nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Imeandikwa na Anastazia Anyimike;
Tarehe: 29th October 2011
VIJANA wa CCM nchini wameruhusiwa kujadili urais wa mwaka 2015 na si kujadili nani atakuwa rais kutokana na chama chao.
Hayo yalisemwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Steven Wasira, alipozungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam.
Wazira ambaye pia ni Waziri Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu, alisema si busara kuzuia mawazo ya vijana ambao ndio wanaoshika mhimili wa nchi, kuacha kujadili urais.
"Utaratibu wa chama chetu uko wazi, linapokuja suala la mgombea urais, kuna taratibu zake ndani ya chama, lakini hatuwezi kuzuia vijana kujadili urais, kwani ndio mhimili wa baadaye wa nchi.
Lakini hawatakiwi kumjadili mtu au sura ya mtu. "Unajua unapotaka kuzungumzia urais kwa kigezo cha sifa za rais, lazima utaangalia matatizo ya Tanzania ambayo ndiyo yanayotengeneza sifa za rais.
Tunataka urais kuwa ajenda na si sura ya mtu," alisema. Akizungumzia mgogoro wa Umoja wa Vijana wa CCM mkoani Arusha, Wasira ambaye ni mlezi wa chama hicho mkoani humo, alisema mgogoro huo umemalizika baada ya kukutanisha pande mbili zilizokuwa zinavutana.
Alisema baada ya kukutana na wahusika, amebaini kuwa kukosekana kwa mawasiliano yanayozingatia kanuni ndicho kilikuwa kilio cha kujengeka kwa hisia ambazo zilikuwa zinachangia mtafaruku.
"Hakuna hata mtu aliyeeleza chanzo, tukabaini kuwa tatizo lilikuwa ni kukosa mawasiliano kati ya wilaya na mkoa, na hili lilichangia hisia zaidi kuliko jambo lenyewe. Baada ya kukutana na pande zote, sasa naweza kutangaza kuwa tatizo hilo limekwisha na sasa wanaungana kuimarisha chama," aliongeza.
Aidha, Wasira alikiri kuwa mtafaruku huo ni matokeo ya kushindwa katika jimbo la Arusha Mjini katika uchaguzi wa mwaka 2010 na kuwa vijana walikuwa na maoni tofauti kutokana na kushindwa huko.
Katika uchaguzi huo, jimbo hilo lilichukuliwa na Godbless Lema wa Chadema.
Naye Katibu Mkuu wa UVCCM, Martin Shigela, alisema mgogoro uliokuwa Arusha, haukuhusu mgombea urais mwaka 2015 na kuwa taratibu za kumpata zinajulikana ndani ya chama.
" UVCCM haina mgombea urais kwa ajili ya uchaguzi ujao, utaratibu ndani ya chama uko wazi, muda ukifika watu watatangaza nia na sisi tutampigia debe mtu atakayepitishwa na chama na si vinginevyo," alisema Shigela.
Ziara ya Wasira ilimkutanisha na UVCCM wilaya ya Arusha, wajumbe wa Baraza la Vijana la Wilaya ya Arusha Mjini, Baraza la Mkoa, Kamati ya Siasa na Baraza la Wazee katika vikao vilivyohudhuriwa pia na Katibu wa CCM wa Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda.
Katika siku za karibuni, Arusha iligeuka chimbuko la vita vya maneno miongoni mwa makada wa CCM, hulka ambayo ilisambaa hadi kwa viongozi wa kitaifa wa chama hicho hasa kutokana na falsafa ya kujivua gamba.
Awali, mgogoro ulikuwa baina ya baadhi ya vijana wa wilaya na mkoa wa Arusha na Katibu wa CCM wa Mkoa, Chatanda, ambaye pamoja na viongozi na makada wengine, walituhumiwa kwa kilichoelezwa kuwa ni kusababisha chama hicho kipoteze ubunge wa Arusha Mjini.
Tarehe: 29th October 2011
VIJANA wa CCM nchini wameruhusiwa kujadili urais wa mwaka 2015 na si kujadili nani atakuwa rais kutokana na chama chao.
Hayo yalisemwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho, Steven Wasira, alipozungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam.
Wazira ambaye pia ni Waziri Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu, alisema si busara kuzuia mawazo ya vijana ambao ndio wanaoshika mhimili wa nchi, kuacha kujadili urais.
"Utaratibu wa chama chetu uko wazi, linapokuja suala la mgombea urais, kuna taratibu zake ndani ya chama, lakini hatuwezi kuzuia vijana kujadili urais, kwani ndio mhimili wa baadaye wa nchi.
Lakini hawatakiwi kumjadili mtu au sura ya mtu. "Unajua unapotaka kuzungumzia urais kwa kigezo cha sifa za rais, lazima utaangalia matatizo ya Tanzania ambayo ndiyo yanayotengeneza sifa za rais.
Tunataka urais kuwa ajenda na si sura ya mtu," alisema. Akizungumzia mgogoro wa Umoja wa Vijana wa CCM mkoani Arusha, Wasira ambaye ni mlezi wa chama hicho mkoani humo, alisema mgogoro huo umemalizika baada ya kukutanisha pande mbili zilizokuwa zinavutana.
Alisema baada ya kukutana na wahusika, amebaini kuwa kukosekana kwa mawasiliano yanayozingatia kanuni ndicho kilikuwa kilio cha kujengeka kwa hisia ambazo zilikuwa zinachangia mtafaruku.
"Hakuna hata mtu aliyeeleza chanzo, tukabaini kuwa tatizo lilikuwa ni kukosa mawasiliano kati ya wilaya na mkoa, na hili lilichangia hisia zaidi kuliko jambo lenyewe. Baada ya kukutana na pande zote, sasa naweza kutangaza kuwa tatizo hilo limekwisha na sasa wanaungana kuimarisha chama," aliongeza.
Aidha, Wasira alikiri kuwa mtafaruku huo ni matokeo ya kushindwa katika jimbo la Arusha Mjini katika uchaguzi wa mwaka 2010 na kuwa vijana walikuwa na maoni tofauti kutokana na kushindwa huko.
Katika uchaguzi huo, jimbo hilo lilichukuliwa na Godbless Lema wa Chadema.
Naye Katibu Mkuu wa UVCCM, Martin Shigela, alisema mgogoro uliokuwa Arusha, haukuhusu mgombea urais mwaka 2015 na kuwa taratibu za kumpata zinajulikana ndani ya chama.
" UVCCM haina mgombea urais kwa ajili ya uchaguzi ujao, utaratibu ndani ya chama uko wazi, muda ukifika watu watatangaza nia na sisi tutampigia debe mtu atakayepitishwa na chama na si vinginevyo," alisema Shigela.
Ziara ya Wasira ilimkutanisha na UVCCM wilaya ya Arusha, wajumbe wa Baraza la Vijana la Wilaya ya Arusha Mjini, Baraza la Mkoa, Kamati ya Siasa na Baraza la Wazee katika vikao vilivyohudhuriwa pia na Katibu wa CCM wa Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda.
Katika siku za karibuni, Arusha iligeuka chimbuko la vita vya maneno miongoni mwa makada wa CCM, hulka ambayo ilisambaa hadi kwa viongozi wa kitaifa wa chama hicho hasa kutokana na falsafa ya kujivua gamba.
Awali, mgogoro ulikuwa baina ya baadhi ya vijana wa wilaya na mkoa wa Arusha na Katibu wa CCM wa Mkoa, Chatanda, ambaye pamoja na viongozi na makada wengine, walituhumiwa kwa kilichoelezwa kuwa ni kusababisha chama hicho kipoteze ubunge wa Arusha Mjini.