UVCCM: Usalama wa taifa haumsaidii rais, unavuruga nchi kwa maslahi yake

Kikwete hakuwahi kuhojiwa na wananchi kabla ya kupata kazi aliyo nayo. Mwaka 2005 hakukuwa na mdahalo, na mwaka 2010 pia hakukuwa na mdahalo. Kwa hiyo alipewa kazi kazi bila intavyuu, na sasa ni wazi kuwa alipewa kazi asiyoijua na asiyoiweza.
 
Nilishawai kuandika kuhusu hwa jamaa TISS, ni kwamba CCM ni kama bango tuu ila wanaoiaribu hii nchi ni hawa jamaa

Mfano:- CCM inatambua bila hawa jamaa awawezi kuingia madarakani na ndio maana kila mkoa kwenye uchaguzi wanakuwepo.
Pili-Hata kumchagua Rais ndio hao wanahusika na ndio maana utakuta marais wote nchini wanaongozwa na wao hawawezi kumweka mtu kama slaa au magufuli cause utakua mwisho wao wa kutukuzwa. Tatu ukikumbuka hawa jamaa ni inteligencier ya mwalimu na wengi wao waliku darasa la saba au hawakusoma kabisa so walipopata mwanya wakajisomesha ili kuja kushika mashirika yote hapa nchini na baadhi ya private sector kujipenyeza kwa ajili ya usalama wa taifa so, utakuta all CEO katika mashirika yote ya uma ni wao na baadhi ya private sector mwanajf utajidanganya kuuomba uCEO kwenye sector za umma na ukapata bila kuwa mwanausalama.
Nne utakumbuka wakati alipokua nyerere mashirika yalikua yanaongozwa na Raia wenye elimu na ujuzi na ndio maana yalikua active so, baada ya nyerere zikafanyika propaganda mpaka wakaweza kuyamiliki mashirika yote ya uma na ndipo kufa kwa mashirika mengi yakaanza hapo.
Tano- Jiulize mikataba yote mibovu lazma wao waipitie hata kuwaleta mainvestors matapeli wao ushiriki mfano EPA na kampuni zake zote zilizoshiriki utakuta ni wao
Sita- Rais awezi kuja kuhutubia taifa bila wao kuhusoma hotuba na kuihakiki, Rais uandaliwa bajet kubwa na safari ukiwa na msururu wa wanausalama ilimradi wapate posho.
SAba- ulishawai kusikia wapi mjadala wa bajeti ya hawa watu? hata kujadiliwa bungeni? wizara zote zinaendakuomba fungu pale lakini hawa warecommend tuu tunataka kiasi fulani na akina mahesabu.

so wanajf mtasumbuka sana kuilaani CCM lakini ccm kwa ujinga wao wanatumiwa kama chambo tuu ila wahusika wanaoisumbua hii nchi ni wao.
Na ukiwa mfuatiliaji sana wanakumaliza hata slaa ataongea sana ila anakikomochake cause baadhi yao walishakula kiapo cha kutunza siri sifahamu kama slaa ameshakula kiapo ila ukishafikia grade kama ya slaa lazma usign hicho kiapo.

Nchi inaendeshwa na TISS na sio chama hata mweke chama gani TISS ndio inayoongoza nchi kupitia mgongo wa chama

Wana jf huu ndio mchango wangu kaa chini na tafakari.


Yaani umelenga baadhi ya mambo kwa undani na uzuri sana na hata hili la kuchomolewa hoja yako uliyoiweka humu jamvini lina ukweli mkubwa hawa jamaa wana mkono humu tena mkubwa
na wa kutosha na kama huamini jidai unaishupalia hii idara utona jinsi mada hiyo itakavyotupwa kapuni anyway tuyaache hayo maana njaa zetu ni mbaya sana ila ukweli umewekwa wazi na wachangiaji kwa kiwango kikubwa sana na Arafat, na kwa undani Dk. Slaa baadhi kashfa ameziweka humu ndani na kuna nyingine nyingi kiasi ambacho ukiziorodhesha hapa utaona hili dude ni janga la kitaifa na ni chombo maalum ambacho mafisadi walioko madarakani wamewaweka viongozi wakuu wa idara na wengine kibao kwa masilahi yao na hivyo rais hafurukuti na hana maamuzi na kama akipishana nao kidogo na viongozi wa idara hii au kuwachukulia hatua mafisadi maisha yake yanakuwa hatarini maana sehemu zote ameshikwa pabaya.
 
Hivi tiss ni nini hasa kwa tz? Maana walianza kulala tokea enzi za mkapa kny nbc na nmb.
 
UVCCM wanakuwa waropokaji,these guys are lazy in the head,they cant even think of creative solutions to solve Youth problems. I feel they sometimes speak from a perspective of what they personally wish to happen rather than allow the wing be informed as to what is most likely to happen based on what is actually on the ground.

