Mzalendo80
JF-Expert Member
- Oct 30, 2010
- 2,508
- 1,338
Nyerere: wafungwa wafundishe Sekondari za kata | Send to a friend |
Monday, 27 June 2011 08:53 |
0diggsdigg Hussein Issa KUTOKANA na uhaba wa walimu nchini, serikali imeshauriwa kuwatumia walimu waliopo magerezani kufundisha shule mbalimbali hususan za kata, ikiwa ni sehemu mojawapo ya adhabu yao. Akizungumza Bungeni wiki iliyopita, Mbunge wa Musoma Mjini (Chadema), Vincent Nyerere, alisema walimu hao wanatakiwa kutumika kufundisha shule zilizopo karibu na magereza kwa sababu hazina walimu wa kutosha. Nyerere alisema magerezani kuna walimu wengi wamefungwa, lakini serikali haiwatumii vyema badala yake inawapa adhabu ya kukata miti ovyo, ambayo ingetumika kutengenezea hata madawati. Alisema walimu hao walioko magerezani wanatakiwa kupelekwa shuleni kufundisha shule za kata na wakimaliza muda wao, wanarudi gerezani kama kawaida kutumikia kifungo chao kama wengine. Alisema shule za kata siyo za watoto wa wakubwa, bali wazazi maskini ndiyo maana haziendelei na hazitaendelea hata siku moja. Hapa Bungeni nina imani hakuna hata mzazi mmoja ambaye mwanaye anasoma shule za kata, hii inatokana na nini hasa zina wenyewe ambao ni walalahoi, alisema Nyerere. Pia, alisema haoni sababu za kuchangia mafuta ya mwenge wa Uhuru kutokana na faida yake kutoonekana. Alisema fedha ambazo zinachangishwa kwa ajili ya mwenge ni nyingi, zinatoka kwa wananchi ambazo zingetumika vizuri maendeleo ya nchi yangekua. Waliwahi kuja kwangu kunichangisha fedha za mafuta ya mwenge, nikawaambia twendeni nikawawekee mafuta kituo cha mafuta, wakasema wanataka fedha siyo mafuta nikawafukuza, alisema Nyerere. Alisema kuchangia mwenge ni sehemu ya ufisadi, kwani hakuna mantiki yoyote ya kuzungusha mwenge nchi nzima kwa sababu tayari umepoteza mwelekeo badala ya kupiga vita mafisadi unachochea. Alisema Mwenge unatakiwa kutumika vizuri kuibua maovu ya viongozi, siyo kuwamulikia taa mafisadi ili waendelee kutafuna nchi vizuri. Huu ni muda wa kuwafichua mafisadi siyo kuwamulika ili waone mbele kuna nini na kuendelea kuitafuna nchi vizuri, alisema Source: Mwananchi |