Ni jambo la ajabu mpaka leo hii hatuwezi kutoa idadi kamili ya abiria wanapokuwa safarini kwenye vyombo vyetu vya usafiri.Tunahitaji kuangalia kwa hekima jambo hili hasa wamilki wa vyombo vya usafiri pamoja waliopewa dhamana ya kusimamia vyombo hivi waelewe masihara au uzembe juu ya suala hili linagharimu maisha ya watanzania.Tuwe na utamaduni wa kuwajibishana bila kuoneana aibu maana kwenye vyombo vya usafiri kulindana ni kuchezea uhai wa mtu ambao hauwezi kuthaminishwa kwa namana yoyote ile. Jisikie kuguswa unapochangia kupotea uhai wa Binadamu mwenzio kwa sababu ya uzembe wako au kutowajibika kwako.THIS IS TOO MUCH!!!
Ndugu zangu nchi hii kwa hivi sasa sijui tunakokwenda kwani matatizo kama haya yanapotokea tunapenda kulaumu vyombo vilivyoweka kusimamia lakini vyombo hivyo vikifanya kazi zake tunavilaumu sana. Kwa mfano siku ya j'mosi iliyopita nilipanda basi la mbeya express kuelekea mbeya na tulipofika morogoro askari aliingia ndani ya basi na kuomba manifest. baada ya kupewa akafanya random check kuthibitisha kama kweli majina ya wasafiri yana kubaliana na list ya manifest. askari huyo alikuta abiria kadhaa ambao majina/na ya tiketi hazikubaliani na list ya manifest hivyo akaamuru kondakta alipte faini palepae stendi. lakini cha kushangaza abiria walilalamika sana kutokana na uamuzi huo wa polisi tena kati ya waliolalamika ni wasomi wa chuo kikuu cha teku ambao walibeba bango hilo hadi likageuka kuwa la kisiasa.
Tanzania ni zaidi tuijuavyo [you are damned if you do and you are damned if you dont] god have mercy on us