UvCCM wahaha kurudisha imani ya vijana kwa CCM

nguluvisonzo

JF-Expert Member
Dec 27, 2010
515
71
Hakika wanavuta shuka asubuhi, kuna mambo mengi sana kiasi kwamba kurudisha imani kwa CCM si rahisi kwa muda huu,kung'ang'ana na bodi ya mikopo ivunjwe eti kwa fikra zao ndio inakimbiza vijana kutoiunga mkono sio sahihi, hiyo bodi ni sera yao na serikali ikatekeleza kuiunda, pesa ya kuindesha kwa kuwapatia mikopo wanafunzi wanalipia mikataba mibovu na mambo mengine yasiyo na tija kwa taifa letu.

Wakumbuke kuna msururu wa mambo mabaya ambayo yameliangamiza taifa letu walitakiwa wayasimamie mapema walishindwa kufanya hivyo walichofanya ni kushirikiana na kutafuna rasilimali za taifa letu kwa mgongo wa UVCCM.

Hii ni dalili ya mfa maji waliwekeza kwa ajili ya kuja kushika hatamu na wao walitafune taifa hili sasa wamebaini kuwa mbele ni giza matarajio yao hayapo tena,watanzania wamekwisha jua mbivu na mbichi na juu maovu yaliyo ligharimu taifa letu yatawekwa wazi na wahusika wote wachukuliwe hatua.

SHUKRANI KWA VIONGOZI WA VYUO KUSHITUKIA DILI LA CCM NA KUKATAA KUSHIRIKIANA NAO KATIKA MAANDAMANO WALIYOYAITISHA,PIA NATOA WITO KWA WANAFUNZI WA SEKONDARI WASIDANGANYIKE HATA KIDOGO KUJIINGIZA KATIKA HIKI WANACHOKIFANYA CCM, TUSEME INATOSHA INATOSHA.

:embarrassed:
 
Tatizo la Bodi ya mikopo ni Ikulu yenyewe, kwani bodi ina miradi gani ya kuingizia pesa? Ni mgodi wowote au bishara ya cocaine?

Kwa nini wasiandamane mwenyekiti wa chama chao apunguze safari za nje? Maana gharama ya kila safari moja ni mkopo wa wanafunzi mamia.

Shame on him, shame on them!
 
wanajidanganya kwa kudhani kuwa wataungwa mkono na movement yao ya kinafiki
 
Hamna mfikiriaji. Hukuona lile tamko lao lilivyokuwa lilivyoandikwa kama wote ni wavuta bangi na mateja?
 
Janja yao ilishagundulika siku nyingi wanajua wazi kua asilimia kubwa ya vijana wameitosa CCM sasa wameamua kutumia mbinu za ujanja kuwateka vijana ili waone wana ccm wanachukizwa na malipo ya dowans. Nawapongeza mawaziri wa mikopo wa vyuo vya elimu ya juu kwa kuwajibu UVCCM kwamba wasiingilie utendaji wa bodi ya mikopo na kutoa ushauri usio na tija..
 
UVCCM :A S thumbs_down::A S thumbs_down::A S thumbs_down::A S thumbs_down::A S thumbs_down::A S thumbs_down::A S thumbs_down::A S thumbs_down::A S thumbs_down:
 
Hata wafanyaje, Hawana issue. Kwanza sela yao Vijana ni taifa la kesho-yaani mpaka uzeeke ndio unafanya kazi za vijana. Hatuwataki, hao taifa la kesho
 
mbna hawa UVCCM siwaelewi?ukiangalia vijana wa CCM UTAKUTA NI WA AKINA JK wadogo,na wengine wengi,watu tunafanya siasa tu tokea miaka 49 iliyopita huku mambo mengi yakienda mrama,na kwa taarifa tu kwa kipindi cha 2010-2015 kuna vijana zaidi ya milioni moja watapiga kur na nina amini ndio utakuwa mwaka wa mageuzi
 
CCM ilishiaandika dhambi zake on SILVER PLATE.....Kutubu kwa aina yoyote ile ni kama WANAZING'ARISHA.......
 
hawa wameshapoteza ushawishi kama baba yao Makamba,hakuna kijana atakae wasapoti,hawana mvuto wamelala mpaka wanafunzi tumeteseka cha kutosha,wengine wameshamaliza vyuo wengine waliishia njiani,walikuwa wapi?walishindwa kuwashawishi wakubwa zao kwa kua wao walipata elimu bora au pengine kwa ujinga wao. vijana werevu waligundua kwamba wanakua watumwa katika nchi yao,tumechoka tunataka suluhu ya kudumu ya matatizo ya elimu ya juu,hawana nia ya kutuendeleza vijana, wanatuonjesha elimu kidogo na duni kutimiza wajibu mbele ya wahisani.
 
inavyoonekana hawaelewi hata taratibu za bodi ya mikopo walizitunga vipi?
 
UVCCM wanajua mambo mawili. Kuporomosha matusi na la pili kula na kufagilia ufisadi. Wamesahau walivyofadhiliwa na Tani Somaiya yule fisadi wa Rada. Shame on UVCCM. Kujikomba wakati huu ni kazi tupu.
 
Wana vyuo kataeni hiyo hadaa ya uvccm. Chama chao ndicho chanzo cha matatizo yote yanaowakabiri hivi sasa; kama hisingelikuwa ubadhirifu mkubwa unao endekezwa na ccm mikopo ya elimu ya juu ingelitolewa kwa asili mia, na hivyo kusingelikuwepo umuhimu wa kuwa na bodi ya mikopo. Mambo yalikuwa hivyo wakati viongozi wa juu wa sasa walipokuwa vyuoni.
 
Ndugu jamaa namarafiki humu ndani ya JF naomba ushauri wa kizalendo, upendo na wakidemokrasia. Wewe binafsi unafikiri wana CCM wafanye nini kuhakikisha imaniwaliyokuwa nayo huko nyuma mbele ya Watanzania iweze kurudi?
Naombakuwasilisha.
 
Wavue magamba kwa vitendo na wala siyo kwa usanii kama wanavyofanya sasa. Na je huo ubavu wa kutekeleza hilo wanao?
 
tieni tieni tieni kwa moyo mmoja............
respect mkulu coz bila ww ccm isingeporomoka.........
 
tieni tieni tieni kwa moyo mmoja............
respect mkulu coz bila ww ccm isingeporomoka.........

Mfumo wa CCM ni wa kushindwa tu,Bila ushirikina CCM inaweza kurudisha imani ile ya kale.Jiulize tu kwa nini CCM haikutumia watumishi wa MUNGU kama Mch.Rwakatare na wengine?bila shaka waliogopa kuchanganya madudu.MUNGU YU MWEMA,CCM MUDA SI MREFU WATAUNGANA NA KANU,ZANU NK KWANI KUNA WABUNGE WAKE KAMA 80 AMBAO NI CLEAN NA SI WANAFIKI WATAJIUNGA NA CDM AS Pentagon in M4C will continue to prevail.
 
Back
Top Bottom