UVCCM acheni kulalamika, ni matokeo ya tamaa zenu!

IsangulaKG

JF-Expert Member
Oct 14, 2010
706
385
Kwanza niseme wazi mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa na hiyo haininyimi haki ya kuchangia mijadala inayoendelea.

Uchaguzi wa UVCCM kama ilivyo chaguzi nyingi naamini umefanyika kwa kupiga kura, kwa maana ya kwamba kila mjumbe alipewa karatasi na kalamu (aghalabu naamini hivyo) na kupewa nafasi ya usiri wa kupiga kura.

Sasa basi kama hilo ndilo lililofanyika, napata wasiwasi na watu wanaolalamika kuwa viongozi waliochaguliwa wamechaguliwa kwa rushwa.

Swali la msingi ni je, kura zilipigwa kwa kunyoosha mikono ili wale waliopewa rushwa waone aibu kwa fedha walizokula na wapige kura kumchagua aliye wahonga? Kama sivyo hivyo, je wakati wa kupiga kura kuna mtu alimsimamia kila mpiga kura ili kuona anampigia kura aliyemhonga? Swali lingine ni je chumba cha mkutano kilikuwa na mitambo maalumu ya kung'amua nani amemchagua nani? Kama mambo haya matatu hayajitokeza na kama kijana amepewa rushwa na yeye kwa UJINGA na TAMAA zake akampigia kura yule aliyempa rushwa then HAMPASWI kulalamika.

Binafsi, naona utamaduni wa rushwa katika chaguzi hasa za CCM umezoeleka, ipi njia nzuri ya kuwakomoa watoa rushwa? Moja ni Kuwa na wagombea imara wasafi kimaadili na kwa usafi wao wafanyike mvuto kwa wapiga kura, hiyo ni hatua ya kwanza swali je UVCCM kuna msafi kimaadili? Hatua ya pili, kwa kuwa utamaduni wa kupokea rushwa umezoeleka na ni kama vile hauwezi kudhibitika katika chaguzi za CCM, then ni kuunda mifumo mizuri ya usiri mkubwa katika kupiga kura na Mwisho ni kutompigia kura yule aliyekupa rushwa.....kwa kumchagua yule aliyemsafi kimaadili. Kamwe hakuna atakayetamani kutoa rushwa na hakuna atakayekuja kukudai rushwa aliyokupa!

Hoja yangu hii imejikita katika ukweli kwamba kupokea rushwa ktk chaguzi za CCM imekuwa ni kawaida, na kwa kuwa mikakati ya kuzuia watu kupokea rushwa pia haipo au imeshindikanika kutekelezeka basi tudeal na MAAMUZI ya mpokea rushwa.

Mimi kama mtaalamu wa kuandaa mikakati mingi ,naamini kuwa kuna ngazi (levels) nyingi za kutatua tatizo na kama ngazi moja ikishindikana ( kama kukemea na kauli za viongozi au uwajibishwaji ulivyoshindwa), na watu wameshindwa kuacha kutoa na kupokea rushwa..ni wakati sasa wa kuangalia ngazi ya watu kufanya maamuzi wakati wa kupiga kura ili mtu asichague kwa kusukumwa na vijisenti alivyopewa au alivyoahidiwa....

Mwisho nasema, kwa kuwa usiri wa kupiga kura ulikuwapo (ninavyoamini) na bado mtu akapiga kura kwa kusukumwa na nguvu ya rushwa...then vijana msilalamike kwa kushwa tamaa zentu zimewafanya mshindwe kukataa kupokea rushwa na mmeshindwa hata kutompigia kura aliyetoa rushwa mlipopewa nafasi ya usiri kufanya hivyo!

Njaa na tamaa zenu
Mawazo na akili yenu
Mkiwa wenyewe sehemu
mkapiga kura zenu
Chagua wezi wenzenu

Mwalalamika nini?

Mnatangaza uasi kumtishia nani?
Hakumbuki baba ridhiwani
Wagonjwa kuweka rehani
Alipotamka hadharani
Madaktari ondokeni?

Nanyi basi ondokeni...
 
