Paulo
JF-Expert Member
- Jan 5, 2009
- 350
- 66
Wana JF naamini wengi wetu tulisoma lile tamko la vijana wa CCM kuwa wanataka mjadala wa Dowans urudishwe bungeni ili umma ujue mmliki wake ni nani. Swali likawa Je, nani kawatuma hawa vijana? Baada ya pekua pekua inaonekana kuwa Edward Lowassa ndiye aliyewatuma. Kwanini EL? Kwasababu EL ndiye mwenyekiti wa bodi ya wadhamini ya UVCCM. Pili ndiye aliyekuwa anapiga debe Beno Malisa awe m/kiti hadi ikafikia stage pale mwanahalisi liliponanga kuwa mtoto wa Kikwete anataka kumhujumu babake likafungiwa. Pili EL amekuwa akipinga tangu mwanzo kuwa dowans si yakwake ila hakutaka kumsema. Tatu, hata Dr. Slaa mwenyewe hajawahi kumtaja EL kama ndo mmiliki wa dowans bali alimtaja yule bwana mkubwa. Nne, EL amekuwa akihudhuria matamasha mbalimbali kama njia ya kujirudisha kwenye jamii ili aweze kupita kilaini hapo 2015. Mfano hivi majuzi alihudhuria uzinduzi wa studio ya Mbasha, pia kabla yake alikua kwenye studio ya THT, na emekua akifanya fundraising ya makanisa. Pia hata kule arusha ambapo yeye ni mjume wa wadhamini wa CCM alionekana kutaka CDM na CCM wakae pamoja watatue tatizo la umeya. Pia amekua akiunga mkono katiba mpya na kusikika akisema watu wadai katiba kwa amani na upendo na tuepuke vurugu! Yaani amebadilika ghafla na sii bure yeye ndo emewatuma wale vijana waseme dowans irudishwe bungeni ili aweze kusafishwa. Ama wakuu mwaonaje kasi ya huyu jamaa?