda tu ....hawa wenzao kila kitu kipo shwari na nchi yao wanailinda sana vilivyo. kwa nini wananchi wasijisahau na kuwaacha waendelee
 
medvedev-putin_2035769i.jpg

hawa jamaa ni school mate wote walisoma st petersburg ...
 
Unajua hii model ya kukabidhiana walitaka kuitumia JK na EL wakati huo, bahati mbaya/nzuri wakakosea taratibu

hawa ufisadi uliwazidi na tamaa wakataka mpaka waione Tanzania inakuwa bankrupt kabisa
Wasingeweza hawa kwa tamaa walizokuwa nazo
Waone jamaa wanavyoelewana Putin na Medvedev hata kama kuna jingine la chini chini ila halionekani kabisa
 
Hivi wakuu, zile vurugu za waandamanaji wakati wa kuapishwa Putin zimekaaje, tunaweza kuzihusisha na hujuma dhidi y Putin kutoka nchi za nje ?

hayo maandamano yapo sana si uliona hata wakati wa uchaguzi walivyokuwa wanaandamana
Ila naona CNN na ABS na wenzake hawayapi kipaumbele sana
Kwa sasa mitambo yao imeelekezwa Syria na Egpty na Libya zaidi kuangalia kinachoeendelea
Na wanaona maslahi ya USA kule sio sana akiwepo huyu jamaa hapo juu na waziri wake mkuu
 
kuna maandamano bado huko moscow sema hayapewi coverage kabisa.

Mi nadhani mpaka ujue kuna maandamano Russia ni kuwa imepewa coverage ya kutosha.
Vyombo vya habari vya Europe na US vinajitahidi kupopularize kila activity inayoleta bad image on Kremlin.
Hata watu kumi wakiandamana Moscow CNN, ABC zitaonyesha.
Haya maandamano bila shaka yanakuwa sponsored na US and alies.
 
401626_10150910910311181_357990416180_12416988_1974681526_n.jpg

564991_423944817624292_207845345900908_1538974_1248833222_n.jpg

149384_423944844290956_207845345900908_1538976_2100241275_n.jpg

528852_423945017624272_207845345900908_1538987_1181753956_n.jpg


May 8, 2012
Moscow Riot Police detaininig participant of an unsanctioned peace campaign protesting Vladimir Putin's return to Presidency.
Photo: Vladimir Astapkovich, RIA Novosti
source:https://www.facebook.com/RiaNovosti
Kumbe kuna maandamano ila ya kimya kimay huko kumpinga jamaa
 
Saint [QUOTE said:
Ivuga;3878116]
401626_10150910910311181_357990416180_12416988_1974681526_n.jpg



528852_423945017624272_207845345900908_1538987_1181753956_n.jpg


May 8, 2012
Moscow Riot Police detaininig participant of an unsanctioned peace campaign protesting Vladimir Putin's return to Presidency.
Photo: Vladimir Astapkovich, RIA Novosti
source:https://www.facebook.com/RiaNovosti
Kumbe kuna maandamano ila ya kimya kimay huko kumpinga jamaa

[/QUOTE]

These guys look like soldiers...hakuna kutoa ushuzi baada ya kuzidiwa nguvu ukibeba mtu kama hao jamaa
 
This are sort of guys wanaojua kulinganisha shabaha za maendeleo na hali halisi ya nchi zao sio ku copy model za nchi nyingine ambazo hawafanani na hali halisi za nchi zao, i liked when he said, we dont have to follow western way of democracy to be democratic!
 
Mi nadhani mpaka ujue kuna maandamano Russia ni kuwa imepewa coverage ya kutosha.
Vyombo vya habari vya Europe na US vinajitahidi kupopularize kila activity inayoleta bad image on Kremlin.
Hata watu kumi wakiandamana Moscow CNN, ABC zitaonyesha.
Haya maandamano bila shaka yanakuwa sponsored na US and alies.

Ni kweli mkuu, Putin aliwahi kuionya Merikani kwamba inatumia mgongo wa NGOs kutaka kuleta vurugu nchini mwake - akaongezea kwamba Merikani wasifikili tawi la usalama la URUSI limekwenda likizo! Huyu jamaa ndiye mwenye uwezo mkubwa wa kufufua uchumi wa Urusi kwa kutumia kikamilifu rasili mali ya taifa hilo kubwa duniani, vile vile ameahidi kutoa fedha za kutosha kuliweka jeshi la nchi hiyo likiwa na zana za kisasa kabisa za VITA hili wakabiliane na NJAMA za NATO zakutaka kuizingira Urusi kwa kisigizio cha Kujiami dhidi ya nchi korofiki, kumbe mwezao alisha wasoma muda mrefu kwa kufanikisha kutengeneza silaha za kukabiliana vilivyo na air defence sheild za NATO, baada ya majaribio ya silaha hizo Putin aliwambia NATO wazi wazi kwamba kwa sasa hivi hakuna air defence system yoyote duniani ambayo inaweza kukabiliana na makombora hayo ya Urusi.

Putin ni moto wa kuotea mbali, naona alipata mafunzo balabala alipo kuwa afisa wa KGB, wakina mama wanapenda sana kumtania eti unatembea unarusha rusha mikono kama BATA.

Siku hizi media za magharibi zimepata mshindani wa hali ya juu kutoka media za KICHINA zifuatazo: CNC (Beijin) na CCTV(Shanghai)-kwa lugha ya Kingereza, Kifaransa,Kichina nk) na imefungua matawi Merikani na Africa (Nairobi) na wana wawakirishi karibu Dunia nzima; picha sauti na rangi vinaonekana vizuri sana. Mataifa ya magharibi yatapata wakati mgumu sasa, itakua sirahisi kuidanganya Dunia tena.
 
Kama Russia ingepata president mwingine baada ya Boris Yeltsin anayefanana kifikra na Boris Russia kwa sasa ingekuwa under the armpits za US.
Yeltsin's Russia adopted mainly western ideas, and were on the right path to its autodestruction of its communist integrity
 
Putin na Medvedev wanatisha,'wanarotate' tu...

jamaa wakoloni kweli lakini putin kaipata pata..for first time since he got into power this time elections watu wengi wameandamana kupinga yeye kua Rais tena...hivi vitu zamani ulikua huvioni..so am sure na wao wamechakachua kura...but bora karudi coz hata wakati yeye ni prime minister bado all the big decisions alikua anafanya yeye...yule medvedev alikua kawekwa pale kuzugia tu
 
halaf wote ex-KGB

Putin alikuwa na cheo cha Kanali, na anajua kuzungumza Kijerumani fluently, kuendesha ndege za kivita mchezo wa karate-lakini Ma-ex KGB wote wanajuha mchezo huu, Ma-ex-KGB wajanja sana Putin anaweza kuwa anajua hata kuzungumza Kingereza lakini akajifanya hajuhi, mbinu hizi na Wachina wanazitumia sana!
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom