Uwajibikaji wa Vyombo vya habari wa Tanzania Media Fund Mlimani City

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
Richard Mgamba wa Sunday Guardian anasema, unapozungumzia media na uwajibikaji, unajiuliza tunawajibika kwa umma ama wamiliki?
 
Kwa kuwa mwandishi, nilijua naweza kutimiliwa anytime naweza kupata zawadi ama kupanda ngazi wakati wowote, kwanza nawajibika na sera ya gazeti na kila chombo kina policy.. Hatuko juu ya sheria, ukiona umekosea lazima uombe radhi na kuwajibika kwa wasomaji wako
 
Je, munawaheshimu wasomaji wenu? English paper ukikosea unarekebisha lakini magazeti ya Kiswahili yanarudia sana, anatoa mfano wa Tanzania Daima kwamba Magufuli amejiuzulu ama Sitta na Mwakyembe wameshughulikiwa na cabinet wakati hakukua na kikao siku hiyo
 
Simbeye anasema kuiwajibisha serikali lazima uwe na sababu, lazima kuwe na kitu cha kuiwajibisha serikali, lakn kama hakuna kitu unadhoofisha serikali bila sababu. Ktk media lazima kuwa objective.
 
Na sisi ni sehemu ya jamii, na si kweli kwamba na sisi tunafanya kila kitu sahihi na serikali tu ndio inakosea?
 
Ichikaeli Maro wa Daily News anasema lazima kama media house unakosea uombe radhi na kurekebisha... Lazima tuwape nafasi wanaotuhumiwa tuwasikilize na wao
 
Mwandishi mmoja anasema: ni mentality ya editors, hawako acountable kwa umma kama yule wa Daily News alikua anawajibika kwa watawala wakati wa uchaguzi na si kwa umma, tumeona Mkurugenzi wa TBC alikua anawajibika kwa umma na tumeona yaliyomkuta.... Anashangiliwa
 
Richard ni kweli kuna rushwa ktk media, lakini hiyo ni mzao wa jamii yetu ilyojengwa na watawala wetu
 
Pamoja na hayo, kuna kazi nzuri iliyofanywa na media, na ni media iliyoifanya serikali kuvunjwa na Bunge kuwa na meno
 
Kikao cha asubuhi cha postmortem kinatumika kupitia habari zilizotumika, na serikali nayo inafanya hivyo japo si kila mara kama media....
 
Mohamed Tiba anasema, kwa uzoefu wake ktk media, nimesoma magazeti, sijaelewa kama ni kuwajibishana ama ni vita kati yao na hii imenishtua maana tumeona media zinajenga uaduia miongoni mwao na ni tishio kwa uhuru wa habari na hatuoni vikifanya kazi pamoja
 
Editors Forum ni lazima iangalie uwajibikaji wa media kama taaluma sababu tungesahihishana kwa njia ya kistaarabu na kirafiki badala ya kufanya vita
 
Daladala producers: Siamini media japo niko ktk media, imebadilika na kuwa biashara. Ukikuta makala marefu mazuri na picha kuna bahasha imetembea
 
Nimetembea nchi nzima, ni vigumu kupata habari kibiashara, na baada ya kazi wakitoka wanasubiri bahasha baada ya kikao... Je, tunasema nje kulaumiana?
 
Kihaule wa EU, nianze ni kweli kuna tabia ya rushwa lkn si kweli kila makala inatolewa kwa fedha...
 
Wamiliki ni tatizo, hawawalipi vizuri waandishi na hapo wanalazimika kupata nauli na wApo wanaopenda waendelee kuteseka na njaa ili wapate nafasi ya kuwatumia
 
Imetokea katika kamoeni mwandishi akashuishwa kigoma kwa kutoandika vizuri mwanasiasa
 
Back
Top Bottom