Uchaguzi wao 2012 watajikuta wamebakia na options za candidates ambao ni pro-
CHADEMA covertly.Hii ni strategy ya divide them from within.Yes i said tunaweza kuwafanyia hivi

They failed to understand the system and National agenda on vital issues.
The success of government depends on the level of creativity, dynamism and coherence in T
azania. The government is an innocent mirror of the collective consciousness of the nation. If Tanzaniais not strong and integrated, no government policy, no matter how wise or how well conceived, will be able to generate progress and success. When collective consciousness is coherent and awake in Tanzania, the life of the nation grows to be in tune with Natural Law. Until now, this important element has been missing from the functioning of government in Tanzania and as a result, the government has continued to be beset by problems. This is why governments have continued to perform with lack of efficiency and effectiveness and have not succeeded in fulfilling their responsibilities to the nation and not the fallout or weakness of TISS. UVCCM ni desperate Entity with immaturity .

Ngoja Tuchukue uongozi wa BAVICHA tuwafundishe kazi !!!We are going to establish a credible entity and Management style of Leadership with perfect managers that discharges the job descriptions perfectly,we believe Bad leadership causes bad followership! UVCCM watch our steps!!



 
UVCCm wanatumwa kusambaratisha chama chao,wanajitahidi kutoa umma kwenye agenda za kitaifa na wanalengo la kiini macho kuwazuga vijana nadhani uongozi wa UVCCm kama ulivyo kwa sasa hauna agenda zaidi ya kusimamia maslahi ya Jakaya Kikwete,wamekosa heshima kwa viongozi wengine wa CCM huo si mwenendo mzuri hata kama ningependa CCM ijizike
 
Wakati TISS walipoingiza kontena la kura kule Tunduma mbaona UVCCM hawakuona wanavuruga nchi?
ukiangalia matokea ya uchaguzi wa mwaka 2010 haiingii akilini kwamba TISS waliingiza makonteina ya kuchakachua kura. Binafsi naona Rais asingepata asilimia 61 kama tulivyoshuhudia. Hizi ni propaganda za kisiasa za kulikuza jambo hili ingawa mtazamo wangu haondoi ukweli kwamba hakuna uchaguzi unaoweza kukosa malalamiko.
 
mimi nadhani vijana wa CCM kuna kitu cha kuwafanya wawe machizi wamelishwa kwanini uwezo wao wa kufikiri ni mdogo kiasi hiki?
 
Mbona Mkapa hawakuwahi kusema usalama wa Taifa haumsaidii? huyu Mkwere ni janga la Taifa, anachotaka kusikia yeye ni mambo matam matam, mfano umwambie kwamba foleni kubwa kwenye barabara za jijini Dar ni dalili za maisha bora hapo ndio atafurahi, hataki umwambie kwamba tatizo barabara ni chache na zile za mitaani hazipitiki ni mbovu na miundombinu ni mibovu, ukimueleza hayo wewe unavunja amani na utulivu.

Tunaposema Mkwere ni kukuza ukabila usiokuwa wa lazima. Tukianza leo kuwabatiza viongozi wetu majina yao kugeuka ya kabila lao kwa mfano kusema yule Mchaga kwa Mbowe, Mbulu kwa Dr Slaa, Mnyamwezi kwa Lipumba, Mzanaki kwa Nyerere, Mmakua kwa Mkapa, Muunguja kwa Mwinyi, hakika tunalipelekea taifa pabaya. Kila jambo baya huanza taratibu na baadaye kuwa janga la kitaifa.
 
Kama nimemwelewa vizuri mtoa hoja alitaka tumsaidie kuthibitisha kama kweli UVCCM walizungumzia kuwa TISS hamsaidii Rais na ndio mada yenyewe, kwa maana hata yeye hakutaka kwenda kwa ndani hana uhakika lakini jambo la ajabu kabisa sisi sote tumeshindwa kuthibitisha na mara moja tumejikuta tunachangia kwa ushabiki zaidi.
 
Heshima kwako Dot Connector,

Mkuu kwa hili niko pamoja na UVCCM.Ukiisikiliza hotuba ya Kikwete mwisho wa mwezi uliopita utagundua kweli TISS wanampatia taarifa za kumwangamiza kabisa badla ya kumsaidia kumjenga.Ipo tafauti kubwa baina ya Kikwete kipindi kile akiishambulia picha ya mapanki [Sangara] au wakati akifungua bunge mwaka 2005 na hotuba alizozitoa baadaye anaonekana akilalamika kama mwananchi wa kawaida asiye na mamlaka yoyote.Kitendo cha kulaani maandamano ya CHADEMA kkiliitimisha hisia zangu Kikwete nchi imeshamshinda siku nyingi.

Hakuna Rais aliyewahi kutoa hotuba kwa vipindi viwili vya utawala wake hapa duniani au kwa miaka kumi hapa Tanzania na hotuba zake zote zikapendwa na wananchi wote. Ni haki yako kuona kwamba Rais hakuongea kitu cha maana lakini pia uwape haki hiyo hiyo watanzania wenzako wanaoona kwamba hotuba ya Rais haikuwa na kasoro kubwa kiasi cha kuibeza kabisa kabisa.
 
