Japhari Shabani (RIP)
R I P
- Jan 16, 2007
- 721
- 176
Kabla ya kuanzisha forums yao nawashauri yafuatayo:Mkuu NM, waambie wajivue gamba kwanza kabla ya kuanzisha hiyo Mapinduzi Forum ambayo itapata wanachama wenye gamba tu na haitakuwa na umaarufu kama wa JF. Njemba hizi zinahaha ile mbaya kutafuta umaarufu wasiokuwa nao.
Wakarabati magazeti na radio zao kama uhuru yawe na mvuto na sio kufungia maandazi na radio kua kituoa ambapo watu wanafungulia kusikiliza utabiri wa hali ya hewa na saa na badala yake yazungumzie matatizo na kero za wananchi na sio kuwalinda viongozi wa CCM na serikali na kuficha maovu yao.Waruhusu mijadala na midahalo huru ISIOCHAKACHULIWA itakaowashirikisha viongozi wake pia,waheshimu mawazo ya kila mtu bila kujali kabila lake,dini,jinsia ushabiki aunafasi yake katika chama au jamii na chama cha CCM kiondoe thana ya kua watatawala maisha na viongozi wake ni miungu watu (Hawakosei na hawapashwi kukosolewa)Waruhusu midahalo katika vyombo vyao vya habari kwa kushikisha pande zote(WASIKIMBIE MIDAHALO)Wakifanya hivyo watafanikiwa au hawatakua na umuhimu wa kuanzisha forum yao bali kujiunga"JAMIIFORUMS"Wakianzisha forums yao kwa kukiuka hayo niyoyataja na mengineyo forum yao haitatofautiana na vikao vya CCM .
Kuhusu mamluki na viwavi waliomwagwa Jamiiforums jia pekee ya kupambana nao ni KUWAIGNORE wanapoleta threads na posts za kipuuzi na kupambana nao kwa hoja wanapoleta hoja muafaka.