Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Watu wanafurahia kupendwa na wanapenda,lakini wapo wanaopendwa na vichwa vinakuwa vikubwa na kujisifia kuwa wanapendwa na kujisahau kabisa kuwa nao wanahitaji kurudisha upendo,uhusiano wa aina hii lazima utakufa tu,hivyo ni vizuri unapopendwa nawe ukarudisha upendo ili mfurahie mahusiano yenu,lakini pia unapokuwa kwenye mahusiano usikae kikondoo ukadhani kuwa huyo hawezi kubadilika,huyo sio malaika.Fikiria na upande mwingine wa shilingi,unaweza ukaachwa hata kama wewe ni mzuri,handsome,una hela,ni mtaalam kitandani n.k.Epuka kuja kuwa kichwa cha habari cha vyombo vya habari kwa kufanya mambo ya ajabu baada ya kuachwa!