Maudhui ya taarifa hii ni kama imetoka kwa mwanachadema ambaye alikaa pamoja na Dr Slaa wakipata bia ndipo stori za TISS na UVCCM zikajitokeza. Dr Slaa aliota CCM muda wote lakini hii isitufanye wote tukashindwa kuchambua ukweli wa thread za kichochezi kama hii. TISS inaweza kuwa na mapungufu kama ilivyo kwa taasisi zingine zote lakini tuitendee haki penye kuhitajika haki.
 
Lakini hawa vijana wanataka TISS ndiyo wawe wanasema kwenye media? Je wanataka TISS iwaambie inamsaidia vipi rais?
Je kuna chochote kinachofichika ambayo JK hayup?
Je gharama za maisha hazijapanda sana?
Je vipato vy Mtanazania havijashuka?
Je ufisadi haujakithiri?
Miundo mbinu, je? Inafanyiwa kazi?
Nchi haipo gizani?
Wale wanaotusaidia budget wameona kuna tatizo na ndiyo maana hawajatoa fedha.
Hata budget ya mwaka 2011/12 inabidi iwe ndogo na yenye kutegemea mapato ya ndani kwa zaidi ya 80% ili angalau tuonyeshe ukweli katika kupanga kwetu na mapato yetu.
Vijana inabidi wajue majukumu yao na siyo kumharibia JK, wao wanadhani wanawaharibia EL na Sumaye, lakini wanamharibia rais zaidi ya CCM yao wanaichimbia kaburi zaidi.
Hawa watoto inabidi saa nyingine wakemewe, waache longolongo na kucheza na media, maana media itawamaliza mara moja!!!!!

Lakini hawa vijana wanataka TISS ndiyo wawe wanasema kwenye media? Je wanataka TISS iwaambie inamsaidia vipi rais?
 
Mkuu Saigon, avatar yako imetulia sana, kipindi hiki cha kasi zaidi...teh..teh..teh....
 
Ukisia ushamba ndio huu, JK original alikuwa anaitwa mchonga, kuna sehemu inaitwa kibaha kwa mfipa, mifano ya namna hiyo iko mingi nadhani wenzangu wataongezea orodha hapa, ninachokiona hapa kwako ni zile posho za lunch mlizopewa pale Dodoma za sh 50,000 kila mjumbe ndio bado zinakulevya. otherwise una point tambaa.

Kuna kipindi chadema ya Mbowe na Mtei walikuwa wanalalamika chama hicho kuhusishwa na wachaga leo tena CCM ya Kikwete inahusishwa na wakwere.... Ni yale yale ya kuleta ukabila kwenye siasa.
 
Nick name yanayokubalika na jamii mara nyingi hubandikwa watu kulinga na hali, jinsi au mambo wanayoyafanya na kwa kweli huya yanakaa vizuri kuliko hata majina yao. Kwa hiyo Mkwere siyo jina baya na kwa kweli linamkaa vema. Kuhusu kulalama kwa UVCCM, Matatizo ya CCM yapo kila idara sasa hivi. Kuanzaia shina hadi taifa na watawalalamikia wengi muno kwa sababu si watu wa kutatua matatizo. Walianza na CDM, Makanisa, sasa TISS. Sasa TISS si ndo wanoongoza nyingi au wamewatenga na kumwajiri sheikh Yahya. Kama ndo hivyo, basi wameshapotea njia. Kila la kheri CMM kwani uswahiba, ufisadi, rushwa na Uvivu ndo vinakuuwa.

Hizi ni siasa za kale zilizojaa ukongwe. Tumekuwa tunasisitiza mara kadhaa TISS isijihusishe na siasa wala chama fulani cha siasa. TISS inaishauri serikali sio chama cha siasa au UVCCM kama hili lilijitokeza katika vikao hivyo ni makosa. TISS ni above UVCCM... TISS haipo kushawishi chama fulani kushinda ni makosa kuiingiza TISS katika mjadala wa kushinda au kushindwa kwa CCM katika uchaguzi uliopita.

TISS ibaki na kazi yake ya kushauri tu yanayotokea katika uwanja wa siasa ni ya wanasiasa wenyewe..... TISS iwajibike kwenye uwanja wa usalama wa nchi.
 
Tatizo hapa JF mkwere linatumika kama jina la kumdhihaki Rais. Tuheshimu makabila ya watu.

Wewe ndio Salva Rweyemamu? hebu tuondolee kiwingu, huna uwezo na hautokuwa nao wa kutufundisha sisi tumuite kwa jina lipi Mkwere, kama inakukera nakushauri nenda kapoteze muda wako kwenye website ya ccm uangalie miradi ya chama, huko utakutana na taarifa ambazo unapenda kuzisikia, hapa umepotea njia, hatupo hapa kumpaka mafuta Mkwere wakati ndugu zetu wanakufa njaa kwa kukosa milo mitatu.
 
Hao UVCCM ina maana walikuwa hawajui kuwa TISS imegeuka taasisi ya ccm kama uwt, uvccm na umoja wa wazazi?TISS ni kama green guard kazi yao kulinda maslahi ya ccm?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom