LUS0MYA
JF-Expert Member
- Aug 4, 2011
- 862
- 1,097
Rais wa awamu iliyopita aliwahi kusema watanzania ni wavivu wa kufikiri! Watu wengine walikebehi na kuona kama wametukanwa!
Hebu angalia watu waliopewa dhamana ya kufikiri badala yetu wanavyochemsha.
Naanza na hili la nishati ya gesi.
Nakumbuka nderemo zilitawala nchi hii pale tulipogundua hazina kubwa ya gesi pale songo songo, watanzania tumepata nishati nafuu sasa mkaa bye bye, aaah wapi mjanja kaingia katoa msaada wa kujenga pipeline toka Huko kuja dsm. Kilichotokea gharama za kusafirisha gesi kuja ikawa kubwa hivyo bei yake ikapanda ikawa sasa inalingana na bei ya kuagiza gesi nje!
Tukifikiri kidogo tukawapa eneo Tanesco huko songo songo wakaweka mitambo inayotumia gesi wakainunua kwa bei nafuu na kusambaza umeme kwa gridi kuna haja ya kununua majenereta yanayotumia mafuta? Hii mitambo ya Tanesco bado yatakiwa kukaa hapa mjini?
Mtazamo wangu: SONGAS imefanya gesi yetu kuwa ghali labda wangejenga pipeline kwenda nchi jirani kama zinahitaji lakini siyo hapahapa nchini. Sasa viwanda vikubwa vya cementi, Nondo, Usindikaji, Tanesco waende kwenye source wasisubiri kuletewa gesi hapa dar!
Unajua kwanini nchi zetu zinaingia katika machafuko? Ni pale wananchi wanapoona rasilimali iliyogunduliwa haijabadilisha kitu chochote ktk maisha ya watu.
Hata tukigundua mafuta hakuna unafuu kama tutakuwa wavivu wa kufikiri na kubaki wajinga.
Hebu angalia watu waliopewa dhamana ya kufikiri badala yetu wanavyochemsha.
Naanza na hili la nishati ya gesi.
Nakumbuka nderemo zilitawala nchi hii pale tulipogundua hazina kubwa ya gesi pale songo songo, watanzania tumepata nishati nafuu sasa mkaa bye bye, aaah wapi mjanja kaingia katoa msaada wa kujenga pipeline toka Huko kuja dsm. Kilichotokea gharama za kusafirisha gesi kuja ikawa kubwa hivyo bei yake ikapanda ikawa sasa inalingana na bei ya kuagiza gesi nje!
Tukifikiri kidogo tukawapa eneo Tanesco huko songo songo wakaweka mitambo inayotumia gesi wakainunua kwa bei nafuu na kusambaza umeme kwa gridi kuna haja ya kununua majenereta yanayotumia mafuta? Hii mitambo ya Tanesco bado yatakiwa kukaa hapa mjini?
Mtazamo wangu: SONGAS imefanya gesi yetu kuwa ghali labda wangejenga pipeline kwenda nchi jirani kama zinahitaji lakini siyo hapahapa nchini. Sasa viwanda vikubwa vya cementi, Nondo, Usindikaji, Tanesco waende kwenye source wasisubiri kuletewa gesi hapa dar!
Unajua kwanini nchi zetu zinaingia katika machafuko? Ni pale wananchi wanapoona rasilimali iliyogunduliwa haijabadilisha kitu chochote ktk maisha ya watu.
Hata tukigundua mafuta hakuna unafuu kama tutakuwa wavivu wa kufikiri na kubaki wajinga.