Mi nakuunga mkono mleta mada. Ila mi naomba kuuliza hivi hao magamba vijana wameamua rasmi kuvaa gwanda?. Mbona wanapenda sn kuiga?. Maana ukiwaangalia mpaka inatia kinyaa. Walitukana gwanda la cdm, kumbe wanalitaman.Angalia walivyokuwa dodoma.
 
hata hao wanaolalamika wa kambi ya makonda pia walipokea rushwa toka kwa riz one, ni upumbavu tu vijana kutumiwa namna hiyo, UVCCM ni tanuru la kuivisha wala rushwa wakubwa wa siku zijazo
 
Once you find Symptoms of CCMonia sicjness, immediately swallow CHADEMAquine tablets you will be cured. CHADEMAquine tablets are available all over the Country. If illness persist consult Dr. Slaa. Do not wast you time do it now!
 
Kwanza niseme wazi mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa na hiyo haininyimi haki ya kuchangia mijadala inayoendelea.

Uchaguzi wa UVCCM kama ilivyo chaguzi nyingi naamini umefanyika kwa kupiga kura, kwa maana ya kwamba kila mjumbe alipewa karatasi na kalamu (aghalabu naamini hivyo) na kupewa nafasi ya usiri wa kupiga kura.

Sasa basi kama hilo ndilo lililofanyika, napata wasiwasi na watu wanaolalamika kuwa viongozi waliochaguliwa wamechaguliwa kwa rushwa.

Swali la msingi ni je, kura zilipigwa kwa kunyoosha mikono ili wale waliopewa rushwa waone aibu kwa fedha walizokula na wapige kura kumchagua aliye wahonga? Kama sivyo hivyo, je wakati wa kupiga kura kuna mtu alimsimamia kila mpiga kura ili kuona anampigia kura aliyemhonga? Swali lingine ni je chumba cha mkutano kilikuwa na mitambo maalumu ya kung'amua nani amemchagua nani? Kama mambo haya matatu hayajitokeza na kama kijana amepewa rushwa na yeye kwa UJINGA na TAMAA zake akampigia kura yule aliyempa rushwa then HAMPASWI kulalamika.

Binafsi, naona utamaduni wa rushwa katika chaguzi hasa za CCM umezoeleka, ipi njia nzuri ya kuwakomoa watoa rushwa? Moja ni Kuwa na wagombea imara wasafi kimaadili na kwa usafi wao wafanyike mvuto kwa wapiga kura, hiyo ni hatua ya kwanza swali je UVCCM kuna msafi kimaadili? Hatua ya pili, kwa kuwa utamaduni wa kupokea rushwa umezoeleka na ni kama vile hauwezi kudhibitika katika chaguzi za CCM, then ni kuunda mifumo mizuri ya usiri mkubwa katika kupiga kura na Mwisho ni kutompigia kura yule aliyekupa rushwa.....kwa kumchagua yule aliyemsafi kimaadili. Kamwe hakuna atakayetamani kutoa rushwa na hakuna atakayekuja kukudai rushwa aliyokupa!

Hoja yangu hii imejikita katika ukweli kwamba kupokea rushwa ktk chaguzi za CCM imekuwa ni kawaida, na kwa kuwa mikakati ya kuzuia watu kupokea rushwa pia haipo au imeshindikanika kutekelezeka basi tudeal na MAAMUZI ya mpokea rushwa.

Mimi kama mtaalamu wa kuandaa mikakati mingi ,naamini kuwa kuna ngazi (levels) nyingi za kutatua tatizo na kama ngazi moja ikishindikana ( kama kukemea na kauli za viongozi au uwajibishwaji ulivyoshindwa), na watu wameshindwa kuacha kutoa na kupokea rushwa..ni wakati sasa wa kuangalia ngazi ya watu kufanya maamuzi wakati wa kupiga kura ili mtu asichague kwa kusukumwa na vijisenti alivyopewa au alivyoahidiwa....

Mwisho nasema, kwa kuwa usiri wa kupiga kura ulikuwapo (ninavyoamini) na bado mtu akapiga kura kwa kusukumwa na nguvu ya rushwa...then vijana msilalamike kwa kushwa tamaa zentu zimewafanya mshindwe kukataa kupokea rushwa na mmeshindwa hata kutompigia kura aliyetoa rushwa mlipopewa nafasi ya usiri kufanya hivyo!

Njaa na tamaa zenu
Mawazo na akili yenu
Mkiwa wenyewe sehemu
mkapiga kura zenu
Chagua wezi wenzenu

Mwalalamika nini?

Mnatangaza uasi kumtishia nani?
Hakumbuki baba ridhiwani
Wagonjwa kuweka rehani
Alipotamka hadharani
Madaktari ondokeni?

Nanyi basi ondokeni...
Wap................................mbavu sana hao,waacha wakione cha moto!Magamba yana wenyewe!
 
Back
Top Bottom