nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[h=2][/h]IJUMAA, SEPTEMBA 21, 2012 06:10 NA MWANDISHI WETU, BUSEGA
HEKAHEKA za uchaguzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), zimeanza kuchukua sura mpya, ambapo Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM), Wilaya ya Busega mkoani Simiyu, kutoa tamko la kuitahadharisha Halmashauri Kuu (NEC), isilogwe ikakata majina ya baadhi ya wagombea akiwamo Dk. Raphael Chegeni.
Kutokana na hali hiyo, wameitaka NEC itende haki kwa kuteua majina ya wagombea wenye sifa na uwezo mkubwa wa kukijenga chama hicho tawala.
Walisema iwapo majina hayo likiwamo la Dk. Chegeni yatakatwa, wapo tayari kuchukuwa uamuzi mgumu.
Akizungumza mjini Nyashimo jana, Mwenyekiti wa UVCCM wilayani Busega, Samuel Ngofilo, alisema: UVCCM imebaini kuwapo kwa njama hizo chafu zinazolenga kumchafua Dk. Chegeni ili asipitishwe na NEC kugombea wilaya hii ya Busega.
Alisema kuna mbinu chafu zimeanza kufanywa na baadhi ya viongozi wa CCM wilayani humo, akiwamo Mbunge wa Busega, Dk. Titus Kamani, anayedaiwa kuandika barua kwenda makao makuu ya CCM Mkoa wa Mwanza, akiomba jina la Dk. Chegeni lisipitishwe na kamati ya siasa, kwa sababu ambazo hazijafahamika.
Aliwataja wagombea wengine watatu wanaogombea Unec wilayani Busega, kuwa ni pamoja na Amos Onesmo, Kashen Fanuel na Miknes Mahela na nafasi hiyo iliombwa na wana CCM wanne akiwamo Dk. Chegeni, anayedaiwa jina lake kukatwa na Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Mwanza.
Hapa Busega kuna baadhi ya watu wameanza kutengeneza fitina na njama chafu na kupakana matope. Njama hizi chafu zimelenga kupanga safu za watu wanaowataka wao.
Dk. Chegeni ambaye pia ni Kamanda wa Vijana wa Wilaya hii ya Busega, ndiye anayesakamwa na kuundiwa njama hizi mbaya za kutaka asipitishwe kugombea Unec katika wilaya yetu hii ya Busega.
Tunachotaka sisi vijana wa Busega NEC itende haki. Isimuonee Dk. Chegeni wala mtu mwingine yeyote mwenye sifa za kiuongozi, alisema Ngofilo.
Alisema kwa kutambua uchapakazi, ushawishi na uhodari wa kujenga na kutetea hoja kwa maslahi ya chama na jamii alionao Chegeni, ndiyo sababu kuu kilichowasukuma kumchukulia fomu ya kugombea Unec, hivyo kama NEC itakata jina hilo, wapo tayari kuchukuwa uamuzi mgumu.
Hatuwezi kusema kama tutaenda Chadema au la, maana bado mapema mno. Ila tunachotaka chama kisituletee watu wasiokubalika ndani ya chama na kwa wananchi wenyewe, alisema Ngofilo.
Aidha, alisema wanategemea wajumbe wa NEC hawatakubali njama hizo chafu zipenye, badala yake watatumia busara na hekima zao kurudisha majina ya wana CCM wenye sifa na uwezo wa kufanya kazi za kijamii.
Kwa mfano, mbunge wetu wa Busega, Dk. Kamani kuna barua kuandika na kuituma kwenda kwa Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza. Barua hiyo anaomba jina la Dk. Chegeni lisipitishwe kwenda ngazi ya Taifa.
Kuna maana gani kumchafua mtu? Mtu anayefanya hivyo anakitakia nini chama chetu?. Tunachotaka ni kujenga chama chetu kwa kuwa na viongozi makini, hodari na imara katika kupigania maendeleo ya chama na wananchi wetu. Tunaisihi NEC ipuuze uzushi wa aina yoyote na ilete majina ya watu wanaokubalika kijamii, alisema Nyofilo.
MTANZANIA lilipomtafuta Dk. Kamani, hakupatikana kuzungumzia tuhuma hizo.