Uzalendo wa Mwl Nyerere: Alimtoa mwanae kwenda vitani Uganda. Je, Mwinyi, Mkapa na Kikwete?

Nisilolifahamu vizuri ni baadhi ya watoto wa Mwalimu kuonekana kama wagonjwa wa akili vile na chapombe kwa sana kama huyu Makongoro na Rosemary. Kwa malezi nyumbani Mwalimu hakuwa mzuri sana. Hakuwa na muda? Mzee Karume hakwenda shule. Watoto wake wawili wamefika mbali. Mzee Ali Hassan Mwinyi watoto wake wengi wamesoma vizuri na wana nafasi zao. Infact, yule aliyegombea ubunge wa EALA jana alijieleza vizuri kuliko mgombea yeyote.
 
Dah! Nadhani wewe ndo unatakiwa ukafanye homework yako upya na vizuri zaidi. Habari za kifo cha rubani mtoto wa Nyerere hata binti yangu wa std 4 anazijua.
Hapana. Hizo si habari za kweli. Ila pilot aliyekufa ni kweli alikuwa mtu wa Musoma, labda ndiyo maana watu walifikiria kuwa ni mtoto wa Nyerere. Lakini kuongezea tu, Ali Hassan Mwinyi alivunja national service ili wanae wasiende huko.
 
Nadhani uko sawa kabisa.hawa wa siku hizi nao wanawatuma vitani ndiyo, ila tofauti ni aina ya majeshi mfano
*HUSSEN ALLY MWINYI, amejiunga na jeshi na amepigana pale mbagala na Gongolamboto hivi karibuni na kufanikiwa kuwafurusha wakazi wa dar es salaam kwa siku kadhaa na wengine bado wako kwenye kambi za wakimbizi.

*RIZ ONE K,amejiunga na jeshi la mafi**di na sasa wanaendelea kusonga mbele wakiwachakaza watanzania sehemu mbalimbali nchini hadi kupelekea wananchi kuanza harakati zao binafsi na wakijinunulia magwanda kwa kuchangishana na kuanzisha falsafa yao ya peoples power ili kupambana na jeshi hilo hatari


Duh, hiyo kali.
Na wengine wanapelekwa hadi wakwe zao frontline!

Hahahahaaaa
 
Hapana. Hizo si habari za kweli. Ila pilot aliyekufa ni kweli alikuwa mtu wa Musoma, labda ndiyo maana watu walifikiria kuwa ni mtoto wa Nyerere. Lakini kuongezea tu, Ali Hassan Mwinyi alivunja national service ili wanae wasiende huko.
Rubani aliyefariki alikuwa rafiki mkubwa wa kaka yangu. Jina lake Emmanuel Kerato. Alifariki muda mfupi tu baada ya kufunga ndoa. Ilitia simanzi sana. Moja ya misiba mikubwa niliopata kuishuhudia ni wa huyu rubani.
 
Hapana. Hizo si habari za kweli. Ila pilot aliyekufa ni kweli alikuwa mtu wa Musoma, labda ndiyo maana watu walifikiria kuwa ni mtoto wa Nyerere. Lakini kuongezea tu, Ali Hassan Mwinyi alivunja national service ili wanae wasiende huko.

true kamanda ..... mzee mwinyi alimkimbizia Hussein Mwinyi Turkey kusomea udaktari ....mara tu baada ya kumaliza form six..ili kumkwepesha na JKT...Tuseme sio Mwinyi pekee aliyechangia jeshi kufutwa ....kwanza kulikuwa na changamoto za benki ya dunia ,walikuwa hawalitai kabisa ...labda walikuwa na sababu za kimkakati ,.....na kuangalia uwezo wa Tanzana kivita ulioopelekea kupiana vita ya uganda,msumbiji,zimbwabwe ,angola na operesheni zake za kikachero south africa,nmibia na Angola....hii iliwatisha......pili ni ukiritimba wa maafisa wa serikali ya mwinyi waliokuwa wakikusudi kuwacheleweshea pesa jkt ..ili tu kujenga hoja kuwa serikali haiwezi kulihudumia ili tu watoto wao wasiende jkt........

kwa kuongezea Tanzania ilikuwa nchi pekee ya kiafrika iliyopata kuikalia nchi zingine ,,,na ikaondoka kwa hiari bila kuwaibia......kama alivyosema makongoro jana ,...baada ya ushindi wa vita mwaka 1979 wao kama maaskari na maafisa wa jeshi [chini ya maj gen msuya..enzi hizo kanali],polisi [akiwamo mahita]....waliendelea kuitawala uganda hadi mwaka 1982 na bado waliendelea kukaa hadi kusimamia ulinzi wa ndani na mipaka hadi Obote alivyoingia mara ya pili...waliondoka baada ya Nyerere kuona Obote hashauriki..n ushahidi ni kuwa Majeshi ta Tanzania yalipoondoka tu uganda ..vita vikaibuka upya......nyerere alikuwa na uwezo wa kufanya uganda kolonni...

