Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Rais Barrack Obama wa Marekani amekatisha likizo yake mara moja na kwenda kujumuika na kituo cha kuchunguza mwenendo wa kimbunga Irene na kuratibu mambo mbalimbali ikiwepo kuokoa maisha ya waadhirika na huduma mbalimbali.
Viongozi wetu wanapaswa kujifunza kutoka kwa hawa wenzetu, maana kwetu utashangaa janga zito kitaifa au kiutawala linatokea utaona kiongozi ndio anadandia ndege kwenda nchi za nje, na matokea yake viongozi waandamizi kila mmoja anafanya na kutoa kauli yake kama anavyoona na kufikiria kwa sababu rubani wa nchi haoni uzito wake na cruel wake wanabaki kwa mtindo wa paka akitoka panya anatawala.
Bahari ya Atlantic si shwari, ni bahari yenya hatari nyingi kuliko bahari nyingine zote katika dunia yetu, na nibahari yenye kina kirefu kuliko hata Pasific ambayo ni kubwa zaidi. Hata usafiri wa angani ndege na usafiri wa meli si huru kukatisha bahari hii ila kuna maeneo maalum yaliyoratibiwa kuwa salama kukatisha. Kama triangle circle karibu na visiwa vya Bermuda baada ya meli nyingi na ndege nyingi kuangamia ni eneo ambao vyombo vya majini havithubutu kutia pua. Afrika wangesema kuna majini.
Chimbuko la vimbunga linaloikumba Marekani si Marekani kwenye ila ni sehemu ya visiwa vya Kerubiani na kuna vimbunga vyenye mianzo tofauti kuendana pia na mieleko yake inakoishia. Kwa maana hiyo wataalamu wamevipa majito kutokana na utaratibu huo wa vianzio na mwelekeo wa vimbunga hivyo.
Bahati nzuri wenzetu wana vyombo vya uhakika na wataalamu wa hali ya hewa waliobobea, maandalizi ya kimbunga hiki cha Irene yalianza wiki mbili zilizopita na kujua ni upande gani kitaelekea baada ya kuzuka huko baharini Atlantic karibu na visiwa vya Sichelesis na Kerubian. Tofauti na kwetu hujui nini kitatokea zaidi ya kusoma ishara za wingu jeuzi na zito.