Binti Magufuli
JF-Expert Member
- Apr 2, 2011
- 7,484
- 5,142
Nimeona nilete hii hoja huku kwenye wengi badala ya kuipost kwenye jukwaa la dini ili meseji ifike kwa wahusika kirahisi. Ni hivi, mbona mada za dini kule kwenye jukwaa husika hazina wachangaiaji wengi? Member wenye access ya jukwaa ni wengi ila mada zikipostiwa utakuta zina wachangiaji hata 10 saa nyingine hawafiki! Mfano mzuri ni mada ya imani na miujiza aliyoposti dada/kaka mmoja (nimemsahau jina) toka juzi hadi muda huu ina michango 3 tu! Hii ni hatari kubwa kwa kizazi cha leo kwani shetani ameamua kuwatawala na kuhakikisha mnabanwa na mada za ulimwengu huu na kuona mada za kiroho kama hazina mshiko! Amelaaniwa yeye ambae hatangulizi mambo ya kiroho mbele......., nimefikisha ujumbe na ukumbuke mjumbe hauwawi!!!