pia tanzania imepata kuitawala Sychells kwa siku kadhaa baada ya kuzima mapinduzi '...pale na kanali iddi ganhu ,baadaye luteni jenerali na mnadhimu enzi ya mkapa ....alikuwa gavana kwa muda tu pale....hadi uchaguzi ukafanyika.....akarudi ....ache re -union etc

Wakati wa mkapa tena jeshi letu kwa kiasi kikubwa ndilo lilikuwa likimlinda kabila mkubwa ...na alipotofautiana na maafisa wa jeshi letu kwa kuchonganishwa na mapandikizi ya rwanda ndipo walipata fursa ya kumuuwa
 
Hahaaaaaaaaaaaaaaaa kweli waungwana mmenena. Sikuhizihata hao Majenerali hawataki watoto washiriki vitan hata kwenda kulinda Amani huko Somalia na kwingineko.
Na lilelile alilo likataaa Mwalimu ndo linatoke kwakusomesha watoto wao Ulaya huku watoto wa Makabwela waki saga jua na Mvua huku kwenye Shule zetu za Msondo ngoma.
 
true kamanda ..... mzee mwinyi alimkimbizia Hussein Mwinyi Turkey kusomea udaktari ....mara tu baada ya kumaliza form six..ili kumkwepesha na JKT...Tuseme sio Mwinyi pekee aliyechangia jeshi kufutwa ....kwanza kulikuwa na changamoto za benki ya dunia ,walikuwa hawalitai kabisa ...labda walikuwa na sababu za kimkakati ,.....na kuangalia uwezo wa Tanzana kivita ulioopelekea kupiana vita ya uganda,msumbiji,zimbwabwe ,angola na operesheni zake za kikachero south africa,nmibia na Angola....hii iliwatisha......pili ni ukiritimba wa maafisa wa serikali ya mwinyi waliokuwa wakikusudi kuwacheleweshea pesa jkt ..ili tu kujenga hoja kuwa serikali haiwezi kulihudumia ili tu watoto wao wasiende jkt........
PM,
Hivi ile sheria iliyokuwa inatupeleka JKT "kwa mujibu wa sheria" ilifutwa? Ni miaka karibu 20 sasa vijana wetu hawaendi huko. Mazuri yote ya Mwalimu yalifutwa kwa kasi ya ajabu. JKT ilichangia sana kutufanya WATANZANIA. Wameifuta kinyemela kama walivyolifuta Azimio la Arusha.
 
PM,
Hivi ile sheria iliyokuwa inatupeleka JKT "kwa mujibu wa sheria" ilifutwa? Ni miaka karibu 20 sasa vijana wetu hawaendi huko. Mazuri yote ya Mwalimu yalifutwa kwa kasi ya ajabu. JKT ilichangia sana kutufanya WATANZANIA. Wameifuta kinyemela kama walivyolifuta Azimio la Arusha.

sheria ya jkt kwa mujibu wa sheria bado ipo ila jkt walifuta kinyemela ..kwa kuanzia na mwaka 1990 wakapunguza toka mwaka mmoja haadi miezi sita ...,mwaka 1993 wakafanya kama sikosei miezi mitatu ....1994 ..hawakuchukua vijana ...toka hapo imebaki stori ,,..mwakani ..mwakani mwakani linarudi ...hata sasa waneahidi mwakani linarudi....ni bora warudishe hata miezi miwili kwa kuanzia ...crush program
 
Nilifurahi sana Makongoro Nyerere alipogusia bungeni ushindi walioiletea tz baada ya uvamizi wa IDD AMIN DADAA,najiuliza marais waliomrithi Nyerere wamepeleka watoto wao vitani kama vile kulinda amani Somalia,Comoro,Burundi nk au wanao siku hizi ni kupelekwa kusoma ulaya na kuja kugombea vyeo vya juu vilivoachwa na wazazi wao?. Mwenye details za mtoto wa rais mwanajeshi au polisi kwa sasa aujuze umma wa Watanzania

Gadaffi? Mubaraka? It doesn't suffice on its own.
 
sio jkt tu ...siku hizi hata maafisa wa jeshi wanaenda kozi miezi 6...eti wanaita kozi ya maafisa wasomi...uppuuzi huuu...ambao enzi ya mwalimu alikuwa hataki ...eti intake ya maafisa wasomi na wa kawaida ...what a waste??? maafisa wasio na degree bado wao wanaenda kozi munduli kwa miezi 12...

enzi ya nyerere afisa anatoka jkt miezi 12....,akiwa recruited ....anakaa miezi sita ..kambini [depo] ...,baada ya hapo akionekana anafaa ndio anaenda monduli,...miezi 12 ...so hata usome vipi unahitaji average miaka 2 kuwa afisa'''
 
umeenda mbali sana yaani,wajukuu wao tu hata chekechea wanasoma nje,Watoto wa Hussein Mwinyi wanasoma South Africa,mmoja miaka 9 na mmoja miaka 12.kama shule tu ni hivyo watakwenda vitani,
 
NIMEIFUTA KAULI YANGU;

reason;

i was wrongly informed.

munisamehe kwa usumbufu uliojitokeza.
mtoto wa nyerere hakufia vitani, lakini nasisitiza idi amini zilimnyeshea za masika hilo halina ubishi!!!!!!!

Umenukuu mpaka speech, sasa unadai ulikuwa wrongly informed?

Sasa haya kama siyo matongotongo kwenye ubongo, basi ni fikra zilizokamata kutu. Mbio za mwenge na slogan za zidumu fikra za sahihi za mwenyekiti wa CCM zimeacha athari kubwa kwa Watanzania kama makatambuga (viatu vya matairi) vilivyoacha athari kwenye viungo vya Watanzania. Just take off your shoes halafu angalia kama hakuna tundu kati ya dole gumba na dole linalofuatia. Hii ni sababu ya kuvaa viatu vya matairi wakati ule wa kufukuza magari ya ugawaji.
 
sio jkt tu ...siku hizi hata maafisa wa jeshi wanaenda kozi miezi 6...eti wanaita kozi ya maafisa wasomi...uppuuzi huuu...ambao enzi ya mwalimu alikuwa hataki ...eti intake ya maafisa wasomi na wa kawaida ...what a waste??? maafisa wasio na degree bado wao wanaenda kozi munduli kwa miezi 12...

enzi ya nyerere afisa anatoka jkt miezi 12....,akiwa recruited ....anakaa miezi sita ..kambini [depo] ...,baada ya hapo akionekana anafaa ndio anaenda monduli,...miezi 12 ...so hata usome vipi unahitaji average miaka 2 kuwa afisa'''
What kind of army are we creating now? Tanzania was capable, but under this leadership it seems Tanzania will always be dependent on "our friends" even for security issues. I cringed when I heard Kikwete asking Hillary Clinton to get us a ship to patrol our coastal line.
 
Umenukuu mpaka speech, sasa unadai ulikuwa wrongly informed?

Sasa haya kama siyo matongotongo kwenye ubongo, basi ni fikra zilizokamata kutu. Mbio za mwenge na slogan za zidumu fikra za sahihi za mwenyekiti wa CCM zimeacha athari kubwa kwa Watanzania kama makatambuga (viatu vya matairi) vilivyoacha athari kwenye viungo vya Watanzania. Just take off your shoes halafu angalia kama hakuna tundu kati ya dole gumba na dole linalofuatia. Hii ni sababu ya kuvaa viatu vya matairi wakati ule wa kufukuza magari ya ugawaji.
Kudadeki,
Kumbe bado umo JF. Kila siku nakusikia unaiponda kumbe ni kiherehere tu? Mweeee!
 
Ungekuwa na point kama tu tungekuwa tumepigana vita kwenye awamu zingine, mfano iwamu ya mwinyi vita labda mtoto wa mwinyi angekataa kwenda vitani ilihali yeye ni mwanajeshi. Ukishakuwa mwanajeshi huwezi ku avoid kwenda vitani, na hamna mwanajeshi anayesifiwa kwa kukubali kwenda vitani hiyo ni duty yake.

Otherwise naona mleta mada ukajipange upya
 
Ungekuwa na point kama tu tungekuwa tumepigana vita kwenye awamu zingine, mfano iwamu ya mwinyi vita labda mtoto wa mwinyi angekataa kwenda vitani ilihali yeye ni mwanajeshi. Ukishakuwa mwanajeshi huwezi ku avoid kwenda vitani, na hamna mwanajeshi anayesifiwa kwa kukubali kwenda vitani hiyo ni duty yake.

Otherwise naona mleta mada ukajipange upya
Mwinyi hana mtoto yeyote ambaye ni mwanajeshi. Hussein ni waziri wa ulinzi lakini hana utaalamu wowote wa kijeshi. Wewe ndiye unayepaswa kujipanga upya.
 
Asprini, kama hata mwanao wa std 4 analifahamu hilo basi twambie ni mtoto yupi wa Mwl. au ndg.gani wa mwl.aliyefia vitani? achana na kufia kwenye urubani.
Dah! Nadhani wewe ndo unatakiwa ukafanye homework yako upya na vizuri zaidi. Habari za kifo cha rubani mtoto wa Nyerere hata binti yangu wa std 4 anazijua.
 
Back
Top Bottom